< Sefania 3 >
1 Ole kwa mji ulioasi! Mji wenye vurugu umenajisiwa.
Woe to her that is filthie and polluted, to the robbing citie.
2 Haukuisikiliza sauti ya Mungu, wala haukupokea masahihisho kutoka kwa Yahwe. Hakumtumaini Yahwe na hatamkaribia Mungu wake.
She heard not the voyce: she receiued not correction: she trusted not in the Lord: she drew not neere to her God.
3 Wafalme wao ni simba wanaounguruma miongoni mwao. Waamuzi wao ni mbwa mwitu wa jioni wasiobakiza kitu ambacho kitakuwa kimemung'unywa asubuhi yake.
Her princes within her are as roaring lyons: her iudges are as wolues in the euening, which leaue not the bones till the morow.
4 Manabii wake wanakiburi na wanaume wasaliti. Makuhani wake wamepanajisi mahali patakatifu na wameifanyia vurugu sheria.
Her prophets are light, and wicked persons: her priests haue polluted the Sanctuarie: they haue wrested the Lawe.
5 Yahwe ni mwenye haki miongoni mwao. Hawezi kufanya makosa. Kila asubuhi husimamia haki yake! Haitafichika nuruni, hata hivyo watu wasio wenye haki hawajui kuona aibu.
The iust Lord is in the middes thereof: he will doe none iniquitie: euery morning doeth hee bring his iudgement to light, he faileth not: but the wicked will not learne to be ashamed.
6 Nimeyaharibu mataifa; ngome zao zimeharibiwa. Nimeifanya mitaa yao magofu, hivyo hakuna hata mmoja anayepitia kwake. Miji yao imeharibiwa kwa hiyo hakuna mtu anayeikaa.
I haue cut off the nations: their towres are desolate: I haue made their streetes waste, that none shall passe by: their cities are destroyed without man and without inhabitant.
7 Nikasema, 'Hakika mtaniogopa mimi. Pokeeni masahihisho na msikatiliwe mbali kutoka kwenye miji yenu kwa yote yale niliyokuwa nimeyapanga kuyafanya kwenu.' Lakini walikuwa na shauku kuanza kila siku kwa kuharibu matendo yao yote.
I said, Surely thou wilt feare me: thou wilt receiue instruction: so their dwelling shoulde not be destroyed howsoeuer I visited them, but they rose earely and corrupted all their workes.
8 Kwa hiyo ningojeni - hili ni tamko la Yahwe - mpaka siku ambayo nitainuka kwa ajili ya waathirika. Uaamuzi wangu nikuwakusanya mataifa, kuzikusanya falme, na kumwaga juu yao hasira yangu, uchungu wangu wote mkali, hivyo nchi yote itamezwa kwa moto wa hasira yangu.
Therefore wait ye vpon me, saith the Lord, vntill the day that I rise vp to the praye: for I am determined to gather the nations, and that I will assemble the kingdomes to powre vpon them mine indignation, euen all my fierce wrath: for all the earth shall be deuoured with the fire of my ielousie.
9 Ndipo nitawapa midomo safi watu, kuwaita wote kwa jina la Bwana kunitumikia wakisimama bega kwa bega.
Surely then will I turne to the people a pure language, that they may all call vpon the Name of the Lord, to serue him with one cosent.
10 Kutoka ng'ambo ya mto Ethiopia waniabuduo - watu wangu waliotawanyika - wataleta dhabihu kwa sababu yangu.
From beyonde the riuers of Ethiopia, the daughter of my dispersed, praying vnto me, shall bring me an offering.
11 Katika siku hiyo hamtawekwa kwenye woga kwa matendo yenu yote ambayo mmeyafanya dhidi yangu, tangu wakati ule nitaondoa kutoka kwenu wale waliosherehekea fahari yenu, na kwa sababu hamtakuwa na muda mrefu kufanya majivuno juu ya mlima wangu mtakatifu.
In that day shalt thou not be ashamed for all thy workes, wherein thou hast transgressed against mee: for then I will take away out of the middes of thee them that reioyce of thy pride, and thou shalt no more be proude of mine holy Mountaine.
12 Lakini nitawaacha kama wa chini zaidi na watu masikini, na mtapata kimbilio katika jina la Yahwe.
Then will I leaue in the middes of thee an humble and poore people: and they shall trust in the Name of the Lord.
13 Mkazi wa Israeli si muda mrefu hatafanya udhalimu au kusema uongo, na hakuna ulimi wa udanganyifu utakaoonekana mdomoni mwao; hivyo watalisha na kulala chini, na hakuna hata mmoja atakayewafanya kuogopa.”
The remnant of Israel shall do none iniquitie, nor speake lies: neither shall a deceitful tongue be found in their mouth: for they shalbe fed, and lie downe, and none shall make them afraide.
14 Imba, binti Sayuni! Piga kelele, Israeli. Ufurahi na kushangilia kwa moyo wako wote, binti wa Yerusalemu.
Reioyce, O daughter Zion: be ye ioyfull, O Israel: be glad and reioyce with all thine heart, O daughter Ierusalem.
15 Yahwe ameiondoa hukumu yako; amewafukuzia mbali adui zako! Yahwe ni mfalme wa Israeli miongoni mwenu. Kamwe hamtamwogopa tena mwovu!
The Lord hath taken away thy iudgements: hee hath cast out thine enemie: the King of Israel, euen the Lord is in the middes of thee: thou shalt see no more euill.
16 Katika siku hizo watasema kwa Yerusalemi, “Usiogope, Sayuni. Usiiache mikono yako ilegee.
In that day it shalbe said to Ierusalem, Feare thou not, O Zion: let not thine handes be faint.
17 Yahwe Mungu wako yuko katikati yenu, mwenye nguvu wa kuwaokoa. Atasherehekea juu yenu na kwa furaha atakuwa kimya juu yenu kwa upendo wake. Atakuwa na furaha juu yenu na atashangilia kwa furaha,
The Lord thy God in the middes of thee is mightie: hee will saue, hee will reioyce ouer thee with ioye: he will quiet himselfe in his loue: he will reioyce ouer thee with ioy.
18 katika siku maalumu ya sherehe. Nitaondoa maafa kutoka kwenu; si muda mrefu hamtabeba aibu kwa ajili yake.
After a certaine time will I gather the afflicted that were of thee, and them that bare the reproch for it.
19 Tazama, Niko tayari kuwashughulikia watesi wenu wote. Katika wakati ule, Nitawaokoa waliolemaa na kuwakusanya waliotupiliwa mbali. Nitawafanya kuwa sifa, na nitaibadilisha aibu yao iwe sifa katika dunia yote.
Beholde, at that time I will bruise all that afflict thee, and I will saue her that halteth, and gather her that was cast out, and I will get them praise and fame in all the landes of their shame.
20 Katika wakati ule nitawaongoza; katika wakati ule nitawakusanya pamoja. Nitawafanya mataifa yote ya dunia kuwaheshimu na kuwasifu, wakati mtakapoona hivyo, Nitakuwa nimewarudisha”, asema Yahwe.
At that time wil I bring you againe, and then wil I gather you: for I wil giue you a name and a praise among all people of the earth, when I turne backe your captiuitie before your eyes, saith the Lord.