< Zekaria 6 >
1 Kisha nikageuka na kuinua macho na nikaona vibandawazi vinne vya farasi vikija kutoka kati ya milima miwili; na milima hiyo ilikuwa imetengenezwa kwa shaba.
And I turned, and I lifted up my eyes and I saw. And behold, four four-horse chariots went out from the middle of two mountains. And the mountains were mountains of brass.
2 Kibandawazi cha kwanza kilikuwa na farasi wekundu, kibandawazi cha pili kilikuwa na farasi weusi,
In the first chariot were red horses, and in the second chariot were black horses,
3 kibandawazi cha tatu kilikuwa na farasi weupe, na kibandawazi cha nne kilikuwa na farasi wa kijivu.
and in the third chariot were white horses, and in the fourth chariot were speckled horses, and they were strong.
4 Hivyo nikamwuliza malaika aliyesema nami, “Ni vitu gani hivi bwana wangu?”
And I responded and said to the angel who was speaking with me, “What are these, my lord?”
5 Malaika akajibu na kuniambia, “Hizi ni pepo nne za mbinguni zisimamazo mbele ya Bwana wa dunia yote.
And the angel answered and said to me, “These are the four winds of heaven, which go forth to stand in the presence of the Sovereign of all the earth.”
6 Lenye farasi weusi linakwenda nchi ya kaskazini; farasi weupe wanakwenda nchi ya magharibi; na farasi wa kijivu wanakwenda nchi ya kusini.”
The one with the black horses was departing into the land of the North, and the white went forth after them, and the speckled went forth towards the land of the South.
7 Farasi hawa wenye nguvu walitoka na wanatafuta kwenda na kuzunguka juu ya nchi, hivyo malaika akasema, “Nendeni na mzunguke juu ya nchi!” nao wakaenda juu ya dunia yote.
Yet those who were the most strong, went out, and sought to go and to roam quickly through all the earth. And he said, “Go, walk throughout the earth.” And they walked throughout the earth.
8 Kisha akaniita na kuniambia, “Tazama wale wanaokwenda nchi ya kaskazini, wataituliza roho yangu juu nchi hiyo.”
And he called me and spoke with me, saying, “Behold, those who go forth to the land of the North, have quieted my spirit in the land of the North.”
9 Hivyo neno la Yahwe likanijia kusema,
And the word of the Lord came to me, saying:
10 “Chukua sadaka kutoka kwa waliohamishwa - kutoka kwa Helidai, Tobiya na Yedaya - leo hii uende na kuipeleka katika nyumba ya Yosia mwana wa Zefania, aliyetoka Babeli.
From those of the captivity, take from Heldai, and from Tobijah, and from Jedaiah. You will approach in that day, and you will go into the house of Josiah, the son of Zephaniah, who came from Babylon.
11 Kisha uchukue fedha na dhahabu, ufanye taji na uivike katika kichwa cha Yoshua mwana wa Yehosadaki kuhani mkuu.
And you will take gold and silver; and you will make crowns, and you will set them on the head of Jesus the son of Jehozadak, the high priest.
12 Ongea naye na useme, Yahwe wa majeshi asema hivi: Mtu huyu, jina lake Tawi! Naye atakuwa alipo na kisha atajenga hekalu la Yahwe!
And you will speak to him, saying: Thus says the Lord of hosts, saying: Behold, a man; the Rising is his name. And under him, he will rise up, and he will build a temple to the Lord.
13 Ndiye atakayejenga hekalu la Yahwe naye atauinua utukufu wake; kisha ataketi na kutawala katika kiti chake cha enzi. Atakuwa kuhani juu ya kiti cha enzi na ufahamu wa amani utakuwa kati ya vyote viwili.
And he will raise a temple to the Lord. And he will carry the glory, and he will sit and rule upon his throne. And he will be a priest upon his throne, and a counsel of peace will be between the two of them.
14 Taji itawekwa hekaluni mwa Yahwe kwa heshima ya Heldai, Tobiya na Yedaya na kama kumbukumbu ya ukarimu wa mwana wa Zefania.
And the crowns will be to Heldai, and Tobijah, and Jedaiah, as well as to Hem, the son of Zephaniah, as a memorial in the temple of the Lord.
15 Ndipo waliombali watakapokuja na kulijenga hekalu la Yahwe, hivyo mtajua kuwa Yahwe wa majeshi amenituma kwenu; kwani ikiwa kweli mnaisikiliza sauti ya Yahwe Mungu wenu hili litatendeka!”
And those who are far away, will approach, and will build in the temple of the Lord. And you will know that the Lord of hosts sent me to you. Yet this shall be only if, when hearing, you will have heeded the voice of the Lord your God.