< Zekaria 7 >
1 Mwaka wa minne wa utawala mfalme Dario, siku ya nne ya mwezi wa Kisleu(ambao ni mwezi wa tisa), neno la Yahwe lilimjia Zekaria kusema.
And in the fourth yeere of King Darius, the worde of the Lord came vnto Zechariah in the fourth day of the ninth moneth, euen in Chisleu,
2 Watu wa Betheli wamemtuma Shareza, Regemu Meleki na watu wao kuomba mbele ya uso wa Yahwe.
For they had sent vnto the House of God Sharezer, and Regem-melech and their men to pray before the Lord,
3 Wakaongea na makuhani waliokuwa katika nyumba ya Yahwe wa majeshi na kwa manabii; wakasema, “Je niomboleze katika mwezi wa tano kwa njia ya kufunga, kama nilivyofanya miaka mingi hii?”
And to speake vnto the Priests, which were in the House of the Lord of hostes, and to the Prophets, saying, Should I weepe in the fift moneth, and separate my selfe as I haue done these so many yeeres?
4 Ndipo neno la Yahwe wa majeshi liliponijia kusema,
Then came the word of the Lord of hostes vnto me, saying,
5 “Ongea na watu wote wa nchi na makuhani uwaambie, “Mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba katika hii miaka sabini, je kweli mlifunga kwa ajili yangu?
Speake vnto all the people of the land, and to the Priests, and say, When ye fasted, and mourned in the fift and seuenth moneth, euen the seuentie yeeres, did ye fast vnto me? doe I approoue it?
6 Na mlipokula na kunywa, hamkula na kunywa kwa ajili yenu wenyewe?
And when ye did eate, and when ye did drinke, did ye not eate for your selues, and drinke for your selues?
7 Je hayo siyo maneno aliyosema Yahwe kwa vinywa vya manabii wa zamani, mlipokuwa bado mnaishi Yerusalemu na miji ya kandokando yenye mafanikio na iliyokaa Negebu, na upande wa magharibi chini ya vilima?”
Should ye not heare the wordes, which the Lord hath cryed by the ministerie of the former Prophets when Ierusalem was inhabited, and in prosperitie, and the cities thereof round about her, when the South and the plaine was inhabited?
8 Neno la Yahwe likamjia Zekaria kusema,
And the worde of the Lord came vnto Zechariah, saying,
9 “Yahwe wa majeshi asema hivi, 'Hukumuni kwa haki, uaminifu wa agano, na rehema. Kila mtu na amtendee hivi ndugu yake.
Thus speaketh the Lord of hostes, saying, Execute true iudgement, and shewe mercy and compassion, euery man to his brother,
10 Juu ya mjane na yatima, mgeni, na masikini - usiwanyanyase, na asiwepo miongoni mwenu anayepanga madhara yoyote dhidi ya mwingine mioyoni mwenu.
And oppresse not the widowe, nor the fatherles, the stranger nor the poore, and let none of you imagine euil against his brother in your heart.
11 Lakini waliyashupaza mabega yao na hawakujari. Waliziba masikio yao ili wasisikie.
But they refused to hearken, and pulled away the shoulder, and stopped their eares, that they should not heare.
12 Waliifanya mioyo yao kuwa migumu kama mwamba ili wasiisikie sheria au neno la Yahwe wa majeshi. Alipeleka ujumbe kwa watu nyakati za zamani kwa Roho wake, kwa vinywa vya manabii. Lakini watu hawakusikia, hivyo Yahwe wa majeshi aliwakasirikia sana.
Yea, they made their hearts as an adamant stone, least they should heare the Lawe and the wordes which the Lord of hostes sent in his spirit by the ministerie of ye former Prophets: therefore came a great wrath from the Lord of hostes.
13 Hata ikawa alipoita hawakusikia. Vilevile,” asema Yahwe wa majeshi, “wataniita, lakini sitasikiliza.
Therefore it is come to passe, that as he cried, and they would not heare, so they cried, and I would not heare, sayth the Lord of hostes.
14 Kwa maana nitawatawanya kwa upepo wa kisurisuri katika mataifa yote ambayo hawajawai kuyaona, na baada yao nchi itakuwa wazi. Kwa kuwa hakuna hata mmoja atakayepita au kukaa katika hiyo nchi kwa kuwa wameigeuza nchi yao yenye kupendeza kuwa isiyofaa.
But I scattered them among all the nations, whom they knew not: thus the land was desolate after them, that no man passed through nor returned: for they layd the pleasant land waste.