< Sefania 3 >
1 Ole kwa mji ulioasi! Mji wenye vurugu umenajisiwa.
Malheur à la réfractaire et souillée, à la cité qui opprime!
2 Haukuisikiliza sauti ya Mungu, wala haukupokea masahihisho kutoka kwa Yahwe. Hakumtumaini Yahwe na hatamkaribia Mungu wake.
Elle n'est docile à aucune voix, ne reçoit pas instruction, en l'Éternel elle ne se confie pas, de son Dieu elle ne s'approche pas.
3 Wafalme wao ni simba wanaounguruma miongoni mwao. Waamuzi wao ni mbwa mwitu wa jioni wasiobakiza kitu ambacho kitakuwa kimemung'unywa asubuhi yake.
Ses princes dans son sein sont des lions rugissants, ses juges des loups du soir, ils ne réservent rien pour le lendemain.
4 Manabii wake wanakiburi na wanaume wasaliti. Makuhani wake wamepanajisi mahali patakatifu na wameifanyia vurugu sheria.
Ses prophètes sont des fanfarons, des hommes perfides, ses sacrificateurs profanent le sanctuaire, violent la loi.
5 Yahwe ni mwenye haki miongoni mwao. Hawezi kufanya makosa. Kila asubuhi husimamia haki yake! Haitafichika nuruni, hata hivyo watu wasio wenye haki hawajui kuona aibu.
L'Éternel est juste au milieu d'elle, Il ne fait rien d'injuste, chaque matin Il produit au jour ses lois, Il n'y manque point; mais le méchant ne connaît point de pudeur.
6 Nimeyaharibu mataifa; ngome zao zimeharibiwa. Nimeifanya mitaa yao magofu, hivyo hakuna hata mmoja anayepitia kwake. Miji yao imeharibiwa kwa hiyo hakuna mtu anayeikaa.
J'ai exterminé des peuples; leurs tours ont été dévastées; j'ai désolé leurs rues, tellement qu'il n'y a plus de passants; leurs villes ont été détruites, dépeuplées, privées d'habitants.
7 Nikasema, 'Hakika mtaniogopa mimi. Pokeeni masahihisho na msikatiliwe mbali kutoka kwenye miji yenu kwa yote yale niliyokuwa nimeyapanga kuyafanya kwenu.' Lakini walikuwa na shauku kuanza kila siku kwa kuharibu matendo yao yote.
J'ai dit: « Pourvu que tu me craignes, que tu reçoives instruction, » la ruine de sa demeure n'arriverait pas, tout le châtiment que je lui avais destiné. Mais dès le matin ils ont perverti toutes leurs œuvres.
8 Kwa hiyo ningojeni - hili ni tamko la Yahwe - mpaka siku ambayo nitainuka kwa ajili ya waathirika. Uaamuzi wangu nikuwakusanya mataifa, kuzikusanya falme, na kumwaga juu yao hasira yangu, uchungu wangu wote mkali, hivyo nchi yote itamezwa kwa moto wa hasira yangu.
Aussi attendez-moi, dit l'Éternel, pour le jour où je me lèverai pour faire du butin; car j'ai arrêté de rassembler les peuples, de réunir les royaumes pour verser sur eux ma fureur, toute l'ardeur de ma colère, car au feu de mon courroux toute la terre sera consumée.
9 Ndipo nitawapa midomo safi watu, kuwaita wote kwa jina la Bwana kunitumikia wakisimama bega kwa bega.
Car alors je donnerai aux peuples des lèvres nouvelles, afin qu'ils invoquent tous le nom de l'Éternel et le servent unanimement.
10 Kutoka ng'ambo ya mto Ethiopia waniabuduo - watu wangu waliotawanyika - wataleta dhabihu kwa sababu yangu.
De par-delà les fleuves de l'Ethiopie mes adorateurs, les enfants de mes dispersés, apporteront mes offrandes.
11 Katika siku hiyo hamtawekwa kwenye woga kwa matendo yenu yote ambayo mmeyafanya dhidi yangu, tangu wakati ule nitaondoa kutoka kwenu wale waliosherehekea fahari yenu, na kwa sababu hamtakuwa na muda mrefu kufanya majivuno juu ya mlima wangu mtakatifu.
En ce temps-là tu n'auras plus à rougir de tous les faits dont tu t'es rendue coupable envers moi, car alors j'éloignerai de toi tes insolents triomphants, et désormais tu ne t'enorgueilliras plus sur ma sainte montagne.
12 Lakini nitawaacha kama wa chini zaidi na watu masikini, na mtapata kimbilio katika jina la Yahwe.
Et je laisserai au milieu de toi un peuple pauvre et chétif, qui se confie dans le nom de l'Éternel.
13 Mkazi wa Israeli si muda mrefu hatafanya udhalimu au kusema uongo, na hakuna ulimi wa udanganyifu utakaoonekana mdomoni mwao; hivyo watalisha na kulala chini, na hakuna hata mmoja atakayewafanya kuogopa.”
Les restes d'Israël ne commettront pas l'iniquité ni ne proféreront le mensonge, et il ne se trouvera dans leur bouche point de langue trompeuse, mais on les fera paître, et ils reposeront sans être troublés.
14 Imba, binti Sayuni! Piga kelele, Israeli. Ufurahi na kushangilia kwa moyo wako wote, binti wa Yerusalemu.
Jubile, fille de Sion! chante victoire, Israël! livre à la joie et à l'allégresse ton cœur tout entier, fille de Jérusalem!
15 Yahwe ameiondoa hukumu yako; amewafukuzia mbali adui zako! Yahwe ni mfalme wa Israeli miongoni mwenu. Kamwe hamtamwogopa tena mwovu!
L'Éternel retire la sentence portée contre toi, Il éloigne ton ennemi: le Roi d'Israël au milieu de toi, c'est l'Éternel; désormais tu ne connaîtras plus les maux.
16 Katika siku hizo watasema kwa Yerusalemi, “Usiogope, Sayuni. Usiiache mikono yako ilegee.
En ce jour on dira à Jérusalem: Ne crains point! Sion, que tes bras ne défaillent point!
17 Yahwe Mungu wako yuko katikati yenu, mwenye nguvu wa kuwaokoa. Atasherehekea juu yenu na kwa furaha atakuwa kimya juu yenu kwa upendo wake. Atakuwa na furaha juu yenu na atashangilia kwa furaha,
L'Éternel, ton Dieu, est au milieu de toi, héros sauveur; tu feras sa joie et ses délices; dans son amour Il gardera le silence, tu feras son allégresse et son ravissement.
18 katika siku maalumu ya sherehe. Nitaondoa maafa kutoka kwenu; si muda mrefu hamtabeba aibu kwa ajili yake.
Je recueille ceux qui s'attristent éloignés de l'assemblée; ils t'appartiennent, ils sont sous le poids de l'opprobre.
19 Tazama, Niko tayari kuwashughulikia watesi wenu wote. Katika wakati ule, Nitawaokoa waliolemaa na kuwakusanya waliotupiliwa mbali. Nitawafanya kuwa sifa, na nitaibadilisha aibu yao iwe sifa katika dunia yote.
Voici, j'aurai affaire à tous tes oppresseurs en ce temps-là, et je sauverai ce qui boite et recueillerai ce qui sera dispersé, et leur ferai obtenir de la louange et de la gloire dans tous les pays où ils subissent l'opprobre.
20 Katika wakati ule nitawaongoza; katika wakati ule nitawakusanya pamoja. Nitawafanya mataifa yote ya dunia kuwaheshimu na kuwasifu, wakati mtakapoona hivyo, Nitakuwa nimewarudisha”, asema Yahwe.
Dans ce temps-là je vous ramènerai, et en ce même temps je vous recueillerai, car je vous rendrai célèbres et illustres auprès de tous les peuples de la terre, en ramenant vos captifs, sous vos yeux, dit l'Éternel.