< Sefania 2 >

1 Kusanyikeni pamoja ninyi wenyewe mkutano wa hadhara na kusanyikeni, taifa lisilokuwa na aibu -
Examinez-vous, examinez-vous avec soin ô nation qui n'êtes pas aimable!
2 kabla amri kuchukua madhara na siku hiyo kupita kama makapi, kabla hasira kali ya ghadhabu ya Yahwe kuja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana kuja juu yenu.
Avant que le décret enfante, et que le jour passe comme de la balle; avant que l'ardeur de la colère de l'Eternel vienne sur vous, avant que le jour de la colère de l'Eternel vienne sur vous.
3 Mtafuteni Yahwe, ninyi watu wote wanyenyekevu duniani mnaozitii amri zake! Tafuteni haki yake. Tafuteni unyenyekevu, na labda mtalindwa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe.
Vous, tous les débonnaires du pays, qui faites ce qu'il ordonne, cherchez l'Eternel, cherchez la justice, cherchez la débonnaireté; peut-être serez-vous mis en sûreté au jour de la colère de l'Eternel.
4 hivyo Gaza utatelekezwa, na Ashkeloni utageuka kuwa uharibifu. Watauondoshea mbali Ashdodi wakati wa mchana, na wataung'oa Ekroni!
Mais Gaza sera abandonnée, et Askélon sera en désolation; on chassera [les habitants] d'Asdod en plein Midi, et Hékron sera arrachée.
5 Ole kwa wanaokaa kando ya bahari, taifa la Wakerethi! Yahwe amesema dhidi yenu, Kanaani, nchi ya Wafilisiti. Nitawaangamiza hakuna mkazi atakayebakia.
Malheur aux habitants de la contrée maritime, à la nation des Kéréthiens, la parole de l'Eternel est contre vous; Canaan, [qui es] le pays des Philistins, je te détruirai, tellement que personne n'y habitera.
6 Hiyo nchi ya kando ya bahari itakuwa malisho kwa wachungaji na kwa mazizi ya kondoo.
Et la contrée maritime ne sera que cabanes, que loges de bergers, et parcs de brebis.
7 Nchi ya kando ya bahari itakuwa mali ya mabaki ya watu wa nyumba ya Yuda, watakaochungia makundi yao huko. Watu wao watalala jioni katika nyumba ya Ashikeloni, kwa kuwa Yahwe Mungu wao atawatunza na kurejesha wafungwa wao.
Et cette contrée sera pour le reste de la maison de Juda; ils paîtront dans ces lieux-là, et le soir ils feront leur gîte dans les maisons d'Askélon; car l'Eternel leur Dieu les visitera, et il ramènera leurs captifs.
8 Nilizisikia dhihaka za Moabu na wakiwatukana watu wa Amoni wakati walipowadhihaki watu wangu na kujitukuza mipakani mwao.
J'ai ouï les insultes de Moab, et les invectives des enfants de Hammon, dont ils ont diffamé mon peuple, et l'ont bravé sur leur frontière.
9 Kwa hiyo, kama ninavyoishi - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, - Moabu itakuja kuwa kama Sodoma, na watu wa Amoni kama Gomora; mahali pa viwavi na shimo la chumvi, jangwa la daima. Lakini watu wangu waliosalia watawateka mateka, na watu wa taifa langu waliobaki watachukua umiliki wao.'
C'est pourquoi, je suis vivant, dit l'Eternel des armées, le Dieu d'Israël, que Moab sera comme Sodome, et les enfants de Mammon comme Gomorrhe, un lieu couvert d'orties, et une carrière de sel et de désolation à jamais; les restes de mon peuple les pilleront, et les restes de [ma] nation les posséderont.
10 Hili litatokea kwa Moabu na Amoni kwa sababu ya kiburi chao, tangu walipowadhihaki na kuwatukana watu wa Yahwe wa majeshi.
Ceci leur arrivera en échange de leur orgueil, parce qu'ils ont usé d'insultes et de vanteries, contre le peuple de l'Eternel des armées.
11 Ndipo watamwogopa Yahwe, kwa kuwa ataidhihaki miungu yote ya dunia. Kila mmoja atamwabudu yeye, kila mmoja kutoka mahali pake, kutoka kila upande wa pwani.
L'Eternel sera terrible contre eux; car il amaigrira tous les dieux du pays; et on se prosternera devant lui, chacun de son lieu, même toutes les Iles des nations.
12 Ninyi Wakushi pia mtakufa kwa upanga wangu,
Vous aussi [habitants] de Cus, vous serez blessés à mort par mon épée.
13 na mkono wa Mungu utaishambulia kaskazini na kuiangamiza Ashuru, Kwa hiyo Ninawi utatelekezwa kwa kuteketezwa, kuwa pakavu kama jangwa.
Il étendra aussi sa main sur l'Aquilon, et il détruira l'Assyrie, et mettra Ninive en désolation, en un lieu aride comme un désert.
14 Ndipo makundi ya wanyama yatalala pale, kila mnyama wa mataifa, wote kirukanjia na nungunungu watapumzika juu ya safu zao. Sauti itasikika kutoka madirishani; kifusi kitakuwa milangoni; nakshi za mwerezi wao mihimili itakuwa imeifunua.
Et les troupeaux feront leur gîte au milieu d'elle, et toutes les bêtes des nations, même le cormoran, et le butor logeront dans ses porteaux, la voix des oiseaux retentira à la fenêtre, la désolation sera au seuil, parce qu'il en aura abbatu des cèdres.
15 huu ni mji wa kushangiliwa ambao umekaa pasipo hofu, ambaye husema moyoni mwake, “Mimi niko, na hakuna mwingine wa kufanana na Mimi”. Kwa namna ulivyokuwa wa kutisha, mahali pa kulala wanyama ndani yake. Kila mmoja ambaye hupitia kwake huuhisia na kutingisha ngumi kwake.
C'est là cette ville remplie de joie, qui se tenait assurée, et qui disait en son cœur; c'est moi, et il n'y en a point d'autre que moi. Comment a-t-elle été réduite en désert, pour être le gîte des bêtes? Quiconque passera près d elle se moquera, et branlera sa main.

< Sefania 2 >