< Zekaria 14 >

1 Tazama! Siku ya Yahwe inakuja wakati mateka wenu watakapogawanywa katikati yenu.
Voici venir un jour de Yahvé, où votre butin sera partagé au milieu de vous.
2 Kwa maana nitayakusanya mataifa yote kinyume cha Yerusalemu kwa vita na mji utatekwa. Nyumba zitatekwa na wanawake watabakwa. Nusu ya mji itapelekwa matekani, lakini kumbukumbu ya watu haitaondolewa mjini.
Car je rassemblerai toutes les nations contre Jérusalem pour qu'elles combattent; la ville sera prise, les maisons pillées, les femmes violées. La moitié de la ville partira en captivité, et le reste du peuple ne sera pas retranché de la ville.
3 Lakini Yahwe ataondoka na kufanya vita dhidi ya mataifa kama apigavyo vita katika siku ya vita.
Alors Yahvé sortira et combattra contre ces nations, comme au jour du combat.
4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, uliopo kando ya Yerusalemu upande wa mashariki. Mlima wa Mizeituni utagawanyika katikati kati ya mashariki na magharibi kwa bonde kubwa sana na nusu ya mlima itarudi nyuma kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
Ses pieds se tiendront en ce jour-là sur la montagne des Oliviers, qui est devant Jérusalem à l'est; et la montagne des Oliviers se fendra en deux d'est en ouest, formant une très grande vallée. La moitié de la montagne se déplacera vers le nord, et l'autre moitié vers le sud.
5 Ndipo mtakapokimbia katika bonde kati ya milima ya Yahwe, kwa kuwa bonde kati ya hiyo milima litafika hata Azali. Mtakimbia kama siku mliyokimbia tetemeko la nchi siku za Uzia, mfalme wa Yuda. Ndipo Yahwe Mungu wangu atakapokuja na watakatifu wake wote.
Vous fuirez par la vallée de mes montagnes, car la vallée des montagnes s'étendra jusqu'à Azel. Oui, vous fuirez, comme vous avez fui avant le tremblement de terre, à l'époque d'Ozias, roi de Juda. Yahvé mon Dieu viendra, et tous les saints avec vous.
6 Hakutakuwa na nuru katika siku hiyo, lakini hakuna baridi wala barafu.
Il arrivera en ce jour-là qu'il n'y aura ni lumière, ni froid, ni gelée.
7 Siku hiyo, siku aijuaye Yahwe peke yake, hakutakuwa tena na mchana wala usiku, kwani jioni itakuwa wakati wa nuru.
Ce sera un jour unique, connu de Yahvé - ni jour, ni nuit - mais il arrivera qu'à l'heure du soir il y aura de la lumière.
8 Siku hiyo maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu. Nusu yake yatatiririka kuelekea bahari ya mashariki na nusu bahari ya magharibi, wakati wa masika na wakati wa kiangazi.
En ce jour-là, des eaux vives sortiront de Jérusalem, pour moitié vers la mer orientale et pour moitié vers la mer occidentale. Il en sera ainsi en été et en hiver.
9 Yahwe atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo kutakuwa na Yahwe, Mungu mmoja, na jina lake pekee.
Yahvé sera roi sur toute la terre. En ce jour-là, Yahvé sera unique, et son nom sera unique.
10 Nchi yote itakuwa kama Araba, kuanzia Geba hadi Rimoni kusini mwa Yerusalemu. Na Yerusalemu itaendelea kuwa juu. Ataishi mahali pake mwenyewe, kutoka lango la Benjamini hata mahali lilipokuwa lango la kwanza, hata Lango la Pembeni, na kutoka Mnara wa Hananeli hata shinikizo la mfalme.
Tout le pays sera rendu semblable à la plaine, depuis Guéba jusqu'à Rimmon, au sud de Jérusalem; elle s'élèvera et habitera à sa place, depuis la porte de Benjamin jusqu'à la place de la première porte, jusqu'à la porte d'angle, et depuis la tour de Hananel jusqu'aux pressoirs du roi.
11 Watu watakaa Yerusalemu na hakutakuwa na maangamizi kamili tena kutoka kwa Mungu dhidi yao. Yerusalemu itakuwa salama.
Les hommes y habiteront, et il n'y aura plus de malédiction; mais Jérusalem habitera en sécurité.
12 Hii itakuwa tauni ambayo kwayo Yahwe atawapiga jamaa zote za watu wapigao vita juu ya Yerusalemu: miili yao itaoza hata wakiwa wamesimama kwa miguu yao. Macho yao yataoza katika matundu yake na ndimi zao zitaoza katika vinywa vyao.
Voici la plaie dont Yahvé frappera tous les peuples qui auront combattu contre Jérusalem: leur chair se consumera pendant qu'ils se tiendront sur leurs pieds, leurs yeux se consumeront dans leurs orbites, et leur langue se consumera dans leur bouche.
13 Siku hiyo ile hofu kuu kutoka kwa Yahwe itakuwa miongoni mwao. Kila mmoja ataushika mkono wa mwingine, na mkono wa mwingine utainuliwa kinyume cha mkono wa mwenzake.
En ce jour-là, il y aura parmi eux une grande panique de la part de l'Éternel; chacun saisira la main de son prochain, et sa main se lèvera contre la main de son prochain.
14 Yuda pia atapigana na Yerusalemu. Watakusanya utajiri wa mataifa yote yanayowazunguka - dhahabu, fedha, na wingi wa nguo safi.
Juda aussi combattra à Jérusalem; et les richesses de toutes les nations d'alentour seront rassemblées: or, argent et vêtements, en grande abondance.
15 Tauni itakuwa pia juu ya farasi na nyumbu, ngamia na punda, na kila mnyama katika kambi hizo atapigwa kwa hilo pigo.
Une telle plaie tombera sur le cheval, sur la mule, sur le chameau, sur l'âne et sur tous les animaux qui seront dans ces camps.
16 Kisha itakuwa wote watakaosalia katika mataifa yaliyo kinyume na Yerusalemu watakwenda mwaka kwa mwaka kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, na kutunza Sikukuu ya Vibanda.
Il arrivera que tous ceux qui resteront de toutes les nations qui sont venues contre Jérusalem monteront d'année en année pour se prosterner devant le roi, l'Yahvé des armées, et pour célébrer la fête des tentes.
17 Na itakuwa kwamba ikiwa mtu yeyote kutoka katika mataifa yote ya dunia haendi Yerusalemu kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, ndipo Yahwe hataleta mvua juu yao.
Celui de toutes les familles de la terre qui ne montera pas à Jérusalem pour se prosterner devant le roi, l'Éternel des armées, celui-là ne recevra pas de pluie.
18 Na ikiwa nchi ya Misri hawatakwenda, ndipo hawatapata mvua. Tauni kutoka kwa Yahwe itayashambulia mataifa yote yasiyokwea kutunza Sikukuu ya Vibanda.
Si la famille d'Égypte ne monte pas et ne vient pas, il ne pleuvra pas non plus sur elle. Ce sera la plaie dont Yahvé frappera les nations qui ne monteront pas pour célébrer la fête des tabernacles.
19 Hii itakuwa ni adhabu kwa Misri na adhabu kwa kila taifa lisilopanda kutunza Sikukuu ya Vibanda.
Ce sera le châtiment de l'Égypte et le châtiment de toutes les nations qui ne monteront pas pour célébrer la fête des kermesses.
20 Lakini katika siku hiyo, kengele za farasi zitasema, “Jitengeni kwa ajili ya Yahwe,” na makalai katika nyumba ya Yahwe yatakuwa kama mabakuri mbele ya madhabahu.
En ce jour-là, on inscrira sur les cloches des chevaux: « SAINTETÉ À YAHVÉ »; et les marmites de la maison de Yahvé seront comme les coupes devant l'autel.
21 Kwa kuwa kila chungu katika Yerusalemu na Yuda kitatengwa kwa ajili ya Yahwe wa majeshi na kila mmoja aletaye sadaka atakula ndani yake na kuyachemshia. Hakutakuwa na wafanyabiashara tena katika nyumba ya Yahwe wa majeshi siku hiyo.
Oui, toutes les marmites de Jérusalem et de Juda seront consacrées à l'Éternel des armées; et tous ceux qui sacrifient viendront s'en servir et cuisineront dedans. En ce jour-là, il n'y aura plus de Cananéen dans la maison de l'Éternel des armées.

< Zekaria 14 >