< Sefania 3 >

1 Ole kwa mji ulioasi! Mji wenye vurugu umenajisiwa.
Woe to the provoking, and redeemed city, the dove.
2 Haukuisikiliza sauti ya Mungu, wala haukupokea masahihisho kutoka kwa Yahwe. Hakumtumaini Yahwe na hatamkaribia Mungu wake.
She hath not hearkened to the voice, neither hath she received discipline: she hath not trusted in the Lord, she drew not near to her God.
3 Wafalme wao ni simba wanaounguruma miongoni mwao. Waamuzi wao ni mbwa mwitu wa jioni wasiobakiza kitu ambacho kitakuwa kimemung'unywa asubuhi yake.
Her princes are in the midst of her as roaring lions: her judges are evening wolves, they left nothing for the morning.
4 Manabii wake wanakiburi na wanaume wasaliti. Makuhani wake wamepanajisi mahali patakatifu na wameifanyia vurugu sheria.
Her prophets are senseless men without faith: her priests have polluted the sanctuary, they have acted unjustly against the law.
5 Yahwe ni mwenye haki miongoni mwao. Hawezi kufanya makosa. Kila asubuhi husimamia haki yake! Haitafichika nuruni, hata hivyo watu wasio wenye haki hawajui kuona aibu.
The just Lord is in the midst thereof, he will not do iniquity: in the morning, in the morning he will bring his judgment to light, and it shall not be hid: but the wicked man hath not known shame.
6 Nimeyaharibu mataifa; ngome zao zimeharibiwa. Nimeifanya mitaa yao magofu, hivyo hakuna hata mmoja anayepitia kwake. Miji yao imeharibiwa kwa hiyo hakuna mtu anayeikaa.
I have destroyed the nations, and their towers are beaten down: I have made their ways desert, so that there is none that passeth by: their cities are desolate, there is not a man remaining, nor any inhabitant.
7 Nikasema, 'Hakika mtaniogopa mimi. Pokeeni masahihisho na msikatiliwe mbali kutoka kwenye miji yenu kwa yote yale niliyokuwa nimeyapanga kuyafanya kwenu.' Lakini walikuwa na shauku kuanza kila siku kwa kuharibu matendo yao yote.
I said: Surely thou wilt fear me, thou wilt receive correction: and her dwelling shall not perish, for all things wherein I have visited her: but they rose early and corrupted all their thoughts.
8 Kwa hiyo ningojeni - hili ni tamko la Yahwe - mpaka siku ambayo nitainuka kwa ajili ya waathirika. Uaamuzi wangu nikuwakusanya mataifa, kuzikusanya falme, na kumwaga juu yao hasira yangu, uchungu wangu wote mkali, hivyo nchi yote itamezwa kwa moto wa hasira yangu.
Wherefore expect me, saith the Lord, in the day of my resurrection that is to come, for my judgment is to assemble the Gentiles, and to gather the kingdoms: and to pour upon them my indignation, all my fierce anger: for with the fire of my jealousy shall all the earth be devoured.
9 Ndipo nitawapa midomo safi watu, kuwaita wote kwa jina la Bwana kunitumikia wakisimama bega kwa bega.
Because then I will restore to the people a chosen lip, that all may call upon the name of the Lord, and may serve him with one shoulder.
10 Kutoka ng'ambo ya mto Ethiopia waniabuduo - watu wangu waliotawanyika - wataleta dhabihu kwa sababu yangu.
From beyond the rivers of Ethiopia, shall my suppliants the children of my dispersed people bring me an offering.
11 Katika siku hiyo hamtawekwa kwenye woga kwa matendo yenu yote ambayo mmeyafanya dhidi yangu, tangu wakati ule nitaondoa kutoka kwenu wale waliosherehekea fahari yenu, na kwa sababu hamtakuwa na muda mrefu kufanya majivuno juu ya mlima wangu mtakatifu.
In that day thou shalt not be ashamed for all thy doings, wherein thou hast transgressed against me: for then I will take away out of the midst of thee thy proud boasters, and thou shalt no more be lifted up because of my holy mountain.
12 Lakini nitawaacha kama wa chini zaidi na watu masikini, na mtapata kimbilio katika jina la Yahwe.
And I will leave in the midst of thee a poor and needy people: and they shall hope in the name of the Lord.
13 Mkazi wa Israeli si muda mrefu hatafanya udhalimu au kusema uongo, na hakuna ulimi wa udanganyifu utakaoonekana mdomoni mwao; hivyo watalisha na kulala chini, na hakuna hata mmoja atakayewafanya kuogopa.”
The remnant of Israel shall not do iniquity, nor speak lies, nor shall a deceitful tongue be found in their mouth: for they shall feed, and shall lie down, and there shall be none to make them afraid.
14 Imba, binti Sayuni! Piga kelele, Israeli. Ufurahi na kushangilia kwa moyo wako wote, binti wa Yerusalemu.
Give praise, O daughter of Sion: shout, O Israel: be glad, and rejoice with all thy heart, O daughter of Jerusalem.
15 Yahwe ameiondoa hukumu yako; amewafukuzia mbali adui zako! Yahwe ni mfalme wa Israeli miongoni mwenu. Kamwe hamtamwogopa tena mwovu!
The Lord hath taken away thy judgment, he hath turned away thy enemies: the king of Israel the Lord is in the midst of thee, thou shalt fear evil no more.
16 Katika siku hizo watasema kwa Yerusalemi, “Usiogope, Sayuni. Usiiache mikono yako ilegee.
In that day it shall be said to Jerusalem: Fear not: to Sion: Let not thy hands be weakened.
17 Yahwe Mungu wako yuko katikati yenu, mwenye nguvu wa kuwaokoa. Atasherehekea juu yenu na kwa furaha atakuwa kimya juu yenu kwa upendo wake. Atakuwa na furaha juu yenu na atashangilia kwa furaha,
The Lord thy God in the midst of thee is mighty, he will save: he will rejoice over thee with gladness, he will be silent in his love, he will be joyful over thee in praise.
18 katika siku maalumu ya sherehe. Nitaondoa maafa kutoka kwenu; si muda mrefu hamtabeba aibu kwa ajili yake.
The triflers that were departed from the law, I will gather together, because they were of thee: that thou mayest no more suffer reproach for them.
19 Tazama, Niko tayari kuwashughulikia watesi wenu wote. Katika wakati ule, Nitawaokoa waliolemaa na kuwakusanya waliotupiliwa mbali. Nitawafanya kuwa sifa, na nitaibadilisha aibu yao iwe sifa katika dunia yote.
Behold I will cut off all that have afflicted thee at that time: and I will save her that halteth, and will gather her that was cast out: and I will get them praise, and a name, in all the land where they had been put to confusion.
20 Katika wakati ule nitawaongoza; katika wakati ule nitawakusanya pamoja. Nitawafanya mataifa yote ya dunia kuwaheshimu na kuwasifu, wakati mtakapoona hivyo, Nitakuwa nimewarudisha”, asema Yahwe.
At that time, when I will bring you: and at the time that I will gather you: for I will give you a name, and praise among all the people of the earth, when I shall have brought back your captivity before your eyes, saith the Lord.

< Sefania 3 >