< Zekaria 12 >

1 Hili ni tamko la neno la Yahwe kwa Israeli - Bwana asema, azitandaye mbingu na kuweka msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mtu ndani yake,
Brzemię słowa Pańskiego nad Izraelem. Tak mówi Pan, który rozpostarł niebiosa, a ugruntował ziemię, który tworzy ducha człowieczego we wnętrznościach jego:
2 “Tazama, nitaifanya Yerusalemu kuwa kikombe kiwafadhaishacho watu wote wamzungukao. Itakuwa hivyo hivyo pia kwa Yuda wakati wa kuhusuriwa kwa Yerusalemu.
Oto Ja postawię Jeruzalem kubkiem opojenia wszystkim narodom okolicznym, którzy będą przeciwko Judzie na oblężenie, i przeciwko Jeruzalemowi.
3 Katika siku hiyo, nitaifanya Yerusalemu kuwa jiwe zito kwa watu wa jamaa zote. Kila atakayejaribu kuliinua jiwe hilo atajihumiza sana, na mataifa yote ya dunia yatakusanyika kinyume cha mji huo.
Owszem, stanie się dnia onego, że uczynię Jeruzalem kamieniem ciężkim wszystkim narodom; wszyscy, którzy go dźwigać będą, bardzo się urażą, choćby się zgromadziły przeciwko niemu wszystkie narody ziemi.
4 Katika siku hiyo asema Yahwe - nitampiga kila farasi kwa ushangao na kila mpanda farasi kwa wendawazimu. Nitaiangalia nyumba ya Yuda kwa upendeleo na nami nitawapiga kwa upofu farasi wa majeshi.
Dnia onego, mówi Pan, zarażę każdego konia zdrętwieniem i jeźdźca jego szaleństwem; ale nad domem Juda otworzę oczy moje, a każdego konia narodów zarażę ślepotą.
5 Ndipo watawala wa Yuda watakapojisemea mioyoni mwao, 'Wakaao Yerusalemu ndio nguvu yetu kwa sababu ya Yahwe wa majeshi, Mungu wao.'
I rzekną książęta Judzcy w sercu swem: Mamy siłę i obywatele Jeruzalemscy w Panu zastępów, Bogu swoim.
6 Katika siku hiyo nitawafanya watawala wa Yuda kuwa kama mitungi ya moto katika miti na kama miali ya moto kati ya nafaka isimamayo, kwani utateketeza watu wote walio karibu upande wao wa kulia na kushoto. Yerusalemu atakaa mahali pake tena.
Dnia onego położę książąt Judzkich jako węgle ogniste między drwy, a jako pochodnię gorejącą między snopy; i pożrą na prawą i na lewą stronę wszystkie narody okoliczne, i zostanie jeszcze Jeruzalem na miejscu swem w Jeruzalemie.
7 Yahwe ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili kwamba utukufu ya nyumba ya Daudi na utukufu wa wale waishio Yerusalemu hautazidi sehemu iliyosalia ya Yuda.
Zachowa Pan i namioty Judzkie pierwej, aby się nie wywyższała chwała domu Dawidowego, i chwała obywateli Jeruzalemskich przeciwko Judzie.
8 Katika siku hiyo Yahwe atakuwa mtetezi wa wakao Yerusalemu, na siku hiyo waliodhaifu miongoni mwao watakuwa kama Daudi, wakati nyumba ya Daudi watakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yahwe mbele yao.
Dnia onego Pan będzie bronił obywateli Jeruzalemskich, a któryby był między nimi najsłabszy, stanie się dnia onego podobny Dawidowi, a dom Dawidowy podobny bogom, podobny Aniołowi Pańskiemu przed nimi.
9 “Itakuwa kwamba katika siku hiyo nitaanza kuyaharibu mataifa yote yajayo kinyume cha Yerusalemu.
Bo się stanie dnia onego, że szukać będę wszystkie narody, które przyciągną przeciwko Jeruzalemowi, abym je wytracił.
10 Lakini nitamwaga roho ya huruma na kuiombea nyumba ya Daudi na wakao Yerusalemu, hivyo wataniangalia mimi, waliomchoma kwa mkuki. Wataniombolezea, kama amwombolezeaye mwana wa pekee; watamwombolezea kwa uchungu sana kama aombolezaye kifo cha mzaliwa wa kwanza.
I wyleję na dom Dawidowy, i na obywateli Jeruzalemskich Ducha łaski i modlitw, a patrzyć będą na mię, którego przebodli; i płakać będą nad nim płaczem, jako nad jednorodzonym; gorzko, mówię, płakać będą nad nim, jako gorzko płaczą nad pierworodnym.
11 Katika siku hiyo maombolezo huko Yerusalemu yatakuwa kama maombolezo ya Hadadi Rimoni katika tambarare za Megido.
Dnia onego będzie wielkie kwilenie w Jeruzalemie, jako kwilenie w Adadrymon na polu Magieddon;
12 Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi utakuwa peke yake na wake zao watakuwa peke yao mbali na wanaume. Ukoo wa nyumba ya Nathani utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
Bo ziemia kwilić będzie, każde pokolenie osobno, pokolenie domu Dawidowego osobno, i niewiasty ich osobno; pokolenie domu Natanowego osobno, i niewiasty ich osobno;
13 Ukoo wa nyumba ya Lawi utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume. Ukoo wa Washimei utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
Pokolenie domu Lewiego osobno, i niewiasty ich osobno; pokolenie Semejego osobno, i niewisty ich osobno;
14 Kila ukoo uliosalia - kila mmoja utakuwa peke yake na wake watakuwa pekee mbali na waume.
Wszystkie insze pokolenia, każde pokolenie osobno, i niewiasty ich osobno.

< Zekaria 12 >