< Zekaria 12 >

1 Hili ni tamko la neno la Yahwe kwa Israeli - Bwana asema, azitandaye mbingu na kuweka msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mtu ndani yake,
The prophecy of the word of Jehovah concerning Israel. Thus saith Jehovah, who stretched out the heavens, And laid the foundation of the earth, And formed the spirit of man within him:
2 “Tazama, nitaifanya Yerusalemu kuwa kikombe kiwafadhaishacho watu wote wamzungukao. Itakuwa hivyo hivyo pia kwa Yuda wakati wa kuhusuriwa kwa Yerusalemu.
Behold, I make Jerusalem a cup of giddiness to all the nations round about, And for Judah also shall it be In the siege against Jerusalem.
3 Katika siku hiyo, nitaifanya Yerusalemu kuwa jiwe zito kwa watu wa jamaa zote. Kila atakayejaribu kuliinua jiwe hilo atajihumiza sana, na mataifa yote ya dunia yatakusanyika kinyume cha mji huo.
And in that day will I make Jerusalem A burdensome stone for all nations; All that lift it up shall tear themselves, And all the nations of the earth shall gather themselves together against it.
4 Katika siku hiyo asema Yahwe - nitampiga kila farasi kwa ushangao na kila mpanda farasi kwa wendawazimu. Nitaiangalia nyumba ya Yuda kwa upendeleo na nami nitawapiga kwa upofu farasi wa majeshi.
In that day, saith Jehovah, I will smite every horse with amazement, And his rider with madness; I will open mine eyes upon the house of Judah, And every horse of the nations will I smite with blindness.
5 Ndipo watawala wa Yuda watakapojisemea mioyoni mwao, 'Wakaao Yerusalemu ndio nguvu yetu kwa sababu ya Yahwe wa majeshi, Mungu wao.'
Then shall the leaders of Judah say in their heart, “Strong are the inhabitants of Jerusalem, Through Jehovah of hosts, their God.”
6 Katika siku hiyo nitawafanya watawala wa Yuda kuwa kama mitungi ya moto katika miti na kama miali ya moto kati ya nafaka isimamayo, kwani utateketeza watu wote walio karibu upande wao wa kulia na kushoto. Yerusalemu atakaa mahali pake tena.
In that day will I make the leaders of Judah Like a fire-pan among wood, And like a torch of fire in a sheaf, And they shall devour, on the right hand and on the left, All the nations round about. And Jerusalem shall again dwell in her own place at Jerusalem.
7 Yahwe ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili kwamba utukufu ya nyumba ya Daudi na utukufu wa wale waishio Yerusalemu hautazidi sehemu iliyosalia ya Yuda.
Jehovah will also save the tents of Judah first, That the glory of the house of David, And the glory of the inhabitants of Jerusalem, May not magnify itself against Judah.
8 Katika siku hiyo Yahwe atakuwa mtetezi wa wakao Yerusalemu, na siku hiyo waliodhaifu miongoni mwao watakuwa kama Daudi, wakati nyumba ya Daudi watakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yahwe mbele yao.
In that day shall Jehovah defend the inhabitants of Jerusalem, And he that is feeble among them in that day shall be like David, And the house of David shall be as God, As the angel of Jehovah before them.
9 “Itakuwa kwamba katika siku hiyo nitaanza kuyaharibu mataifa yote yajayo kinyume cha Yerusalemu.
And it shall come to pass in that day That I will seek to destroy all the nations Which come against Jerusalem.
10 Lakini nitamwaga roho ya huruma na kuiombea nyumba ya Daudi na wakao Yerusalemu, hivyo wataniangalia mimi, waliomchoma kwa mkuki. Wataniombolezea, kama amwombolezeaye mwana wa pekee; watamwombolezea kwa uchungu sana kama aombolezaye kifo cha mzaliwa wa kwanza.
Then will I pour upon the house of David, And upon the inhabitants of Jerusalem, A spirit of supplication, and of prayer; And they shall look to me whom they pierced, And they shall mourn for him, as one mourneth for his only son, And shall be in bitterness for him, as one that is in bitterness for his first-born.
11 Katika siku hiyo maombolezo huko Yerusalemu yatakuwa kama maombolezo ya Hadadi Rimoni katika tambarare za Megido.
In that day the mourning shall be great in Jerusalem, As the mourning of Hadadrimmon in the valley of Megiddo.
12 Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi utakuwa peke yake na wake zao watakuwa peke yao mbali na wanaume. Ukoo wa nyumba ya Nathani utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
And the land shall mourn, every family apart; The family of the house of David apart, and their wives apart; The family of the house of Nathan apart, and their wives apart;
13 Ukoo wa nyumba ya Lawi utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume. Ukoo wa Washimei utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
The family of the house of Levi apart, and their wives apart; The family of the house of Shimei apart, and their wives apart;
14 Kila ukoo uliosalia - kila mmoja utakuwa peke yake na wake watakuwa pekee mbali na waume.
All the families that remain, Every family apart, and their wives apart.

< Zekaria 12 >