< Zekaria 14 >

1 Tazama! Siku ya Yahwe inakuja wakati mateka wenu watakapogawanywa katikati yenu.
There! a day [is] coming of Yahweh and it will be divided plunder your in midst your.
2 Kwa maana nitayakusanya mataifa yote kinyume cha Yerusalemu kwa vita na mji utatekwa. Nyumba zitatekwa na wanawake watabakwa. Nusu ya mji itapelekwa matekani, lakini kumbukumbu ya watu haitaondolewa mjini.
And I will gather all the nations - to Jerusalem for battle and it will be captured the city and they will be plundered the houses and the women (they will be lain with *Q(K)*) and it will go out half of the city in exile and [the] rest of the people not it will be cut off from the city.
3 Lakini Yahwe ataondoka na kufanya vita dhidi ya mataifa kama apigavyo vita katika siku ya vita.
And he will go forth Yahweh and he will fight against the nations those like [the] day (fought he *L(abh)*) in a day of battle.
4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, uliopo kando ya Yerusalemu upande wa mashariki. Mlima wa Mizeituni utagawanyika katikati kati ya mashariki na magharibi kwa bonde kubwa sana na nusu ya mlima itarudi nyuma kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
And they will stand feet his on the day that on [the] mountain of Olives which [is] on [the] face of Jerusalem from [the] east and it will be split open [the] mountain of Olives from middle its east-ward and west-ward a valley great very and it will depart half of the mountain north-ward and half of it south-ward.
5 Ndipo mtakapokimbia katika bonde kati ya milima ya Yahwe, kwa kuwa bonde kati ya hiyo milima litafika hata Azali. Mtakimbia kama siku mliyokimbia tetemeko la nchi siku za Uzia, mfalme wa Yuda. Ndipo Yahwe Mungu wangu atakapokuja na watakatifu wake wote.
And you will flee [the] valley of mountains my for it will reach [the] valley of mountains to Azal and you will flee just as you fled from before the earthquake in [the] days of Uzziah [the] king of Judah and he will come Yahweh God my all holy [ones] [will be] with you.
6 Hakutakuwa na nuru katika siku hiyo, lakini hakuna baridi wala barafu.
And it will be on the day that not it will be light splendid [ones] (and frost. *Q(K)*)
7 Siku hiyo, siku aijuaye Yahwe peke yake, hakutakuwa tena na mchana wala usiku, kwani jioni itakuwa wakati wa nuru.
And it will be a day one it it will be known to Yahweh not day and not night and it will be to [the] time of evening it will be light.
8 Siku hiyo maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu. Nusu yake yatatiririka kuelekea bahari ya mashariki na nusu bahari ya magharibi, wakati wa masika na wakati wa kiangazi.
And it will be - on the day that they will go out waters living from Jerusalem half of them to the sea eastern and half of them to the sea western in the summer and in the winter it will be.
9 Yahwe atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo kutakuwa na Yahwe, Mungu mmoja, na jina lake pekee.
And he will become Yahweh king over all the earth on the day that he will be Yahweh one and name his one.
10 Nchi yote itakuwa kama Araba, kuanzia Geba hadi Rimoni kusini mwa Yerusalemu. Na Yerusalemu itaendelea kuwa juu. Ataishi mahali pake mwenyewe, kutoka lango la Benjamini hata mahali lilipokuwa lango la kwanza, hata Lango la Pembeni, na kutoka Mnara wa Hananeli hata shinikizo la mfalme.
It will change all the land like the Arabah from Geba to Rimmon [the] south of Jerusalem and it will rise and it will remain in place its from [the] gate of Benjamin to [the] place of [the] gate first to [the] gate of the corners and [the] tower of Hananel to [the] wine-presses of the king.
11 Watu watakaa Yerusalemu na hakutakuwa na maangamizi kamili tena kutoka kwa Mungu dhidi yao. Yerusalemu itakuwa salama.
And people will dwell in it and total destruction not it will be again and it will remain Jerusalem to security.
12 Hii itakuwa tauni ambayo kwayo Yahwe atawapiga jamaa zote za watu wapigao vita juu ya Yerusalemu: miili yao itaoza hata wakiwa wamesimama kwa miguu yao. Macho yao yataoza katika matundu yake na ndimi zao zitaoza katika vinywa vyao.
And this - it will be the plague which he will strike Yahweh all the peoples which they have waged war on Jerusalem he will cause to rot - flesh its and it [is] standing on feet its and eyes its they will rot in sockets their and tongue its it will rot in mouth their.
13 Siku hiyo ile hofu kuu kutoka kwa Yahwe itakuwa miongoni mwao. Kila mmoja ataushika mkono wa mwingine, na mkono wa mwingine utainuliwa kinyume cha mkono wa mwenzake.
And it will be on the day that it will be a panic of Yahweh great among them and they will take hold of each [the] hand of neighbor his and it will go up hand his on [the] hand of neighbor his.
14 Yuda pia atapigana na Yerusalemu. Watakusanya utajiri wa mataifa yote yanayowazunguka - dhahabu, fedha, na wingi wa nguo safi.
And also Judah it will fight at Jerusalem and it will be gathered [the] wealth of all the nations all around gold and silver and garments to abundance very great.
15 Tauni itakuwa pia juu ya farasi na nyumbu, ngamia na punda, na kila mnyama katika kambi hizo atapigwa kwa hilo pigo.
And thus it will be [the] plague of the horse the mule the camel and the donkey and all the livestock which it will be in the camps those like the plague this.
16 Kisha itakuwa wote watakaosalia katika mataifa yaliyo kinyume na Yerusalemu watakwenda mwaka kwa mwaka kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, na kutunza Sikukuu ya Vibanda.
And it will be every [one who] remains of all the nations which came on Jerusalem and they will go up as often as a year in a year to bow down to [the] king Yahweh of hosts and to celebrate a festival [the] festival of Tabernacles.
17 Na itakuwa kwamba ikiwa mtu yeyote kutoka katika mataifa yote ya dunia haendi Yerusalemu kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, ndipo Yahwe hataleta mvua juu yao.
And it will be [one] who not he will go up from with [the] clans of the earth to Jerusalem to bow down to [the] king Yahweh of hosts and not on them it will be rain.
18 Na ikiwa nchi ya Misri hawatakwenda, ndipo hawatapata mvua. Tauni kutoka kwa Yahwe itayashambulia mataifa yote yasiyokwea kutunza Sikukuu ya Vibanda.
And if [the] clan of Egypt not it will go up and not [is] going and not on them it will be the plague which he will strike Yahweh the nations which not they will go up to celebrate a festival [the] festival of Tabernacles.
19 Hii itakuwa ni adhabu kwa Misri na adhabu kwa kila taifa lisilopanda kutunza Sikukuu ya Vibanda.
This it will be [the] punishment for sin of Egypt and [the] punishment for sin of all the nations which not they will go up to celebrate a festival [the] festival of Tabernacles.
20 Lakini katika siku hiyo, kengele za farasi zitasema, “Jitengeni kwa ajili ya Yahwe,” na makalai katika nyumba ya Yahwe yatakuwa kama mabakuri mbele ya madhabahu.
On the day that it will be on [the] bells of the horse[s] holiness to Yahweh and it will be the pots in [the] house of Yahweh [will be] like the bowls before the altar.
21 Kwa kuwa kila chungu katika Yerusalemu na Yuda kitatengwa kwa ajili ya Yahwe wa majeshi na kila mmoja aletaye sadaka atakula ndani yake na kuyachemshia. Hakutakuwa na wafanyabiashara tena katika nyumba ya Yahwe wa majeshi siku hiyo.
And it will be every pot in Jerusalem and in Judah a holy thing to Yahweh of hosts and they will come all those [who] sacrifice and they will take some of them and they will boil in them and not [he] will be a Canaanite again in [the] house of Yahweh of hosts on the day that.

< Zekaria 14 >