< Zekaria 7 >

1 Mwaka wa minne wa utawala mfalme Dario, siku ya nne ya mwezi wa Kisleu(ambao ni mwezi wa tisa), neno la Yahwe lilimjia Zekaria kusema.
And it came to pass in the fourth year of king Darius, that the word of the LORD came unto Zechariah in the fourth day of the ninth month, even in Chislev;
2 Watu wa Betheli wamemtuma Shareza, Regemu Meleki na watu wao kuomba mbele ya uso wa Yahwe.
When Bethel-sarezer, and Regem-melech and his men, had sent to entreat the favour of the LORD,
3 Wakaongea na makuhani waliokuwa katika nyumba ya Yahwe wa majeshi na kwa manabii; wakasema, “Je niomboleze katika mwezi wa tano kwa njia ya kufunga, kama nilivyofanya miaka mingi hii?”
and to speak unto the priests of the house of the LORD of hosts, and to the prophets, saying: 'Should I weep in the fifth month, separating myself, as I have done these so many years?'
4 Ndipo neno la Yahwe wa majeshi liliponijia kusema,
Then came the word of the LORD of hosts unto me, saying:
5 “Ongea na watu wote wa nchi na makuhani uwaambie, “Mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba katika hii miaka sabini, je kweli mlifunga kwa ajili yangu?
'Speak unto all the people of the land, and to the priests, saying: When ye fasted and mourned in the fifth and in the seventh month, even these seventy years, did ye at all fast unto Me, even to Me?
6 Na mlipokula na kunywa, hamkula na kunywa kwa ajili yenu wenyewe?
And when ye eat, and when ye drink, are ye not they that eat, and they that drink?
7 Je hayo siyo maneno aliyosema Yahwe kwa vinywa vya manabii wa zamani, mlipokuwa bado mnaishi Yerusalemu na miji ya kandokando yenye mafanikio na iliyokaa Negebu, na upande wa magharibi chini ya vilima?”
Should ye not hearken to the words which the LORD hath proclaimed by the former prophets, when Jerusalem was inhabited and in prosperity, and the cities thereof round about her, and the South and the Lowland were inhabited?'
8 Neno la Yahwe likamjia Zekaria kusema,
And the word of the LORD came unto Zechariah, saying:
9 “Yahwe wa majeshi asema hivi, 'Hukumuni kwa haki, uaminifu wa agano, na rehema. Kila mtu na amtendee hivi ndugu yake.
'Thus hath the LORD of hosts spoken, saying: Execute true judgment, and show mercy and compassion every man to his brother;
10 Juu ya mjane na yatima, mgeni, na masikini - usiwanyanyase, na asiwepo miongoni mwenu anayepanga madhara yoyote dhidi ya mwingine mioyoni mwenu.
and oppress not the widow, nor the fatherless, the stranger, nor the poor; and let none of you devise evil against his brother in your heart.
11 Lakini waliyashupaza mabega yao na hawakujari. Waliziba masikio yao ili wasisikie.
But they refused to attend, and turned a stubborn shoulder, and stopped their ears, that they might not hear.
12 Waliifanya mioyo yao kuwa migumu kama mwamba ili wasiisikie sheria au neno la Yahwe wa majeshi. Alipeleka ujumbe kwa watu nyakati za zamani kwa Roho wake, kwa vinywa vya manabii. Lakini watu hawakusikia, hivyo Yahwe wa majeshi aliwakasirikia sana.
Yea, they made their hearts as an adamant stone, lest they should hear the law, and the words which the LORD of hosts had sent by His spirit by the hand of the former prophets; therefore came there great wrath from the LORD of hosts.
13 Hata ikawa alipoita hawakusikia. Vilevile,” asema Yahwe wa majeshi, “wataniita, lakini sitasikiliza.
And it came to pass that, as He called, and they would not hear; so they shall call, and I will not hear, said the LORD of hosts;
14 Kwa maana nitawatawanya kwa upepo wa kisurisuri katika mataifa yote ambayo hawajawai kuyaona, na baada yao nchi itakuwa wazi. Kwa kuwa hakuna hata mmoja atakayepita au kukaa katika hiyo nchi kwa kuwa wameigeuza nchi yao yenye kupendeza kuwa isiyofaa.
but I will scatter them with a whirlwind among all the nations whom they have not known. Thus the land was desolate after them, so that no man passed through nor returned; for they laid the pleasant land desolate.'

< Zekaria 7 >