< Zekaria 9 >

1 Hili ni tamko la neno la Yahwe kuhusu nchi ya Hadraki na Damesiki. Kwa maana jicho la Yahwe liko juu ya wanadamu wote, na juu ya kabila zote za Israeli pia.
The burden of a word of YHWH against the land of Hadrach, and Demmeseh—his place of rest: (When to YHWH [is] the eye of man, And of all the tribes of Israel).
2 Azimio hili pia linaihusu Hamathi, inayopakana na Damesiki, na linahusu Tiro na Sidoni, japokuwa ni werevu sana.
And also Hamath borders thereon, Tyre and Sidon, for—very wise!
3 Tiro amejijengea ngome na kurundika fedha kama mavumbi na dhahabu safi kama matope mitaani.
And Tyre builds a bulwark for herself, And heaps silver as dust, And gold as mire of out-places.
4 Tazama! Bwana atamnyang'anya na kuharibu nguvu zake juu ya bahari, kwa hiyo atateketezwa kwa moto.
Behold, the Lord dispossesses her, And He has struck her force in the sea, And she is consumed with fire.
5 Ashikeloni ataona na kuogopa! Gaza pia atatemeka sana! Ekroni, tumanini lake litatikiswa! Mfalme ataangamizwa kuanzia Gaza, na Ashikeloni haitakuwa na watu tena!
Ashkelon sees and fears, Also Gaza, and she is exceedingly pained, Also Ekron—for her expectation dried up, And a king has perished from Gaza, And Ashkelon does not remain,
6 Wageni watafanya makao yao katika Ashidodi, nami nitakiondoa kiburi cha Wafilisiti.
“And a foreigner has dwelt in Ashdod, And I have cut off the excellence of the Philistines.
7 Kwani nitaondoa damu yao katika vinywa vyao na machukizo yao kutoka kati ya meno yao. Ndipo watakapokuwa masalia kwa Mungu wetu kama ukoo katika Yuda, na Ekironi atakuwa kama Wayebusi.
And turned aside his blood from his mouth, His abominations from between his teeth, And he has remained, even he, to our God, And he has been as a leader in Judah, And Ekron as a Jebusite.
8 Nitaweka kambi kuzunguka nchi yangu kinyume cha majeshi ya adui hata hakuna atakayeweza kupita ndani yake tena, kwani hakuna mtesaji atakayeipita tena. Kwa kuwa sasa nitaangalia nchi yangu kwa macho yangu mwenyewe!
And I have pitched a camp for My house, Because of the passer through, and of the returner, And an exactor does not pass through against them again, For now, I have seen with My eyes.
9 Piga kelele kwa furaha, ewe binti Sayuni! Piga kelele kwa shangwe, ewe binti Yerusalem! Tazama! Mfalme wako anakuja kwako pamoja na uadilifu na anakuokoa. Ni mnyenyekevu, amepanda punda, mwanapunda.
Rejoice exceedingly, O daughter of Zion, Shout, O daughter of Jerusalem, Behold, your King comes to you, Righteous and having salvation, Afflicted—and riding on a donkey, And on a colt—a son of female donkeys.
10 Ndipo nitakapoondoa kibandawazi kutoka Efraimu na farasi kutoka Yerusalemu, na upinde utaondolewa katika vita; kwani atasema amani kwa mataifa, na utawala wake utakuwa kutoka bahari hata bahari, na kutoka katika mto hadi miisho ya dunia!
And I have cut off the chariot from Ephraim, And the horse from Jerusalem, Indeed, the bow of battle has been cut off, And He has spoken peace to nations, And His rule [is] from sea to sea, And from the river to the ends of the earth.
11 Lakini kwenu, kwa sababu ya damu ya agano langu nanyi, nitawaweka wafungwa wenu huru kutoka shimoni pasipo na maji.
Also You—by the blood of Your covenant, I have sent Your prisoners out of the pit, There is no water in it.
12 Rudini ngomeni, wafungwa wa matumaini! Hata leo natamka kwamba nitawarudishia mara mbili, kwani nimempinda Yuda kama upinde wangu.
Return to a stronghold, You prisoners of the hope, Even today a second announcer I restore to you.
13 Hata nimelijaza podo langu pamoja na Efraimu. Nimewainua wana wenu, Sayuni, kinyume cha wana wenu, Ugiriki, na amekufanya wewe, Sayuni, kama upanga wa shujaa!
For I have trodden for Myself with Judah, I have filled a bow [with] Ephraim, And I have stirred up your sons, O Zion, Against your sons, O Javan, And I have set you as the sword of a hero.”
14 Yahwe atawatokea, na mishale yake itapiga kama radi! Kwa maana Yahwe Bwana wangu atapiga tarumbeta naye ataendelea pamoja na dhoruba kutoka Temani.
And YHWH appears for them, And His arrow has gone forth as lightning, And Lord YHWH blows with a horn, And He has gone with whirlwinds of the south.
15 Yahwe wa majeshi atawatetea, nao watawararua na kuyashinda mawe ya kombeo. Ndipo watakapo kunywa na kupiga kelele kama mtu aliyelewa kwa mvunyo, nao watajazwa na mvinyo kama mabakuri, kama pembe za madhabahu.
YHWH of Hosts covers them over, And they consumed, and subdued sling-stones, Indeed, they have drunk, They have made a noise as wine, And they have been full as a bowl, As corners of an altar.
16 Hivyo Yahwe Mungu wao atawaokoa siku hiyo; watakuwa kama kundi la kondoo lililo na watu wake, kwani watakuwa mapambo ya taji, yaliyoinuliwa juu ya nchi yake.
And their God YHWH has saved them in that day, As a flock of His people, For stones of a crown are displaying themselves over His ground.
17 Jinsi gani watakavyokuwa wazuri na warembo! vijana watastawi juu ya nafaka na bikra juu ya divai tamu!
For what His goodness! And what His beauty! Grain the young men, And new wine the virgins—make fruitful!

< Zekaria 9 >