< Zekaria 9 >
1 Hili ni tamko la neno la Yahwe kuhusu nchi ya Hadraki na Damesiki. Kwa maana jicho la Yahwe liko juu ya wanadamu wote, na juu ya kabila zote za Israeli pia.
The oracle of the word of Yahweh on the land of Hadrach, and, Damascus, shall be the resting-place thereof, —For, Yahweh, hath an eye—to mankind, and to all the tribes of Israel;
2 Azimio hili pia linaihusu Hamathi, inayopakana na Damesiki, na linahusu Tiro na Sidoni, japokuwa ni werevu sana.
Moreover also, Hamath, adjoineth thereto, Tyre and Zidon, —because very wise;
3 Tiro amejijengea ngome na kurundika fedha kama mavumbi na dhahabu safi kama matope mitaani.
Therefore did Tyre build a stronghold for herself, —and did heap up silver like dust, yea gold, like the mire of the lanes.
4 Tazama! Bwana atamnyang'anya na kuharibu nguvu zake juu ya bahari, kwa hiyo atateketezwa kwa moto.
Lo! My Lord, shall dispossess her, and smite, into the sea, her fortress, —and, she herself, in fire, shall be consumed.
5 Ashikeloni ataona na kuogopa! Gaza pia atatemeka sana! Ekroni, tumanini lake litatikiswa! Mfalme ataangamizwa kuanzia Gaza, na Ashikeloni haitakuwa na watu tena!
Ashkelon, shall see, and fear, Gaza, also, which shall writhe in great anguish, Ekron, also, because abashed is her expectation, —and the king, shall perish, from Gaza, and, Ashkelon, not be inhabited;
6 Wageni watafanya makao yao katika Ashidodi, nami nitakiondoa kiburi cha Wafilisiti.
And there shall be seated a half-breed in Ashdod, —So will I cut off the arrogance of the Philistines;
7 Kwani nitaondoa damu yao katika vinywa vyao na machukizo yao kutoka kati ya meno yao. Ndipo watakapokuwa masalia kwa Mungu wetu kama ukoo katika Yuda, na Ekironi atakuwa kama Wayebusi.
And will take away his reeking prey out of his mouth, and his abominations, from between his teeth, but, he that is left, even he, shall belong to our God, —So shall he become as a chief in Judah, and, Ekron, as a Jebusite!
8 Nitaweka kambi kuzunguka nchi yangu kinyume cha majeshi ya adui hata hakuna atakayeweza kupita ndani yake tena, kwani hakuna mtesaji atakayeipita tena. Kwa kuwa sasa nitaangalia nchi yangu kwa macho yangu mwenyewe!
Then will I encamp about my house—against an army, against him that passeth by, and against him that returneth, neither shall an exactor, tread them down any more, —for, now, have I seen with mine own eyes.
9 Piga kelele kwa furaha, ewe binti Sayuni! Piga kelele kwa shangwe, ewe binti Yerusalem! Tazama! Mfalme wako anakuja kwako pamoja na uadilifu na anakuokoa. Ni mnyenyekevu, amepanda punda, mwanapunda.
Exult greatly, O daughter of Zion, Shout in triumph, O daughter of Jerusalem, Lo! thy king, cometh unto thee, vindicated and victorious, is he, —lowly, and riding upon an ass, yea, upon a colt, a young ass.
10 Ndipo nitakapoondoa kibandawazi kutoka Efraimu na farasi kutoka Yerusalemu, na upinde utaondolewa katika vita; kwani atasema amani kwa mataifa, na utawala wake utakuwa kutoka bahari hata bahari, na kutoka katika mto hadi miisho ya dunia!
So will he cut off the chariot out of Ephraim, and the horse out of Jerusalem, and the war-bow, shall be cut off, So shall he speak peace to the nations, and, his dominion, shall be from sea to sea, and from the river [Euphrates] to the ends of the earth.
11 Lakini kwenu, kwa sababu ya damu ya agano langu nanyi, nitawaweka wafungwa wenu huru kutoka shimoni pasipo na maji.
As for thee also, —By the blood of thy covenant, have I sent forth thy prisoners out of a pit, wherein is no water.
12 Rudini ngomeni, wafungwa wa matumaini! Hata leo natamka kwamba nitawarudishia mara mbili, kwani nimempinda Yuda kama upinde wangu.
Return to the stronghold, ye prisoners of hope, —Even to-day, do I declare—Double, will I return to thee!
13 Hata nimelijaza podo langu pamoja na Efraimu. Nimewainua wana wenu, Sayuni, kinyume cha wana wenu, Ugiriki, na amekufanya wewe, Sayuni, kama upanga wa shujaa!
For I have bent for me—Judah, As a bow, have I grasped Ephraim, Thus will I rouse up thy sons, O Zion, against the sons of Greece, and will make thee as the sword of a mighty one.
14 Yahwe atawatokea, na mishale yake itapiga kama radi! Kwa maana Yahwe Bwana wangu atapiga tarumbeta naye ataendelea pamoja na dhoruba kutoka Temani.
But, Yahweh, over them, will appear, and forth shall go, as lightning, his arrow, —Yea, My Lord Yahweh, with a horn, will blow, and will move along in the whirlwinds of the south.
15 Yahwe wa majeshi atawatetea, nao watawararua na kuyashinda mawe ya kombeo. Ndipo watakapo kunywa na kupiga kelele kama mtu aliyelewa kwa mvunyo, nao watajazwa na mvinyo kama mabakuri, kama pembe za madhabahu.
Yahweh of hosts, will throw a covering over them, so shall they eat, and trample underfoot sling-stones, and shall drink—shall shout as with wine, —and shall be filled like tossing-bowls, —like the corners of an altar.
16 Hivyo Yahwe Mungu wao atawaokoa siku hiyo; watakuwa kama kundi la kondoo lililo na watu wake, kwani watakuwa mapambo ya taji, yaliyoinuliwa juu ya nchi yake.
So will Yahweh their God, save them, on that day. yea, as a flock of sheep, his people, —for [they shall be like] the jewels of a diadem sparkling over his land.
17 Jinsi gani watakavyokuwa wazuri na warembo! vijana watastawi juu ya nafaka na bikra juu ya divai tamu!
For how excellent it is! Yea how beautiful! Corn, shall make the young men flourish, and new wine the maidens.