< Zekaria 14 >
1 Tazama! Siku ya Yahwe inakuja wakati mateka wenu watakapogawanywa katikati yenu.
Behold, a day is coming unto the Lord, when thy spoil shall be divided in the midst of thee.
2 Kwa maana nitayakusanya mataifa yote kinyume cha Yerusalemu kwa vita na mji utatekwa. Nyumba zitatekwa na wanawake watabakwa. Nusu ya mji itapelekwa matekani, lakini kumbukumbu ya watu haitaondolewa mjini.
And I will assemble all the nations against Jerusalem to battle; and the city shall be captured, and the houses plundered, and the women ravished; and half of the city shall go forth into exile, and the residue of the people shall not be cut off from the city.
3 Lakini Yahwe ataondoka na kufanya vita dhidi ya mataifa kama apigavyo vita katika siku ya vita.
Then will the Lord go forth, and fight against these nations, as on the day when he fought on the day of battle.
4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, uliopo kando ya Yerusalemu upande wa mashariki. Mlima wa Mizeituni utagawanyika katikati kati ya mashariki na magharibi kwa bonde kubwa sana na nusu ya mlima itarudi nyuma kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
And his feet will stand on that day upon the mount of Olives, which is before Jerusalem on the east, and the mount of Olives shall be split in twain in its middle eastward and westward, making a very great valley; and half of the mount shall remove northward, and half of it southward.
5 Ndipo mtakapokimbia katika bonde kati ya milima ya Yahwe, kwa kuwa bonde kati ya hiyo milima litafika hata Azali. Mtakimbia kama siku mliyokimbia tetemeko la nchi siku za Uzia, mfalme wa Yuda. Ndipo Yahwe Mungu wangu atakapokuja na watakatifu wake wote.
And ye shall flee [from] the valley of my mountains; for the valley of the mountains shall reach unto Azal; and ye shall flee, just as ye fled from before the earthquake in the days of 'Uzziyah the king of Judah: and then will come the Lord my God, and all the saints with thee.
6 Hakutakuwa na nuru katika siku hiyo, lakini hakuna baridi wala barafu.
And it shall come to pass on that day, that there shall be no light, but fleeting light and thick darkness;
7 Siku hiyo, siku aijuaye Yahwe peke yake, hakutakuwa tena na mchana wala usiku, kwani jioni itakuwa wakati wa nuru.
But it shall be one particular day which shall indeed be known as the Lord's, neither day nor night; but it shall come to pass, that at evening-time there shall be light.
8 Siku hiyo maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu. Nusu yake yatatiririka kuelekea bahari ya mashariki na nusu bahari ya magharibi, wakati wa masika na wakati wa kiangazi.
And it shall happen on that day, that living waters shall go out from Jerusalem, the half of them toward the eastern sea, and the other half of them toward the western sea: in summer and in winter shall it be so.
9 Yahwe atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo kutakuwa na Yahwe, Mungu mmoja, na jina lake pekee.
And the Lord will be king over all the earth: on that day shall the Lord be [acknowledged] one, and his name be one.
10 Nchi yote itakuwa kama Araba, kuanzia Geba hadi Rimoni kusini mwa Yerusalemu. Na Yerusalemu itaendelea kuwa juu. Ataishi mahali pake mwenyewe, kutoka lango la Benjamini hata mahali lilipokuwa lango la kwanza, hata Lango la Pembeni, na kutoka Mnara wa Hananeli hata shinikizo la mfalme.
All the land shall be changed as it were into a plain from Geba' to Rimmon to the south of Jerusalem; and she herself shall be elevated, and be inhabited on her former site, from the gate of Benjamin unto the place of the first gate, up to the corner gate, and from the tower of Chananel unto the king's wine-presses.
11 Watu watakaa Yerusalemu na hakutakuwa na maangamizi kamili tena kutoka kwa Mungu dhidi yao. Yerusalemu itakuwa salama.
And men shall dwell in it, and no destruction shall any more take place; but Jerusalem shall be inhabited in safety.
12 Hii itakuwa tauni ambayo kwayo Yahwe atawapiga jamaa zote za watu wapigao vita juu ya Yerusalemu: miili yao itaoza hata wakiwa wamesimama kwa miguu yao. Macho yao yataoza katika matundu yake na ndimi zao zitaoza katika vinywa vyao.
And this shall be the plague wherewith the Lord will afflict all the people that shall have come to battle against Jerusalem: The flesh of every one shall consume away while he standeth upon his feet, and his eyes shall consume away in their holes, and the tongue of every one shall consume away in his mouth.
13 Siku hiyo ile hofu kuu kutoka kwa Yahwe itakuwa miongoni mwao. Kila mmoja ataushika mkono wa mwingine, na mkono wa mwingine utainuliwa kinyume cha mkono wa mwenzake.
And it shall come to pass on that day, that a great confusion from the Lord shall be among them: and they shall lay hold every one on the hand of his neighbor, and his hand shall rise up against the hand of his neighbor.
14 Yuda pia atapigana na Yerusalemu. Watakusanya utajiri wa mataifa yote yanayowazunguka - dhahabu, fedha, na wingi wa nguo safi.
And also Judah will have to fight against Jerusalem: and there shall be gathered together the wealth of all the nations round about, gold, and silver, and garments, in great abundance.
15 Tauni itakuwa pia juu ya farasi na nyumbu, ngamia na punda, na kila mnyama katika kambi hizo atapigwa kwa hilo pigo.
And thus shall be the plague of the horses, of the mules, of the camels, and of the asses, and of all the beasts that will be in these camps, just like this plague.
16 Kisha itakuwa wote watakaosalia katika mataifa yaliyo kinyume na Yerusalemu watakwenda mwaka kwa mwaka kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, na kutunza Sikukuu ya Vibanda.
And it shall come to pass, that every one that is left out of all the nations who will have come against Jerusalem, yea, these shall go up year by year to bow down before the King, the Lord of hosts, and to celebrate the feast of tabernacles.
17 Na itakuwa kwamba ikiwa mtu yeyote kutoka katika mataifa yote ya dunia haendi Yerusalemu kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, ndipo Yahwe hataleta mvua juu yao.
And it shall happen, that whoso will not come up out of the families of the earth unto Jerusalem to bow down before the King, the Lord of hosts, —even upon these there shall be no rain.
18 Na ikiwa nchi ya Misri hawatakwenda, ndipo hawatapata mvua. Tauni kutoka kwa Yahwe itayashambulia mataifa yote yasiyokwea kutunza Sikukuu ya Vibanda.
And if the family of Egypt go not up, and come not, then shall not [any rain fall] upon them also: this shall be the plague, wherewith the Lord will afflict the nations that will not come up to celebrate the feast of tabernacles.
19 Hii itakuwa ni adhabu kwa Misri na adhabu kwa kila taifa lisilopanda kutunza Sikukuu ya Vibanda.
This shall be the punishment of Egypt, and the punishment of all the nations that will not come up to celebrate the feast of tabernacles.
20 Lakini katika siku hiyo, kengele za farasi zitasema, “Jitengeni kwa ajili ya Yahwe,” na makalai katika nyumba ya Yahwe yatakuwa kama mabakuri mbele ya madhabahu.
On that day shall [every thing], even to the bells of the horses, be holy unto the Lord; and the pots in the Lord's house shall be like the bowls before the altar.
21 Kwa kuwa kila chungu katika Yerusalemu na Yuda kitatengwa kwa ajili ya Yahwe wa majeshi na kila mmoja aletaye sadaka atakula ndani yake na kuyachemshia. Hakutakuwa na wafanyabiashara tena katika nyumba ya Yahwe wa majeshi siku hiyo.
And every pot in Jerusalem and in Judah shall be holy unto the Lord of hosts; and all those that sacrifice will come and take some of them, and seethe therein: and on that day there shall be no more any trader in the house of the Lord of host.