< Sefania 2 >
1 Kusanyikeni pamoja ninyi wenyewe mkutano wa hadhara na kusanyikeni, taifa lisilokuwa na aibu -
Venez tous ensemble, réunissez-vous, nation indigne d’être aimée;
2 kabla amri kuchukua madhara na siku hiyo kupita kama makapi, kabla hasira kali ya ghadhabu ya Yahwe kuja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana kuja juu yenu.
Avant qu’un ordre enfante un jour comme la poussière qui passe, avant que vienne sur vous la colère de la fureur du Seigneur, avant que vienne sur vous le jour de l’indignation du Seigneur.
3 Mtafuteni Yahwe, ninyi watu wote wanyenyekevu duniani mnaozitii amri zake! Tafuteni haki yake. Tafuteni unyenyekevu, na labda mtalindwa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe.
Cherchez le Seigneur, vous tous humbles de la terre, qui avez exécuté ses jugements; cherchez la justice, cherchez la douceur; peut-être serez-vous à couvert au jour de la fureur du Seigneur.
4 hivyo Gaza utatelekezwa, na Ashkeloni utageuka kuwa uharibifu. Watauondoshea mbali Ashdodi wakati wa mchana, na wataung'oa Ekroni!
Parce que Gaza a été détruite et Ascalon réduite en un désert; on chassera Azot, en plein midi, et Accaron sera déracinée.
5 Ole kwa wanaokaa kando ya bahari, taifa la Wakerethi! Yahwe amesema dhidi yenu, Kanaani, nchi ya Wafilisiti. Nitawaangamiza hakuna mkazi atakayebakia.
Malheur à vous qui habitez la région de la mer, nation d’hommes perdus: la parole du Seigneur a été prononcée contre vous, Chanaan, terre des Philistins, et je t’exterminerai, en sorte qu’il n’y ait pas en toi d’habitant.
6 Hiyo nchi ya kando ya bahari itakuwa malisho kwa wachungaji na kwa mazizi ya kondoo.
Et la région de la mer sera le lieu de repos des pasteurs, et le parc des troupeaux de menu bétail;
7 Nchi ya kando ya bahari itakuwa mali ya mabaki ya watu wa nyumba ya Yuda, watakaochungia makundi yao huko. Watu wao watalala jioni katika nyumba ya Ashikeloni, kwa kuwa Yahwe Mungu wao atawatunza na kurejesha wafungwa wao.
Et cette région appartiendra à celui qui sera resté de la maison de Juda; là ils paîtront les troupeaux, dans les maisons d’Ascalon ils se reposeront le soir; parce que le Seigneur leur Dieu les visitera, et les ramènera de leur captivité.
8 Nilizisikia dhihaka za Moabu na wakiwatukana watu wa Amoni wakati walipowadhihaki watu wangu na kujitukuza mipakani mwao.
J’ai entendu les paroles outrageantes de Moab et les blasphèmes des fils d’Ammon, quand ils ont outragé mon peuple et l’ont bravé sur ses frontières.
9 Kwa hiyo, kama ninavyoishi - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, - Moabu itakuja kuwa kama Sodoma, na watu wa Amoni kama Gomora; mahali pa viwavi na shimo la chumvi, jangwa la daima. Lakini watu wangu waliosalia watawateka mateka, na watu wa taifa langu waliobaki watachukua umiliki wao.'
À cause de cela, je vis, moi, dit le Seigneur des armées, le Dieu d’Israël, Moab sera comme Sodome, et les fils d’Ammon comme Gomorrhe; ils auront des épines sèches, et des morceaux de sel, et un désert pour toujours; les restes de mon peuple les pilleront, et ceux de ma nation qui auront survécu en seront les maîtres.
10 Hili litatokea kwa Moabu na Amoni kwa sababu ya kiburi chao, tangu walipowadhihaki na kuwatukana watu wa Yahwe wa majeshi.
Cela leur arrivera à cause de leur orgueil; parce qu’ils ont blasphémé, et ont bravé le peuple du Seigneur des armées.
11 Ndipo watamwogopa Yahwe, kwa kuwa ataidhihaki miungu yote ya dunia. Kila mmoja atamwabudu yeye, kila mmoja kutoka mahali pake, kutoka kila upande wa pwani.
Le Seigneur sera terrible contre eux, et il anéantira tous les dieux de la terre; et les hommes l’adoreront, chacun en son lieu, ainsi que toutes les îles des nations.
12 Ninyi Wakushi pia mtakufa kwa upanga wangu,
Mais vous aussi, Ethiopiens, vous serez tués par mon glaive.
13 na mkono wa Mungu utaishambulia kaskazini na kuiangamiza Ashuru, Kwa hiyo Ninawi utatelekezwa kwa kuteketezwa, kuwa pakavu kama jangwa.
Et il étendra sa main vers l’aquilon et perdra Assur; et il fera de la cité magnifique une solitude, et un lieu inaccessible, et comme un désert.
14 Ndipo makundi ya wanyama yatalala pale, kila mnyama wa mataifa, wote kirukanjia na nungunungu watapumzika juu ya safu zao. Sauti itasikika kutoka madirishani; kifusi kitakuwa milangoni; nakshi za mwerezi wao mihimili itakuwa imeifunua.
Et se coucheront au milieu d’elle les troupeaux, et toutes les bêtes des nations; et l’onocrotale et le hérisson demeureront sur ses linteaux: la voix de l’oiseau chantant retentira sur la fenêtre; le corbeau croassera sur le linteau, parce que j’anéantirai sa force.
15 huu ni mji wa kushangiliwa ambao umekaa pasipo hofu, ambaye husema moyoni mwake, “Mimi niko, na hakuna mwingine wa kufanana na Mimi”. Kwa namna ulivyokuwa wa kutisha, mahali pa kulala wanyama ndani yake. Kila mmoja ambaye hupitia kwake huuhisia na kutingisha ngumi kwake.
Voilà la cité glorieuse qui demeurait dans la confiance; qui disait en son cœur: Moi je suis, et hors moi il n’y en a plus d’autre; comment est-elle devenue un désert, un repaire de bête sauvage? Quiconque la traversera, sifflera et agitera sa main.