< Zekaria 14 >

1 Tazama! Siku ya Yahwe inakuja wakati mateka wenu watakapogawanywa katikati yenu.
Behold, the days of the Lord will arrive, and your spoils will be divided in your midst.
2 Kwa maana nitayakusanya mataifa yote kinyume cha Yerusalemu kwa vita na mji utatekwa. Nyumba zitatekwa na wanawake watabakwa. Nusu ya mji itapelekwa matekani, lakini kumbukumbu ya watu haitaondolewa mjini.
And I will gather all the Gentiles in battle against Jerusalem, and the city will be captured, and the houses will be ravaged, and the women will be violated. And the central part of the city will go forth into captivity, and the remainder of the people will not be taken away from the city.
3 Lakini Yahwe ataondoka na kufanya vita dhidi ya mataifa kama apigavyo vita katika siku ya vita.
Then the Lord will go forth, and he will fight against those Gentiles, just as when he fought in the day of conflict.
4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, uliopo kando ya Yerusalemu upande wa mashariki. Mlima wa Mizeituni utagawanyika katikati kati ya mashariki na magharibi kwa bonde kubwa sana na nusu ya mlima itarudi nyuma kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
And his feet will stand firm, in that day, upon the Mount of Olives, which is opposite Jerusalem towards the East. And the mount of Olives will be divided down its center part, towards the East and towards the West, with a very great rupture, and the center of the mountain will be separated towards the North, and its center towards the Meridian.
5 Ndipo mtakapokimbia katika bonde kati ya milima ya Yahwe, kwa kuwa bonde kati ya hiyo milima litafika hata Azali. Mtakimbia kama siku mliyokimbia tetemeko la nchi siku za Uzia, mfalme wa Yuda. Ndipo Yahwe Mungu wangu atakapokuja na watakatifu wake wote.
And you will flee to the valley of those mountains, because the valley of the mountains will be joined all the way to the next. And you will flee, just as you fled from the face of the earthquake in the days of Uzziah king of Judah. And the Lord my God will arrive, and all the saints with him.
6 Hakutakuwa na nuru katika siku hiyo, lakini hakuna baridi wala barafu.
And this shall be in that day: there will not be light, only cold and frost.
7 Siku hiyo, siku aijuaye Yahwe peke yake, hakutakuwa tena na mchana wala usiku, kwani jioni itakuwa wakati wa nuru.
And there will be one day, which is known to the Lord, not day and not night. And in the time of the evening, there will be light.
8 Siku hiyo maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu. Nusu yake yatatiririka kuelekea bahari ya mashariki na nusu bahari ya magharibi, wakati wa masika na wakati wa kiangazi.
And this shall be in that day: the living waters will go out from Jerusalem, half of them towards the East sea, and half of them towards the furthest sea. They will be in summer and in winter.
9 Yahwe atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo kutakuwa na Yahwe, Mungu mmoja, na jina lake pekee.
And the Lord will be King over all the earth. In that day, there will be one Lord, and his name will be one.
10 Nchi yote itakuwa kama Araba, kuanzia Geba hadi Rimoni kusini mwa Yerusalemu. Na Yerusalemu itaendelea kuwa juu. Ataishi mahali pake mwenyewe, kutoka lango la Benjamini hata mahali lilipokuwa lango la kwanza, hata Lango la Pembeni, na kutoka Mnara wa Hananeli hata shinikizo la mfalme.
And all the land will return even to the desert, from the hill of Rimmon to the South of Jerusalem. And she will be exalted, and she will dwell in her own place, from the gate of Benjamin even to the place of the former gate, and even to the gate of the corners, and from the tower of Hananel even to the pressing room of the king.
11 Watu watakaa Yerusalemu na hakutakuwa na maangamizi kamili tena kutoka kwa Mungu dhidi yao. Yerusalemu itakuwa salama.
And they will dwell in it, and there will be no further anathema, but Jerusalem shall sit securely.
12 Hii itakuwa tauni ambayo kwayo Yahwe atawapiga jamaa zote za watu wapigao vita juu ya Yerusalemu: miili yao itaoza hata wakiwa wamesimama kwa miguu yao. Macho yao yataoza katika matundu yake na ndimi zao zitaoza katika vinywa vyao.
And this will be the plague by which the Lord will strike all the Gentiles that have fought against Jerusalem. The flesh of each one will waste away while they are standing on their feet, and their eyes will be consumed in their sockets, and their tongue will be consumed in their mouth.
13 Siku hiyo ile hofu kuu kutoka kwa Yahwe itakuwa miongoni mwao. Kila mmoja ataushika mkono wa mwingine, na mkono wa mwingine utainuliwa kinyume cha mkono wa mwenzake.
In that day, there will be a great tumult from the Lord among them. And a man will take the hand of his neighbor, and his hand will be clasped upon the hand of his neighbor.
14 Yuda pia atapigana na Yerusalemu. Watakusanya utajiri wa mataifa yote yanayowazunguka - dhahabu, fedha, na wingi wa nguo safi.
And even Judah will fight against Jerusalem. And the riches of all the Gentiles will be gathered together around them: gold, and silver, and more than enough garments.
15 Tauni itakuwa pia juu ya farasi na nyumbu, ngamia na punda, na kila mnyama katika kambi hizo atapigwa kwa hilo pigo.
And, like the ruin of the horse, and the mule, and the camel, and the donkey, and all the beasts of burden, which will have been in those encampments, so will be this ruination.
16 Kisha itakuwa wote watakaosalia katika mataifa yaliyo kinyume na Yerusalemu watakwenda mwaka kwa mwaka kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, na kutunza Sikukuu ya Vibanda.
And all those who will be the remnant of all the Gentiles that came against Jerusalem, will go up, from year to year, to adore the King, the Lord of hosts, and to celebrate the feast of tabernacles.
17 Na itakuwa kwamba ikiwa mtu yeyote kutoka katika mataifa yote ya dunia haendi Yerusalemu kumwabudu mfalme, Yahwe wa majeshi, ndipo Yahwe hataleta mvua juu yao.
And this shall be: whoever will not go up, from the families of the earth to Jerusalem, so as to adore the King, the Lord of hosts, there will be no showers upon them.
18 Na ikiwa nchi ya Misri hawatakwenda, ndipo hawatapata mvua. Tauni kutoka kwa Yahwe itayashambulia mataifa yote yasiyokwea kutunza Sikukuu ya Vibanda.
But if even the family of Egypt will go not up, nor approach, neither will it be upon them, but there will be ruin, by which the Lord will strike all the Gentiles, who will not go up to celebrate the feast of tabernacles.
19 Hii itakuwa ni adhabu kwa Misri na adhabu kwa kila taifa lisilopanda kutunza Sikukuu ya Vibanda.
This will be the sin of Egypt, and this will be the sin of all the Gentiles, who will not go up to celebrate the feast of tabernacles.
20 Lakini katika siku hiyo, kengele za farasi zitasema, “Jitengeni kwa ajili ya Yahwe,” na makalai katika nyumba ya Yahwe yatakuwa kama mabakuri mbele ya madhabahu.
In that day, that which is on the bridle of the horse will be holy to the Lord. And even the cooking pots in the house of the Lord will be like holy vessels before the altar.
21 Kwa kuwa kila chungu katika Yerusalemu na Yuda kitatengwa kwa ajili ya Yahwe wa majeshi na kila mmoja aletaye sadaka atakula ndani yake na kuyachemshia. Hakutakuwa na wafanyabiashara tena katika nyumba ya Yahwe wa majeshi siku hiyo.
And every cooking pot in Jerusalem and Judah will be sanctified to the Lord of hosts. And all those who make sacrifices will come and take from them, and will cook with them. And the merchant will no longer be in the house of the Lord of hosts, in that day.

< Zekaria 14 >