< Zekaria 9 >

1 Hili ni tamko la neno la Yahwe kuhusu nchi ya Hadraki na Damesiki. Kwa maana jicho la Yahwe liko juu ya wanadamu wote, na juu ya kabila zote za Israeli pia.
The burden of the word of the LORD. In the land of Hadrach, and in Damascus shall be His resting-place; for the LORD'S is the eye of man and all the tribes of Israel.
2 Azimio hili pia linaihusu Hamathi, inayopakana na Damesiki, na linahusu Tiro na Sidoni, japokuwa ni werevu sana.
And Hamath also shall border thereon; Tyre and Zidon, for she is very wise.
3 Tiro amejijengea ngome na kurundika fedha kama mavumbi na dhahabu safi kama matope mitaani.
And Tyre did build herself a stronghold, and heaped up silver as the dust, and fine gold as the mire of the streets.
4 Tazama! Bwana atamnyang'anya na kuharibu nguvu zake juu ya bahari, kwa hiyo atateketezwa kwa moto.
Behold, the Lord will impoverish her, and He will smite her power into the sea; and she shall be devoured with fire.
5 Ashikeloni ataona na kuogopa! Gaza pia atatemeka sana! Ekroni, tumanini lake litatikiswa! Mfalme ataangamizwa kuanzia Gaza, na Ashikeloni haitakuwa na watu tena!
Ashkelon shall see it, and fear, Gaza also, and shall be sore pained, and Ekron, for her expectation shall be ashamed; and the king shall perish from Gaza, and Ashkelon shall not be inhabited.
6 Wageni watafanya makao yao katika Ashidodi, nami nitakiondoa kiburi cha Wafilisiti.
And a bastard shall dwell in Ashdod, and I will cut off the pride of the Philistines.
7 Kwani nitaondoa damu yao katika vinywa vyao na machukizo yao kutoka kati ya meno yao. Ndipo watakapokuwa masalia kwa Mungu wetu kama ukoo katika Yuda, na Ekironi atakuwa kama Wayebusi.
And I will take away his blood out of his mouth, and his detestable things from between his teeth, and he also shall be a remnant for our God; and he shall be as a chief in Judah, and Ekron as a Jebusite.
8 Nitaweka kambi kuzunguka nchi yangu kinyume cha majeshi ya adui hata hakuna atakayeweza kupita ndani yake tena, kwani hakuna mtesaji atakayeipita tena. Kwa kuwa sasa nitaangalia nchi yangu kwa macho yangu mwenyewe!
And I will encamp about My house against the army, that none pass through or return; and no oppressor shall pass through them any more; for now have I seen with Mine eyes.
9 Piga kelele kwa furaha, ewe binti Sayuni! Piga kelele kwa shangwe, ewe binti Yerusalem! Tazama! Mfalme wako anakuja kwako pamoja na uadilifu na anakuokoa. Ni mnyenyekevu, amepanda punda, mwanapunda.
Rejoice greatly, O daughter of Zion, shout, O daughter of Jerusalem; behold, thy king cometh unto thee, he is triumphant, and victorious, lowly, and riding upon an ass, even upon a colt the foal of an ass.
10 Ndipo nitakapoondoa kibandawazi kutoka Efraimu na farasi kutoka Yerusalemu, na upinde utaondolewa katika vita; kwani atasema amani kwa mataifa, na utawala wake utakuwa kutoka bahari hata bahari, na kutoka katika mto hadi miisho ya dunia!
And I will cut off the chariot from Ephraim, and the horse from Jerusalem, and the battle bow shall be cut off, and he shall speak peace unto the nations; and his dominion shall be from sea to sea, and from the River to the ends of the earth.
11 Lakini kwenu, kwa sababu ya damu ya agano langu nanyi, nitawaweka wafungwa wenu huru kutoka shimoni pasipo na maji.
As for thee also, because of the blood of thy covenant I send forth thy prisoners out of the pit wherein is no water.
12 Rudini ngomeni, wafungwa wa matumaini! Hata leo natamka kwamba nitawarudishia mara mbili, kwani nimempinda Yuda kama upinde wangu.
Return to the stronghold, ye prisoners of hope; even to-day do I declare that I will render double unto thee.
13 Hata nimelijaza podo langu pamoja na Efraimu. Nimewainua wana wenu, Sayuni, kinyume cha wana wenu, Ugiriki, na amekufanya wewe, Sayuni, kama upanga wa shujaa!
For I bend Judah for Me, I fill the bow with Ephraim; and I will stir up thy sons, O Zion, against thy sons, O Javan, and will make thee as the sword of a mighty man.
14 Yahwe atawatokea, na mishale yake itapiga kama radi! Kwa maana Yahwe Bwana wangu atapiga tarumbeta naye ataendelea pamoja na dhoruba kutoka Temani.
And the LORD shall be seen over them, and His arrow shall go forth as the lightning; and the Lord GOD will blow the horn, and will go with whirlwinds of the south.
15 Yahwe wa majeshi atawatetea, nao watawararua na kuyashinda mawe ya kombeo. Ndipo watakapo kunywa na kupiga kelele kama mtu aliyelewa kwa mvunyo, nao watajazwa na mvinyo kama mabakuri, kama pembe za madhabahu.
The LORD of hosts will defend them; and they shall devour, and shall tread down the sling-stones; and they shall drink, and make a noise as through wine; and they shall be filled like the basins, like the corners of the altar.
16 Hivyo Yahwe Mungu wao atawaokoa siku hiyo; watakuwa kama kundi la kondoo lililo na watu wake, kwani watakuwa mapambo ya taji, yaliyoinuliwa juu ya nchi yake.
And the LORD their God shall save them in that day as the flock of His people; for they shall be as the stones of a crown, glittering over His land.
17 Jinsi gani watakavyokuwa wazuri na warembo! vijana watastawi juu ya nafaka na bikra juu ya divai tamu!
For how great is their goodness, and how great is their beauty! Corn shall make the young men flourish, and new wine the maids.

< Zekaria 9 >