< Zekaria 9 >

1 Hili ni tamko la neno la Yahwe kuhusu nchi ya Hadraki na Damesiki. Kwa maana jicho la Yahwe liko juu ya wanadamu wote, na juu ya kabila zote za Israeli pia.
Le poids de la parole de l’Eternel est sur le pays de Hadrâc, il repose sur Damas; car l’Eternel a l’œil sur les hommes, comme sur toutes les tribus d’Israël!
2 Azimio hili pia linaihusu Hamathi, inayopakana na Damesiki, na linahusu Tiro na Sidoni, japokuwa ni werevu sana.
Elle pèse aussi sur Hamath qui en est limitrophe, sur Tyr et Sidon, si grandement avisées.
3 Tiro amejijengea ngome na kurundika fedha kama mavumbi na dhahabu safi kama matope mitaani.
Tyr s’est bâti une enceinte fortifiée, elle a entassé de l’argent comme de la poussière, de l’or fin comme la boue des rues.
4 Tazama! Bwana atamnyang'anya na kuharibu nguvu zake juu ya bahari, kwa hiyo atateketezwa kwa moto.
Mais voici, l’Eternel va la déposséder, il abattra ses remparts dans la mer, elle-même sera la proie du feu.
5 Ashikeloni ataona na kuogopa! Gaza pia atatemeka sana! Ekroni, tumanini lake litatikiswa! Mfalme ataangamizwa kuanzia Gaza, na Ashikeloni haitakuwa na watu tena!
Ascalon la verra et aura peur, Gaza en tremblera de tous ses membres, de même Ekron, dont l’espoir est déçu. Plus de roi à Gaza! Ascalon cessera d’être habité.
6 Wageni watafanya makao yao katika Ashidodi, nami nitakiondoa kiburi cha Wafilisiti.
Des bâtards rempliront Asdod, et j’anéantirai l’orgueil du peuple des Philistins.
7 Kwani nitaondoa damu yao katika vinywa vyao na machukizo yao kutoka kati ya meno yao. Ndipo watakapokuwa masalia kwa Mungu wetu kama ukoo katika Yuda, na Ekironi atakuwa kama Wayebusi.
Puis, j’enlèverai le sang de sa bouche et ses mets horribles d’entre ses dents; de la sorte il survivra lui aussi pour notre Dieu et sera l’égal des chefs dans Juda, et Ekron sera comme le Jébuséen.
8 Nitaweka kambi kuzunguka nchi yangu kinyume cha majeshi ya adui hata hakuna atakayeweza kupita ndani yake tena, kwani hakuna mtesaji atakayeipita tena. Kwa kuwa sasa nitaangalia nchi yangu kwa macho yangu mwenyewe!
Et je ferai bonne garde autour de ma maison contre toute armée, contre les allants et venants. Nul oppresseur ne viendra plus les attaquer, car à présent j’aurai les yeux ouverts.
9 Piga kelele kwa furaha, ewe binti Sayuni! Piga kelele kwa shangwe, ewe binti Yerusalem! Tazama! Mfalme wako anakuja kwako pamoja na uadilifu na anakuokoa. Ni mnyenyekevu, amepanda punda, mwanapunda.
Réjouis-toi fort, fille de Sion, jubile, fille de Jérusalem! Voici que ton roi vient à toi juste et victorieux, humble, monté sur un âne, sur le petit de l’ânesse.
10 Ndipo nitakapoondoa kibandawazi kutoka Efraimu na farasi kutoka Yerusalemu, na upinde utaondolewa katika vita; kwani atasema amani kwa mataifa, na utawala wake utakuwa kutoka bahari hata bahari, na kutoka katika mto hadi miisho ya dunia!
Plus de chars en Ephraïm, plus de chevaux à Jérusalem, plus d’arc de guerre! Il dictera la paix aux nations. Son empire s’étendra d’une mer à l’autre, et du fleuve aux extrémités de la terre.
11 Lakini kwenu, kwa sababu ya damu ya agano langu nanyi, nitawaweka wafungwa wenu huru kutoka shimoni pasipo na maji.
Et pour toi, en vertu du sang de ton alliance, je tirerai tes captifs de la citerne où il n’y a pas d’eau.
12 Rudini ngomeni, wafungwa wa matumaini! Hata leo natamka kwamba nitawarudishia mara mbili, kwani nimempinda Yuda kama upinde wangu.
Retournez dans la place forte, vous qui êtes engagés dans les liens de l’espérance! Aujourd’hui même je vous annonce que je vous paierai au double.
13 Hata nimelijaza podo langu pamoja na Efraimu. Nimewainua wana wenu, Sayuni, kinyume cha wana wenu, Ugiriki, na amekufanya wewe, Sayuni, kama upanga wa shujaa!
Oui, je me fais de Juda comme un arc bandé, d’Ephraïm un carquois bien garni. Je vais lancer tes fils, ô Sion, contre les tiens, ô lavân! Tu seras pour moi comme une épée de héros.
14 Yahwe atawatokea, na mishale yake itapiga kama radi! Kwa maana Yahwe Bwana wangu atapiga tarumbeta naye ataendelea pamoja na dhoruba kutoka Temani.
Et l’Eternel apparaîtra au-dessus d’eux; sa flèche s’élancera comme un éclair. Le Seigneur Dieu fera retentir la trompette et s’avancera dans les ouragans du Midi.
15 Yahwe wa majeshi atawatetea, nao watawararua na kuyashinda mawe ya kombeo. Ndipo watakapo kunywa na kupiga kelele kama mtu aliyelewa kwa mvunyo, nao watajazwa na mvinyo kama mabakuri, kama pembe za madhabahu.
L’Eternel-Cebaot étendra sa protection sur eux: ils ne feront qu’une bouchée des pierres de fronde qu’ils fouleront aux pieds, ils boiront et seront animés, comme pris de vin, gorgés comme les bassins et les angles de l’autel.
16 Hivyo Yahwe Mungu wao atawaokoa siku hiyo; watakuwa kama kundi la kondoo lililo na watu wake, kwani watakuwa mapambo ya taji, yaliyoinuliwa juu ya nchi yake.
L’Eternel, leur Dieu, leur prêtera main-forte, en ce jour, à ce peuple qui est son troupeau, car ce sont des pierres de diadème étincelant sur son territoire.
17 Jinsi gani watakavyokuwa wazuri na warembo! vijana watastawi juu ya nafaka na bikra juu ya divai tamu!
Ah! Quel est son bonheur! Quelle est leur beauté! Le blé fait prospérer les jeunes gens et le vin généreux les jeunes filles.

< Zekaria 9 >