< Zekaria 6 >

1 Kisha nikageuka na kuinua macho na nikaona vibandawazi vinne vya farasi vikija kutoka kati ya milima miwili; na milima hiyo ilikuwa imetengenezwa kwa shaba.
And I lifted up mine eyes again, and looked, and, behold, there came four chariots out from between two mountains; and the mountains were mountains of brass.
2 Kibandawazi cha kwanza kilikuwa na farasi wekundu, kibandawazi cha pili kilikuwa na farasi weusi,
In the first chariot were red horses; and in the second chariot, black horses;
3 kibandawazi cha tatu kilikuwa na farasi weupe, na kibandawazi cha nne kilikuwa na farasi wa kijivu.
and in the third chariot, white horses; and in the fourth chariot, spotted-red horses.
4 Hivyo nikamwuliza malaika aliyesema nami, “Ni vitu gani hivi bwana wangu?”
Then I spake, and said to the angel that talked with me, What are these, my lord?
5 Malaika akajibu na kuniambia, “Hizi ni pepo nne za mbinguni zisimamazo mbele ya Bwana wa dunia yote.
And the angel answered and said to me, These are the four Winds of heaven, which go forth from standing before the Lord of all the earth.
6 Lenye farasi weusi linakwenda nchi ya kaskazini; farasi weupe wanakwenda nchi ya magharibi; na farasi wa kijivu wanakwenda nchi ya kusini.”
The black horses, which are thereto, go forth into the north country, and the white go forth after them; and the spotted go forth into the south country.
7 Farasi hawa wenye nguvu walitoka na wanatafuta kwenda na kuzunguka juu ya nchi, hivyo malaika akasema, “Nendeni na mzunguke juu ya nchi!” nao wakaenda juu ya dunia yote.
And the red ones went forth, and sought to go, even to walk to and fro through the earth. And he said, Go, walk ye to and fro through the earth! So they walked to and fro through the earth.
8 Kisha akaniita na kuniambia, “Tazama wale wanaokwenda nchi ya kaskazini, wataituliza roho yangu juu nchi hiyo.”
Then he cried to me, and spake to me, saying, Behold, these that go forth toward the land of the North shall execute my wrath against the land of the North.
9 Hivyo neno la Yahwe likanijia kusema,
And the word of Jehovah came to me, saying:
10 “Chukua sadaka kutoka kwa waliohamishwa - kutoka kwa Helidai, Tobiya na Yedaya - leo hii uende na kuipeleka katika nyumba ya Yosia mwana wa Zefania, aliyetoka Babeli.
Take from those of the captivity, from Heldai, from Tobijah, and from Jedaiah, and come thou the same day, and go into the house of Josiah, the son of Zephaniah, whither they are come from Babylon;
11 Kisha uchukue fedha na dhahabu, ufanye taji na uivike katika kichwa cha Yoshua mwana wa Yehosadaki kuhani mkuu.
take from them silver and gold, and make a crown, and set it upon the head of Joshua, the son of Josedech, the high-priest,
12 Ongea naye na useme, Yahwe wa majeshi asema hivi: Mtu huyu, jina lake Tawi! Naye atakuwa alipo na kisha atajenga hekalu la Yahwe!
and speak to him, saying, Thus saith Jehovah of hosts: — Behold a man whose name is the Branch, He shall spring up from his place, And he shall build the temple of Jehovah.
13 Ndiye atakayejenga hekalu la Yahwe naye atauinua utukufu wake; kisha ataketi na kutawala katika kiti chake cha enzi. Atakuwa kuhani juu ya kiti cha enzi na ufahamu wa amani utakuwa kati ya vyote viwili.
He shall build the temple of Jehovah, And he shall bear the majesty, And sit and rule upon his throne, And be a priest upon his throne, And the counsel of peace shall be between them both.
14 Taji itawekwa hekaluni mwa Yahwe kwa heshima ya Heldai, Tobiya na Yedaya na kama kumbukumbu ya ukarimu wa mwana wa Zefania.
And the crown shall be to Helem, and to Tobijah, and to Jedaiah, and to Hen, the son of Zephaniah, for a memorial in the temple of Jehovah.
15 Ndipo waliombali watakapokuja na kulijenga hekalu la Yahwe, hivyo mtajua kuwa Yahwe wa majeshi amenituma kwenu; kwani ikiwa kweli mnaisikiliza sauti ya Yahwe Mungu wenu hili litatendeka!”
And they that are far off shall come and build in the temple of Jehovah; and ye shall know that Jehovah of hosts hath sent me to you. And this shall come to pass, if ye will diligently obey the voice of Jehovah, your God.

< Zekaria 6 >