< Zekaria 9 >
1 Hili ni tamko la neno la Yahwe kuhusu nchi ya Hadraki na Damesiki. Kwa maana jicho la Yahwe liko juu ya wanadamu wote, na juu ya kabila zote za Israeli pia.
oracle word LORD in/on/with land: country/planet Hadrach and Damascus resting his for to/for LORD eye man and all tribe Israel
2 Azimio hili pia linaihusu Hamathi, inayopakana na Damesiki, na linahusu Tiro na Sidoni, japokuwa ni werevu sana.
and also Hamath to border in/on/with her Tyre and Sidon for be wise much
3 Tiro amejijengea ngome na kurundika fedha kama mavumbi na dhahabu safi kama matope mitaani.
and to build Tyre siege to/for her and to heap silver: money like/as dust and gold like/as mud outside
4 Tazama! Bwana atamnyang'anya na kuharibu nguvu zake juu ya bahari, kwa hiyo atateketezwa kwa moto.
behold Lord to possess: take her and to smite in/on/with sea strength her and he/she/it in/on/with fire to eat
5 Ashikeloni ataona na kuogopa! Gaza pia atatemeka sana! Ekroni, tumanini lake litatikiswa! Mfalme ataangamizwa kuanzia Gaza, na Ashikeloni haitakuwa na watu tena!
to see: see Ashkelon and to fear and Gaza and to twist: writh in pain much and Ekron for be ashamed expectation her and to perish king from Gaza and Ashkelon not to dwell
6 Wageni watafanya makao yao katika Ashidodi, nami nitakiondoa kiburi cha Wafilisiti.
and to dwell bastard in/on/with Ashdod and to cut: eliminate pride Philistine
7 Kwani nitaondoa damu yao katika vinywa vyao na machukizo yao kutoka kati ya meno yao. Ndipo watakapokuwa masalia kwa Mungu wetu kama ukoo katika Yuda, na Ekironi atakuwa kama Wayebusi.
and to turn aside: remove blood his from lip his and abomination his from between tooth his and to remain also he/she/it to/for God our and to be like/as chief in/on/with Judah and Ekron like/as Jebusite
8 Nitaweka kambi kuzunguka nchi yangu kinyume cha majeshi ya adui hata hakuna atakayeweza kupita ndani yake tena, kwani hakuna mtesaji atakayeipita tena. Kwa kuwa sasa nitaangalia nchi yangu kwa macho yangu mwenyewe!
and to camp to/for house: home my guard from to pass and from to return: repent and not to pass upon them still to oppress for now to see: see in/on/with eye my
9 Piga kelele kwa furaha, ewe binti Sayuni! Piga kelele kwa shangwe, ewe binti Yerusalem! Tazama! Mfalme wako anakuja kwako pamoja na uadilifu na anakuokoa. Ni mnyenyekevu, amepanda punda, mwanapunda.
to rejoice much daughter Zion to shout daughter Jerusalem behold king your to come (in): come to/for you righteous and to save he/she/it afflicted and to ride upon donkey and upon colt son: child she-ass
10 Ndipo nitakapoondoa kibandawazi kutoka Efraimu na farasi kutoka Yerusalemu, na upinde utaondolewa katika vita; kwani atasema amani kwa mataifa, na utawala wake utakuwa kutoka bahari hata bahari, na kutoka katika mto hadi miisho ya dunia!
and to cut: eliminate chariot from Ephraim and horse from Jerusalem and to cut: eliminate bow battle and to speak: speak peace to/for nation and dominion his from sea till sea and from River till end land: country/planet
11 Lakini kwenu, kwa sababu ya damu ya agano langu nanyi, nitawaweka wafungwa wenu huru kutoka shimoni pasipo na maji.
also you(f. s.) in/on/with blood covenant your to send: let go prisoner your from pit nothing water in/on/with him
12 Rudini ngomeni, wafungwa wa matumaini! Hata leo natamka kwamba nitawarudishia mara mbili, kwani nimempinda Yuda kama upinde wangu.
to return: return to/for stronghold prisoner [the] hope also [the] day to tell second to return: rescue to/for you
13 Hata nimelijaza podo langu pamoja na Efraimu. Nimewainua wana wenu, Sayuni, kinyume cha wana wenu, Ugiriki, na amekufanya wewe, Sayuni, kama upanga wa shujaa!
for to tread to/for me Judah bow to fill Ephraim and to rouse son: descendant/people your Zion upon son: descendant/people your Greece and to set: put you like/as sword mighty man
14 Yahwe atawatokea, na mishale yake itapiga kama radi! Kwa maana Yahwe Bwana wangu atapiga tarumbeta naye ataendelea pamoja na dhoruba kutoka Temani.
and LORD upon them to see: see and to come out: come like/as lightning arrow his and Lord YHWH/God in/on/with trumpet to blow and to go: walk in/on/with tempest south
15 Yahwe wa majeshi atawatetea, nao watawararua na kuyashinda mawe ya kombeo. Ndipo watakapo kunywa na kupiga kelele kama mtu aliyelewa kwa mvunyo, nao watajazwa na mvinyo kama mabakuri, kama pembe za madhabahu.
LORD Hosts to defend upon them and to eat and to subdue stone sling and to drink to roar like wine and to fill like/as bowl like/as corner altar
16 Hivyo Yahwe Mungu wao atawaokoa siku hiyo; watakuwa kama kundi la kondoo lililo na watu wake, kwani watakuwa mapambo ya taji, yaliyoinuliwa juu ya nchi yake.
and to save them LORD God their in/on/with day [the] he/she/it like/as flock people his for stone consecration: crown to shine upon land: soil his
17 Jinsi gani watakavyokuwa wazuri na warembo! vijana watastawi juu ya nafaka na bikra juu ya divai tamu!
for what? goodness his and what? beauty his grain youth and new wine to bear fruit virgin