< Zekaria 13 >
1 Katika siku hiyo kijito kitafunguliwa kwa ajili ya nyumba ya Daudi na wenyeji wa Yerusalemu, kwa ajili ya dhambi na uchafu wao.
On that day a fountain will be opened for the house of David, and for the inhabitants of Jerusalem, for sin and for uncleanness.
2 Katika siku hiyo - asema Yahwe wa majeshi - kwamba nitaondoa majina ya sanamu katika nchi ili kwamba yasikumbukwe tena. Nitawaondoa pia katika nchi manabii wa uongo na roho wao mchafu
And it will be on that day, says the Lord of hosts, I will cut off the names of the idols from the land and they will be remembered no more. And the prophets and the unclean spirit I will banish from the land.
3 Ikiwa mtu yeyote ataendelea kutoa unabii, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, 'Hautaishi, kwa kuwa umenena uongo kwa jina la Yahwe! Ndipo baba na mama waliomzaa watakapomchoma wakati akitabiri.
If any man prophesy any more, his father and his mother who bore him, will say to him, “You will not live, for you speak falsehood in the name of the Lord.” And his father and his mother who bore him will stab him through when he is seized by the prophetic frenzy.
4 Katika siku hiyo kila nabii ataonea aibu maono yake aelekeapo kutoa unabii. Manabii hawa hawatavaa tena vazi la singa, ili kuwadanganya watu.
And it will be in that day that the prophets will be ashamed, each of his vision, and will not wear the hairy mantle in order to deceive.
5 Kwa maana kila mmoja atasema, 'Mimi siyo nabii! mimi ni mkulima, kwa maana ardhi ndiyo kazi yangu tangu ujana wangu!
Each will say, “I am not a prophet, a tiller of the ground am I, for the ground is my possession from my youth.”
6 Lakini mtu mwingine atamwambia, 'Majeraha haya kati ya mikono yako ni ya nini?' naye atajibu, nilijeruhiwa na waliokuwa katika nyumba ya rafiki zangu.”
And they will say to him, “What are these scars on your back?” And he will say, “The scars which I received in the house of my friends.”
7 Upanga! inuka mwenyewe dhidi ya mchungaji wangu, mtu asimamaye karibu nami - hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi. Mpige mchungaji, na kondoo watatawanyika! Kwa maana nitageuza mkono wangu dhidi ya wadogo.
Awake, sword, against my shepherd, against the man who stands near to me, says the Lord of hosts. I will strike the shepherd so that the sheep may be scattered, I will turn my hand against the little ones.
8 Kisha itakuwa kwamba katika nchi yote - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - kwamba theluthi mbili yake itaondolewa! Watu hao wataangamia; theluthi moja tu ndiyo itakayosalia.
In all the land, says the Lord, two-thirds in it will be cut off and die, but a third will be left in it.
9 Nitaipitisha hiyo ya tatu motoni na kuwasafisha kama fedha isafishwavyo; nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo. Wataliitia jina langu nami nitawajibu na kusema, 'Hawa ni watu wangu!' nao watasema, Yahwe ndiye Mungu wangu!”
I will bring the third into the fire, and melt it as one melts silver, and test it as one tests gold. Then they will call on my name, and I myself will answer them. I will say, “They are my people.” They will say, “The Lord is our God.”