< Sefania 3 >
1 Ole kwa mji ulioasi! Mji wenye vurugu umenajisiwa.
Malheur, cité provocatrice et rachetée, colombe!
2 Haukuisikiliza sauti ya Mungu, wala haukupokea masahihisho kutoka kwa Yahwe. Hakumtumaini Yahwe na hatamkaribia Mungu wake.
Elle n’a pas écouté la voix, et elle n’a pas reçu les instructions; elle ne s’est pas confiée au Seigneur, elle ne s’est pas approchée de son Dieu.
3 Wafalme wao ni simba wanaounguruma miongoni mwao. Waamuzi wao ni mbwa mwitu wa jioni wasiobakiza kitu ambacho kitakuwa kimemung'unywa asubuhi yake.
Ses princes au milieu d’elle sont comme des lions rugissants; ses juges, loups du soir, ne laissaient rien pour le matin.
4 Manabii wake wanakiburi na wanaume wasaliti. Makuhani wake wamepanajisi mahali patakatifu na wameifanyia vurugu sheria.
Ses prophètes sont insensés et sans foi, ses prêtres ont souillé les choses saintes et ont agi injustement contre la loi.
5 Yahwe ni mwenye haki miongoni mwao. Hawezi kufanya makosa. Kila asubuhi husimamia haki yake! Haitafichika nuruni, hata hivyo watu wasio wenye haki hawajui kuona aibu.
Le Seigneur, juste au milieu d’elle, ne commettra pas l’iniquité; chaque matin il produira sont jugement à la lumière, et ne se cachera pas; mais le peuple inique n’a pas connu sa confusion.
6 Nimeyaharibu mataifa; ngome zao zimeharibiwa. Nimeifanya mitaa yao magofu, hivyo hakuna hata mmoja anayepitia kwake. Miji yao imeharibiwa kwa hiyo hakuna mtu anayeikaa.
J’ai exterminé les nations, et leurs angles ont été détruits; j’ai rendu leurs voies désertes, en sorte qu’il n’y a personne qui y passe; leurs cités ont été désolées, pas un homme n’y restant, et nul n’y habitant.
7 Nikasema, 'Hakika mtaniogopa mimi. Pokeeni masahihisho na msikatiliwe mbali kutoka kwenye miji yenu kwa yote yale niliyokuwa nimeyapanga kuyafanya kwenu.' Lakini walikuwa na shauku kuanza kila siku kwa kuharibu matendo yao yote.
J’ai dit: Mais cependant tu me craindras, tu recevras les instructions; et ta demeure ne périra pas à cause de toutes les choses pour lesquelles je l’ai visitée; mais cependant se levant au point du jour, ils ont corrompu toutes leurs pensées.
8 Kwa hiyo ningojeni - hili ni tamko la Yahwe - mpaka siku ambayo nitainuka kwa ajili ya waathirika. Uaamuzi wangu nikuwakusanya mataifa, kuzikusanya falme, na kumwaga juu yao hasira yangu, uchungu wangu wote mkali, hivyo nchi yote itamezwa kwa moto wa hasira yangu.
C’est pourquoi, attends-moi, dit le Seigneur, au jour de ma résurrection à venir; parce que ma résolution est de rassembler les nations, et de réunir les royaumes et de répandre sur eux mon indignation et toute la colère de ma fureur; car par le feu de ma colère toute la terre sera dévorée.
9 Ndipo nitawapa midomo safi watu, kuwaita wote kwa jina la Bwana kunitumikia wakisimama bega kwa bega.
Parce que alors je donnerai aux peuples une lèvre choisie, afin que tous invoquent le nom du Seigneur, et qu’ils le servent d’un commun accord.
10 Kutoka ng'ambo ya mto Ethiopia waniabuduo - watu wangu waliotawanyika - wataleta dhabihu kwa sababu yangu.
D’au-delà des fleuves d’Ethiopie viendront mes suppliants, les fils de mes dispersés m’apporteront un présent.
11 Katika siku hiyo hamtawekwa kwenye woga kwa matendo yenu yote ambayo mmeyafanya dhidi yangu, tangu wakati ule nitaondoa kutoka kwenu wale waliosherehekea fahari yenu, na kwa sababu hamtakuwa na muda mrefu kufanya majivuno juu ya mlima wangu mtakatifu.
En ce jour-là, tu ne seras pas confondue pour toutes les inventions par lesquelles tu as prévariqué contre moi; parce que j’enlèverai du milieu de toi les flatteurs fastueux de ton orgueil; tu ne t’enorgueilliras plus désormais sur ma montagne sainte.
12 Lakini nitawaacha kama wa chini zaidi na watu masikini, na mtapata kimbilio katika jina la Yahwe.
Et je laisserai au milieu de toi un peuple pauvre et indigent, et ils espéreront dans le nom du Seigneur.
13 Mkazi wa Israeli si muda mrefu hatafanya udhalimu au kusema uongo, na hakuna ulimi wa udanganyifu utakaoonekana mdomoni mwao; hivyo watalisha na kulala chini, na hakuna hata mmoja atakayewafanya kuogopa.”
Les restes d’Israël ne commettront pas l’iniquité et ne parleront pas mensonge; il ne se trouvera pas dans leur bouche de langue trompeuse; parce qu’eux-mêmes paîtront, et se coucheront, et il n’y aura personne qui les épouvante.
14 Imba, binti Sayuni! Piga kelele, Israeli. Ufurahi na kushangilia kwa moyo wako wote, binti wa Yerusalemu.
Loue, fille de Sion; jubile, Israël; réjouis-toi, et exulte en tout ton cœur, fille de Jérusalem.
15 Yahwe ameiondoa hukumu yako; amewafukuzia mbali adui zako! Yahwe ni mfalme wa Israeli miongoni mwenu. Kamwe hamtamwogopa tena mwovu!
Le Seigneur a effacé ton arrêt, il a éloigné tes ennemis; le roi d’Israël, le Seigneur, est au milieu de toi; tu ne craindras plus le malheur.
16 Katika siku hizo watasema kwa Yerusalemi, “Usiogope, Sayuni. Usiiache mikono yako ilegee.
En ce jour-là, on dira à Jérusalem: Ne crains pas; Sion, que tes mains ne s’affaiblissent point.
17 Yahwe Mungu wako yuko katikati yenu, mwenye nguvu wa kuwaokoa. Atasherehekea juu yenu na kwa furaha atakuwa kimya juu yenu kwa upendo wake. Atakuwa na furaha juu yenu na atashangilia kwa furaha,
Le Seigneur, ton Dieu, le Dieu fort sera au milieu de toi; lui-même te sauvera; il se réjouira de joie en toi, il se reposera en ton amour, il exultera en toi, au milieu des louanges.
18 katika siku maalumu ya sherehe. Nitaondoa maafa kutoka kwenu; si muda mrefu hamtabeba aibu kwa ajili yake.
Les hommes légers qui s’étaient écartés de la loi, je les rassemblerai, parce qu’ils t’appartenaient, afin que tu n’aies plus en eux un sujet d’opprobre.
19 Tazama, Niko tayari kuwashughulikia watesi wenu wote. Katika wakati ule, Nitawaokoa waliolemaa na kuwakusanya waliotupiliwa mbali. Nitawafanya kuwa sifa, na nitaibadilisha aibu yao iwe sifa katika dunia yote.
Voici que moi, je tuerai tous ceux qui t’ont affligée en ce temps-là, et je sauverai celle qui boitait, et celle qui avait été rejetée, je la ramènerai; je les établirai en louange et en nom dans tout pays où ils étaient couverts de confusion.
20 Katika wakati ule nitawaongoza; katika wakati ule nitawakusanya pamoja. Nitawafanya mataifa yote ya dunia kuwaheshimu na kuwasifu, wakati mtakapoona hivyo, Nitakuwa nimewarudisha”, asema Yahwe.
En ce temps-là, je vous ramènerai, et dans ce temps-là, je vous rassemblerai; car je vous établirai en nom et en louange devant tous les peuples de la terre, lorsque j’aurai changé votre captivité devant vos yeux, dit le Seigneur.