< Sefania 2 >

1 Kusanyikeni pamoja ninyi wenyewe mkutano wa hadhara na kusanyikeni, taifa lisilokuwa na aibu -
Search yourselves; yea, search, O nation without shame!
2 kabla amri kuchukua madhara na siku hiyo kupita kama makapi, kabla hasira kali ya ghadhabu ya Yahwe kuja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana kuja juu yenu.
Before the decree bring forth, Before the day come upon you like chaff; Before the fierce anger of Jehovah come upon you, Before the day of the anger of Jehovah come upon you.
3 Mtafuteni Yahwe, ninyi watu wote wanyenyekevu duniani mnaozitii amri zake! Tafuteni haki yake. Tafuteni unyenyekevu, na labda mtalindwa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe.
Seek ye Jehovah, all ye lowly of the land, Ye, who obey his commands! Seek righteousness; seek lowliness; It may be that ye shall be hid in the day of the anger of Jehovah.
4 hivyo Gaza utatelekezwa, na Ashkeloni utageuka kuwa uharibifu. Watauondoshea mbali Ashdodi wakati wa mchana, na wataung'oa Ekroni!
For Gaza shall be forsaken, And Askelon a desolation; Ashdod shall be driven out at noonday, And Ekron shall be rooted up.
5 Ole kwa wanaokaa kando ya bahari, taifa la Wakerethi! Yahwe amesema dhidi yenu, Kanaani, nchi ya Wafilisiti. Nitawaangamiza hakuna mkazi atakayebakia.
Woe to the inhabitants of the sea-coasts, the nation of the Cherethites! This is the word of Jehovah against you, O Canaan, land of the Philistines: “I will destroy thee, that there shall be no inhabitant.”
6 Hiyo nchi ya kando ya bahari itakuwa malisho kwa wachungaji na kwa mazizi ya kondoo.
And the sea-coast shall be pastures full of habitations for shepherds, and folds for flocks.
7 Nchi ya kando ya bahari itakuwa mali ya mabaki ya watu wa nyumba ya Yuda, watakaochungia makundi yao huko. Watu wao watalala jioni katika nyumba ya Ashikeloni, kwa kuwa Yahwe Mungu wao atawatunza na kurejesha wafungwa wao.
The coast shall be for the residue of the house of Judah; Thereon shall they feed; In the houses of Askelon shall they lie down in the evening; For Jehovah their God will look upon them, and bring back their captives.
8 Nilizisikia dhihaka za Moabu na wakiwatukana watu wa Amoni wakati walipowadhihaki watu wangu na kujitukuza mipakani mwao.
I have heard the reproach of Moab, And the revilings of the sons of Ammon, With which they have reproached my people, And exalted themselves against their borders.
9 Kwa hiyo, kama ninavyoishi - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, - Moabu itakuja kuwa kama Sodoma, na watu wa Amoni kama Gomora; mahali pa viwavi na shimo la chumvi, jangwa la daima. Lakini watu wangu waliosalia watawateka mateka, na watu wa taifa langu waliobaki watachukua umiliki wao.'
Therefore, as I live, saith Jehovah of hosts, the God of Israel, Moab shall be as Sodom, And the sons of Ammon as Gomorrah, A possession for thorns, and a pit for salt, and a perpetual desolation. The residue of my people shall spoil them, And the remainder of my nation shall possess them.
10 Hili litatokea kwa Moabu na Amoni kwa sababu ya kiburi chao, tangu walipowadhihaki na kuwatukana watu wa Yahwe wa majeshi.
This shall come upon them for their pride, Because they have uttered reproaches, and exalted themselves against the people of Jehovah of hosts.
11 Ndipo watamwogopa Yahwe, kwa kuwa ataidhihaki miungu yote ya dunia. Kila mmoja atamwabudu yeye, kila mmoja kutoka mahali pake, kutoka kila upande wa pwani.
Jehovah will be terrible against them; For he will destroy all the gods of the earth; And before him shall worship, every one from his place, All the islands of the nations.
12 Ninyi Wakushi pia mtakufa kwa upanga wangu,
Ye, also, O Ethiopians! Ye shall be slain by my sword!
13 na mkono wa Mungu utaishambulia kaskazini na kuiangamiza Ashuru, Kwa hiyo Ninawi utatelekezwa kwa kuteketezwa, kuwa pakavu kama jangwa.
He will also stretch out his hand against the North, And destroy Assyria, And make Nineveh a desolation, Even dry like a desert.
14 Ndipo makundi ya wanyama yatalala pale, kila mnyama wa mataifa, wote kirukanjia na nungunungu watapumzika juu ya safu zao. Sauti itasikika kutoka madirishani; kifusi kitakuwa milangoni; nakshi za mwerezi wao mihimili itakuwa imeifunua.
And flocks shall lie down in the midst of her, Yea, all the tribes of wild beasts; The pelican and the hedgehog shall lodge in the capitals of her pillars; A cry shall resound in the window; Desolation shall be upon the threshold; For her cedar-work shall be laid bare.
15 huu ni mji wa kushangiliwa ambao umekaa pasipo hofu, ambaye husema moyoni mwake, “Mimi niko, na hakuna mwingine wa kufanana na Mimi”. Kwa namna ulivyokuwa wa kutisha, mahali pa kulala wanyama ndani yake. Kila mmoja ambaye hupitia kwake huuhisia na kutingisha ngumi kwake.
This is the rejoicing city that dwelt in security, That said in her heart, “I, and none besides me!” Now is she become a desolation, a resting-place for wild beasts! Every one that passeth by her shall hiss, and wag his hand.

< Sefania 2 >