< Sefania 2 >
1 Kusanyikeni pamoja ninyi wenyewe mkutano wa hadhara na kusanyikeni, taifa lisilokuwa na aibu -
Recueillez-vous, rentrez en vous-mêmes, race sans pudeur,
2 kabla amri kuchukua madhara na siku hiyo kupita kama makapi, kabla hasira kali ya ghadhabu ya Yahwe kuja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana kuja juu yenu.
avant que le décret ait enfanté, que le jour ait passé comme la paille; avant que vienne sur vous l’ardeur de la colère de Yahweh, avant que vienne sur vous le jour de la colère de Yahweh.
3 Mtafuteni Yahwe, ninyi watu wote wanyenyekevu duniani mnaozitii amri zake! Tafuteni haki yake. Tafuteni unyenyekevu, na labda mtalindwa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe.
Cherchez Yahweh, vous tous humbles du pays, qui avez pratiqué sa loi; recherchez la justice, recherchez l’humilité. Peut-être serez-vous à l’abri au jour de la colère de Yahweh!...
4 hivyo Gaza utatelekezwa, na Ashkeloni utageuka kuwa uharibifu. Watauondoshea mbali Ashdodi wakati wa mchana, na wataung'oa Ekroni!
Car Gaza sera abandonnée, et Ascalon réduite en désert; on chassera Azot en plein midi, et Accaron sera déracinée.
5 Ole kwa wanaokaa kando ya bahari, taifa la Wakerethi! Yahwe amesema dhidi yenu, Kanaani, nchi ya Wafilisiti. Nitawaangamiza hakuna mkazi atakayebakia.
Malheur aux habitants de la région de la mer, à la nation des Crétois! La parole de Yahweh est prononcée contre vous, Canaan, terre des Philistins: « Et je te détruirai en sorte qu’il ne te reste plus d’habitants. »
6 Hiyo nchi ya kando ya bahari itakuwa malisho kwa wachungaji na kwa mazizi ya kondoo.
La région de la mer deviendra des pâturages, des grottes de bergers et des parcs de moutons.
7 Nchi ya kando ya bahari itakuwa mali ya mabaki ya watu wa nyumba ya Yuda, watakaochungia makundi yao huko. Watu wao watalala jioni katika nyumba ya Ashikeloni, kwa kuwa Yahwe Mungu wao atawatunza na kurejesha wafungwa wao.
Ce sera un territoire pour le reste de la maison de Juda, ils y paîtront leurs troupeaux; le soir, ils prendront leur gîte dans les maisons d’Ascalon, car Yahweh, leur Dieu, les visitera et les rétablira.
8 Nilizisikia dhihaka za Moabu na wakiwatukana watu wa Amoni wakati walipowadhihaki watu wangu na kujitukuza mipakani mwao.
J’ai entendu les insultes de Moab, et les outrages des fils d’Ammon, qui insultaient mon peuple, et s’agrandissaient aux dépens de ses frontières.
9 Kwa hiyo, kama ninavyoishi - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, - Moabu itakuja kuwa kama Sodoma, na watu wa Amoni kama Gomora; mahali pa viwavi na shimo la chumvi, jangwa la daima. Lakini watu wangu waliosalia watawateka mateka, na watu wa taifa langu waliobaki watachukua umiliki wao.'
C’est pourquoi, je suis vivant, — oracle de Yahweh des armées, le Dieu d’Israël: Moab sera comme Sodome, et les fils d’Ammon comme Gomorrhe: un lieu livré aux orties, une carrière de sel, un désert à jamais. Le reste de mon peuple le pillera, et ce qui demeurera de ma nation, les aura en héritage.
10 Hili litatokea kwa Moabu na Amoni kwa sababu ya kiburi chao, tangu walipowadhihaki na kuwatukana watu wa Yahwe wa majeshi.
Cela leur arrivera pour leur orgueil, parce qu’ils ont été méprisants et insolents, contre le peuple de Yahweh des armées.
11 Ndipo watamwogopa Yahwe, kwa kuwa ataidhihaki miungu yote ya dunia. Kila mmoja atamwabudu yeye, kila mmoja kutoka mahali pake, kutoka kila upande wa pwani.
Yahweh sera un objet de terreur pour eux, car il anéantira tous les dieux de la terre; et devant lui se prosterneront, chacun de son lieu, les habitants de toutes les îles des nations.
12 Ninyi Wakushi pia mtakufa kwa upanga wangu,
Vous aussi, Ethiopiens!... Ils seront transpercés par mon épée.
13 na mkono wa Mungu utaishambulia kaskazini na kuiangamiza Ashuru, Kwa hiyo Ninawi utatelekezwa kwa kuteketezwa, kuwa pakavu kama jangwa.
Il étendra aussi sa main contre le nord, il détruira Assur, et il fera de Ninive une solitude, aride comme le désert.
14 Ndipo makundi ya wanyama yatalala pale, kila mnyama wa mataifa, wote kirukanjia na nungunungu watapumzika juu ya safu zao. Sauti itasikika kutoka madirishani; kifusi kitakuwa milangoni; nakshi za mwerezi wao mihimili itakuwa imeifunua.
Au milieu d’elle prendront leur gîte des troupeaux, des animaux de toute espèce; même le pélican, même le hérisson se logeront sur ses chapiteaux; on entendra des chants dans les fenêtres, la désolation sera sur le seuil, car on a mis à nu les boiseries de cèdres.
15 huu ni mji wa kushangiliwa ambao umekaa pasipo hofu, ambaye husema moyoni mwake, “Mimi niko, na hakuna mwingine wa kufanana na Mimi”. Kwa namna ulivyokuwa wa kutisha, mahali pa kulala wanyama ndani yake. Kila mmoja ambaye hupitia kwake huuhisia na kutingisha ngumi kwake.
C’est là la ville joyeuse, assise avec assurance, qui disait en son cœur: « Moi, et rien que moi! » Comment est-elle devenue un désert, une demeure pour les bêtes? Quiconque passera sur elle sifflera et agitera la main.