< Zekaria 14 >

1 Tazama! Siku ya Yahwe inakuja wakati mateka wenu watakapogawanywa katikati yenu.
Siehe, ein Tag kommt dem Jehovah, da man die Beute teilt in deiner Mitte.
2 Kwa maana nitayakusanya mataifa yote kinyume cha Yerusalemu kwa vita na mji utatekwa. Nyumba zitatekwa na wanawake watabakwa. Nusu ya mji itapelekwa matekani, lakini kumbukumbu ya watu haitaondolewa mjini.
Und Ich versammle alle Völkerschaften nach Jerusalem zum Streit, und die Stadt wird erobert und die Häuser werden geplündert und die Weiber geschändet, und die Hälfte der Stadt zieht in die Verbannung hinaus, aber das übrige des Volkes wird nicht ausgerottet aus der Stadt.
3 Lakini Yahwe ataondoka na kufanya vita dhidi ya mataifa kama apigavyo vita katika siku ya vita.
Und wider diese Völkerschaften wird ausziehen Jehovah und streiten, wie am Tage, da Er stritt am Tage des Kampfes.
4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, uliopo kando ya Yerusalemu upande wa mashariki. Mlima wa Mizeituni utagawanyika katikati kati ya mashariki na magharibi kwa bonde kubwa sana na nusu ya mlima itarudi nyuma kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
Und Seine Füße werden an jenem Tag auf dem Berg der Ölbäume stehen, der vor Jerusalem gen Osten ist. Und der Berg der Ölbäume wird sich spalten in seine Hälfte gen Aufgang und zum Meere hin in eine sehr große Schlucht, und eine Hälfte des Berges weicht hin gen Mitternacht, und seine Hälfte gen Mittag.
5 Ndipo mtakapokimbia katika bonde kati ya milima ya Yahwe, kwa kuwa bonde kati ya hiyo milima litafika hata Azali. Mtakimbia kama siku mliyokimbia tetemeko la nchi siku za Uzia, mfalme wa Yuda. Ndipo Yahwe Mungu wangu atakapokuja na watakatifu wake wote.
Und ihr werdet fliehen durch die Schlucht Meiner Berge; denn die Schlucht der Berge wird reichen bis Azal; und ihr flieht, wie ihr geflohen seid vor dem Erdbeben in den Tage Ussijahs, des Königs von Jehudah, und es kommt Jehovah, mein Gott; all Seine Heiligen mit Dir.
6 Hakutakuwa na nuru katika siku hiyo, lakini hakuna baridi wala barafu.
Und es geschieht an jenem Tage: kein Licht wird sein, nur Kälte und Frost.
7 Siku hiyo, siku aijuaye Yahwe peke yake, hakutakuwa tena na mchana wala usiku, kwani jioni itakuwa wakati wa nuru.
Und es wird ein Tag sein, - dem Jehovah ist er bekannt - nicht Tag und nicht Nacht, und zur Zeit des Abends wird Licht werden.
8 Siku hiyo maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu. Nusu yake yatatiririka kuelekea bahari ya mashariki na nusu bahari ya magharibi, wakati wa masika na wakati wa kiangazi.
Und es geschieht an jenem Tag, daß lebendige Wasser ausgehen von Jerusalem, zur Hälfte nach dem vorderen Meere und zur Hälfte nach dem hinteren Meer. Im Sommer und im Winter wird es sein.
9 Yahwe atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo kutakuwa na Yahwe, Mungu mmoja, na jina lake pekee.
Und König wird Jehovah sein über die ganze Erde. An jenem Tage wird Jehovah einer sein, und Sein Name einer.
10 Nchi yote itakuwa kama Araba, kuanzia Geba hadi Rimoni kusini mwa Yerusalemu. Na Yerusalemu itaendelea kuwa juu. Ataishi mahali pake mwenyewe, kutoka lango la Benjamini hata mahali lilipokuwa lango la kwanza, hata Lango la Pembeni, na kutoka Mnara wa Hananeli hata shinikizo la mfalme.
Das ganze Land wird ringsum sein wie das Gefilde von Geba bis nach Rimmon, mittäglich von Jerusalem, und es wird erhöht sein und bewohnt sein an seiner Stelle, vom Tore Benjamins bis zum Orte des ersten Tores bis zum Tore der Ecken und dem Turm Chananeels bis zu den Kelterkufen des Königs.
11 Watu watakaa Yerusalemu na hakutakuwa na maangamizi kamili tena kutoka kwa Mungu dhidi yao. Yerusalemu itakuwa salama.
Und sie werden darin wohnen, und kein Bann wird mehr sein, und man wohnt in Jerusalem in Sicherheit.
12 Hii itakuwa tauni ambayo kwayo Yahwe atawapiga jamaa zote za watu wapigao vita juu ya Yerusalemu: miili yao itaoza hata wakiwa wamesimama kwa miguu yao. Macho yao yataoza katika matundu yake na ndimi zao zitaoza katika vinywa vyao.
Dies aber wird die Plage sein, womit Jehovah plagt alle Völker, die wider Jerusalem ausrücken: sein Fleisch schwindet dahin, da er noch auf seinen Füßen steht, und seine Augen schwinden dahin in ihren Höhlen, und seine Zunge schwindet dahin in ihrem Munde.
13 Siku hiyo ile hofu kuu kutoka kwa Yahwe itakuwa miongoni mwao. Kila mmoja ataushika mkono wa mwingine, na mkono wa mwingine utainuliwa kinyume cha mkono wa mwenzake.
Und an jenem Tage wird geschehen, daß viel Toben von Jehovah unter ihnen sein wird: und der Mann wird die Hand seines Genossen erfassen, und seine Hand steigt auf über die Hand seines Genossen.
14 Yuda pia atapigana na Yerusalemu. Watakusanya utajiri wa mataifa yote yanayowazunguka - dhahabu, fedha, na wingi wa nguo safi.
Und auch Jehudah wird wider Jerusalem streiten; und gesammelt wird das Vermögen aller Völkerschaften ringsumher, sehr viel Gold und Silber und Kleider.
15 Tauni itakuwa pia juu ya farasi na nyumbu, ngamia na punda, na kila mnyama katika kambi hizo atapigwa kwa hilo pigo.
Und ebenso wird sein die Plage des Rosses, des Maultiers, des Kamels und des Esels, und alles Viehs, das in jenen Heerlagern ist, wie diese Plage.
16 Kisha itakuwa wote watakaosalia katika mataifa yaliyo kinyume na Yerusalemu watakwenda mwaka kwa mwaka kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, na kutunza Sikukuu ya Vibanda.
Und wird geschehen, daß alle von allen Völkerschaften, die übrigblieben, die wider Jerusalem gekommen waren, heraufziehen werden von Jahr zu Jahr, um anzubeten den König Jehovah der Heerscharen, und das Fest der Laubhütten zu feiern.
17 Na itakuwa kwamba ikiwa mtu yeyote kutoka katika mataifa yote ya dunia haendi Yerusalemu kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, ndipo Yahwe hataleta mvua juu yao.
Und es soll geschehen, wer von den Familien der Erde nicht heraufzieht nach Jerusalem, um den König Jehovah der Heerscharen anzubeten, auf ihnen wird kein Regen sein.
18 Na ikiwa nchi ya Misri hawatakwenda, ndipo hawatapata mvua. Tauni kutoka kwa Yahwe itayashambulia mataifa yote yasiyokwea kutunza Sikukuu ya Vibanda.
Und wenn die Familie Ägypten nicht heraufzieht, und nicht kommt, und nicht mit ihnen ist, so wird sein die Plage, womit Jehovah die Völkerschaften schlägt, die nicht heraufzogen, das Fest der Laubhütten zu feiern.
19 Hii itakuwa ni adhabu kwa Misri na adhabu kwa kila taifa lisilopanda kutunza Sikukuu ya Vibanda.
Das wird die Sünde Ägyptens sein, und die Sünde all der Völkerschaften, die nicht heraufzogen, das Fest der Laubhütten zu feiern.
20 Lakini katika siku hiyo, kengele za farasi zitasema, “Jitengeni kwa ajili ya Yahwe,” na makalai katika nyumba ya Yahwe yatakuwa kama mabakuri mbele ya madhabahu.
An jenem Tage wird sein auf den Glöckchen der Rosse: Heiligkeit dem Jehovah! Und die Töpfe werden sein im Haus Jehovahs wie die Sprengbecken vor dem Altar.
21 Kwa kuwa kila chungu katika Yerusalemu na Yuda kitatengwa kwa ajili ya Yahwe wa majeshi na kila mmoja aletaye sadaka atakula ndani yake na kuyachemshia. Hakutakuwa na wafanyabiashara tena katika nyumba ya Yahwe wa majeshi siku hiyo.
Und jeder Topf in Jerusalem und in Jehudah wird Heiligkeit sein dem Jehovah der Heerscharen; und alle, die opfern, werden kommen und davon nehmen und darin kochen, und wird kein Kanaaniter mehr im Hause Jehovahs der Heerscharen sein an jenem Tage.

< Zekaria 14 >