< Zekaria 13 >

1 Katika siku hiyo kijito kitafunguliwa kwa ajili ya nyumba ya Daudi na wenyeji wa Yerusalemu, kwa ajili ya dhambi na uchafu wao.
En ce jour-là, il y aura une fontaine ouverte à la maison de David et aux habitants de Jérusalem, pour laver le pécheur et la femme qui est dans ses mois.
2 Katika siku hiyo - asema Yahwe wa majeshi - kwamba nitaondoa majina ya sanamu katika nchi ili kwamba yasikumbukwe tena. Nitawaondoa pia katika nchi manabii wa uongo na roho wao mchafu
Et il arrivera en ce jour-là, dit le Seigneur des armées, que je détruirai de la terre les noms des idoles, et qu’on n’en conservera plus la mémoire; et les faux prophètes et l’esprit immonde, je les enlèverai de là terre.
3 Ikiwa mtu yeyote ataendelea kutoa unabii, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, 'Hautaishi, kwa kuwa umenena uongo kwa jina la Yahwe! Ndipo baba na mama waliomzaa watakapomchoma wakati akitabiri.
Et il arrivera que si quelqu’un prophétise encore, son père et sa mère qui l’ont engendré, lui diront: Tu ne vivras pas, parce que tu as proféré le mensonge au nom du Seigneur; et son père et sa mère, les auteurs de ses jours, le perceront, parce qu’il aura prophétisé.
4 Katika siku hiyo kila nabii ataonea aibu maono yake aelekeapo kutoa unabii. Manabii hawa hawatavaa tena vazi la singa, ili kuwadanganya watu.
Et il arrivera en ce jour-là que les prophètes seront confondus, chacun par sa propre vision, lorsqu’il prophétisera; et ils ne se couvriront pas d’un sac, afin de mentir;
5 Kwa maana kila mmoja atasema, 'Mimi siyo nabii! mimi ni mkulima, kwa maana ardhi ndiyo kazi yangu tangu ujana wangu!
Mais chacun d’eux dira: Je ne suis point prophète; je suis un homme laboureur; car Adam est mon modèle depuis ma jeunesse.
6 Lakini mtu mwingine atamwambia, 'Majeraha haya kati ya mikono yako ni ya nini?' naye atajibu, nilijeruhiwa na waliokuwa katika nyumba ya rafiki zangu.”
Et on lui dira: Que sont ces plaies au milieu de tes mains? Et il dira: J’ai été percé de ces plaies que j’ai reçues dans la maison de ceux qui m’aimaient.
7 Upanga! inuka mwenyewe dhidi ya mchungaji wangu, mtu asimamaye karibu nami - hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi. Mpige mchungaji, na kondoo watatawanyika! Kwa maana nitageuza mkono wangu dhidi ya wadogo.
Ô épée à deux tranchants, réveille-toi; viens contre mon pasteur, contre l’homme qui se tient attaché à moi, dit le Seigneur des armées; frappe le pasteur, et les brebis seront dispersées; et je tournerai ma main vers les petits.
8 Kisha itakuwa kwamba katika nchi yote - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - kwamba theluthi mbili yake itaondolewa! Watu hao wataangamia; theluthi moja tu ndiyo itakayosalia.
Et il y aura dans toute la terre, dit le Seigneur, deux parties qui seront dispersées, et qui défaudront, et la troisième partie y sera laissée.
9 Nitaipitisha hiyo ya tatu motoni na kuwasafisha kama fedha isafishwavyo; nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo. Wataliitia jina langu nami nitawajibu na kusema, 'Hawa ni watu wangu!' nao watasema, Yahwe ndiye Mungu wangu!”
Et je ferai passer la troisième partie par le feu, et je la chaufferai fortement, comme on chauffe l’argent, et je l’éprouverai comme on éprouve l’or. Elle invoquera mon nom, et moi je l’exaucerai. Je lui dirai: Tu es mon peuple; et elle, elle dira: Le Seigneur est mon Dieu.

< Zekaria 13 >