< Zekaria 1 >

1 Katika mwezi wa nane mwaka wa pili wa kutawala kwake Dario, neno la Yahwe lilimjia nabii Zekaria, mwana wa Berekia mwana wa Ido, kusema,
[I am] Zechariah, a prophet, the son of Berekiah and grandson of Iddo. When Darius [had been the emperor of Persia] for almost two years, during November [of that year], Yahweh gave me this message:
2 “Yawhe alikuwa na hasira sana juu ya baba zenu!
“I was very angry with your ancestors.
3 Wambie, 'Yahwe wa majeshi asema hivi: Nirudieni! - nami nitawarudia ninyi, asema Yahwe wa majeshi.
So tell this to the people: [I, ] the Commander of the armies of angels, say, ‘Return to me, and [if you do that], I will [help] you again.
4 Msiwe kama baba zenu ambao hapo zamani manabii waliwambia, wakisema, “Yahwe wa majeshi asema hivi: Geukeni kutoka katika njia zenu za mbaya na matendo yenu mabaya!” Lakini hawakuweza kusikia wala kunijari - asema Yahwe.'
Do not be like your ancestors. [Other] prophets, who have now died, [continually] proclaimed to your ancestors that they should stop doing the evil things that they were continually doing. But they refused to pay attention to what I said.
5 Wako wapi baba zenu? Na manabii, je wapo hapa daima?
Your ancestors [have died and are now in their graves] [RHQ]. And the prophets did not [RHQ] live forever, [either].
6 Lakini maneno yangu na maagizo niliyowaamru watumishi wangu manabii, je hayakuwapata baba zenu? Hivyo walitubu na kusema, 'Kama vile Yahwe wa majeshi alivyokusudia kututenda kwa kadili zinavyostahili njia na matendo yetu, ndivyo alivyotutenda.”
But I punished [IDM] [the people for disobeying] the commands and the decrees which I commanded my servants the prophets [to tell to the people]. Then they (repented/turned away from their evil behavior) and said, ‘The Commander of the armies of angels has done to us what we deserved for our evil behavior, just like he said that he would do.’”
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, ndiyo mwezi wa Shebati, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yahwe lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido, akasema,
[Three months later], on February 15, Yahweh gave [another] message to me.
8 “niliona wakati wa usiku, na tazama! mtu alikuwa amepanda farasi mwekundu, naye alikuwa kati ya miti ya mihadasi iliyoko bondeni; na nyuma yake kulikuwa na farasi mwekundu, farasi wa kijivu, na farasi mweupe.”
During the night [I had a vision. In the vision] I saw an [angel] who was on a red horse. He was in a narrow valley among some myrtle trees. Behind him were [angels on] red, brown, and white horses.
9 Nikauliza, “Bwana, hivi ni vitu gani?” Malaika aliyesema nami akaniambia, “Nitakueleza vitu hivi ni nini.”
I asked the angel who had been talking to me, “Sir, who are those [angels on the horses]?” He replied, “I will show you who they are.”
10 Kisha mtu aliyesimama kati ya miti ya mihadasi akajibu na kusema, “Hawa ndiyo Yahwe aliowatuma kuzunguka katika dunia yote.”
Then the [angel] who had been under the myrtle trees explained. [He said, ] “They are the [angels] whom Yahweh sent [to (patrol/see what is happening in)] the [entire] world.”
11 Wakamjibu malaika wa Yahwe aliyekuwa amesimama kati ya miti ya mihadasi na kumwambia, “Tumekuwa tukizunguka duniani pote; tazama, dunia yote imekaa na kutulia.”
Then those angels reported to the angel who was [there] among the myrtle trees, “We have traveled throughout the world, and we have found out that [the army of the emperor of Persia has conquered nations] throughout the world, [and that] those nations are now (helpless/unable to resist his army).”
12 Ndipo malaika wa Yahwe alipojibu na kusema, “Yahwe wa majeshi, hata lini usiuhurumie Yerusalemu na miji ya Yuda ambayo imeteswa na kudhurumiwa miaka hii sabini?”
Then the angel asked, “Commander of the armies of angels, how long will you continue to not be merciful to Jerusalem and the [other] towns in Judah? You have been angry with them for 70 years!”
13 Yahwe akamjibu malaika aliyekuwa amesema nami, kwa maneno mazuri, maneno ya faraja.
[So] Yahweh spoke kindly to the angel who had talked to me, saying things that comforted/encouraged him.
14 Hivyo malaika aliyekuwa anaongea nami akaniambia, “Ita kwa sauti na useme 'Yahwe wa majeshi asema: Nina wivu kwa ajili ya Yerusalemu yaani Sayuni kwa uchungu mkubwa!
Then the angel who had been talking with me said to me, “Proclaim this [to the people of Jerusalem]: The Commander of the armies of angels says that he is very concerned about [the people who live on] Zion [Hill] and [in the other parts of] Jerusalem.
15 Nami nina hasira juu ya mataifa yaliyo na utulivu. Kwa maana nilikasirika kidogo tu, lakini wao wakasababisha madhara mabaya.
But he is very angry with the nations that are [proud and feel] safe. He was only a little bit angry [with the people of Judah], but [he is very angry with the surrounding nations because] they caused [the people of Judah to experience] complete disaster.
16 Kwa hiyo Yahwe wa majeshi asema hivi: Nimeirudia Yerusalema kwa huruma. Hivyo nyumba yangu itajengwa ndani yake - asema Yahwe wa majeshi. Kipimo kitanyoshwa juu ya Yerusalemu!
Therefore, this is what he says: ‘I will again be merciful to [the people of] Jerusalem, and they will rebuild my temple. Men will measure [all the land in] the city [before they start rebuilding the houses].’
17 Ita tena, ukisema, 'Yahwe wa majeshi asema hivi: Miji yangu kwa mara nyingine itajawa na uzuri, na Yahwe ataifariji tena Sayuni, na kuichagua Yerusalemu kwa mara nyingine tena.”
The Commander of the armies of angels [also] said this: ‘Tell the people that [the people in] my towns [in Judah] will soon be very prosperous again, and I will encourage [the people of] Jerusalem, and their city will again be my chosen [city].’”
18 Kisha nikainua macho na kuona pembe nne!
Then I looked up, and I saw in front of me four [animal] horns.
19 Nikaongea na malaika aliyesema nami, “Hivi ni vitu gani? Akanijibu “hizi ni pembe zilisosababisha kutawanyika kwa Yuda, Israeli, na Yerusalemu.”
I asked the angel who had been speaking to me, “What are those [horns]?” He replied, “Those horns [represent the armies that] forced [the people of] Jerusalem and [other places in] Judah and Israel to go [to other countries].”
20 Kisha Yahwe akanionesha mafundi stadi wanne.
Then Yahweh showed me four (craftsmen/men who make things from metal).
21 Nikasema, “Watu hawa wanakuja kufanya nini?” Akajibu na kusema, “Hizi ni pembe zililoitawanya Yuda na hakuna mtu angeweza kuinua kichwa chake. Lakini watu hawa wanakuja kuziondoa, kutupa chini pembe za mataifa yaliyoinua nguvu zao kinyume cha nchi ya Yuda na kuisambaza.”
I asked, “What are those men coming to do?” He replied, “[The armies represented by] those horns caused [the people of] Judah to be scattered, with the result that they suffered greatly. But the craftsmen have come to cause those who attacked [IDM] Judah to be terrified and crushed.”

< Zekaria 1 >