< Zekaria 10 >
1 Mwombeni Yahwe mvua nyakati za kipupwe - Yahwe afanyaye mvua ya radi - naye hufanya mvua inyeshe kwa kila mmoja na uoto kondeni.
Proście PANA o deszcz w późnej porze [deszczowej], a PAN stworzy chmury burzowe i da wam obfity deszcz i każdemu trawę na polu.
2 Kwani sanamu za wenye nyumba husema uongo; waganga hunena uongo; wanasema ndoto za udanganyifu na hutoa faraja tupu, hivyo wapotea kama kondoo na wanaumia kwa sababu hakuna mchungaji.
Bożki wypowiadają bowiem [słowa] próżności, a wróżbici prorokują kłamstwo i opowiadają zmyślone sny, daremnie pocieszają. Dlatego błąkali się jak trzoda, byli utrapieni, bo nie było pasterza.
3 Gadhabu yangu inawaka dhidi ya wachungaji; ni mabeberu - viongozi - nitakao waadhibu. Yahwe wa majeshi atalihudumia pia kundi la kondoo wake, nyumba ya Yuda, na kuwafanya kama farasi wake wa vita!
Mój gniew zapłonął przeciwko tym pasterzom i ukarałem te kozły, ale PAN zastępów nawiedzi swoją trzodę, dom Judy, i uczyni z niej wspaniałego konia do boju.
4 Kutoka kwao litatoka jiwe kuu la pembeni; kutoka kwao kitatoka kigingi cha hema; kutoka kwao utatoka upinde wa vita; kutoka kwao watakuja viongozi wote kwa pamoja.
Od niego wywodzi się kamień węgielny, od niego gwóźdź, od niego łuk wojenny, od niego także wszelki poborca.
5 Watakuwa kama mashujaa wawakanyagao adui zao katika matope ya mitaani vitani; watafanya vita, kwa maana Yahwe yu pamoja nao, nao watawaabisha wapanda farasi wa vita.
I będą jak mocarze, którzy wdeptują wroga w błoto uliczne podczas bitwy. I będą walczyć, bo PAN [jest] z nimi; a zawstydzą jeźdźców konnych.
6 Nitaitia nguvu nyumba ya Yuda na kuiokoa nyumba ya Yusufu; kwani nitawarejesha na kuwahurumia. Watakuwa kama nilikuwa sijawaondoa, kwani mimi ni Yahwe Mungu wao, nami nitawaitikia.
Umocnię dom Judy, wybawię dom Józefa i sprowadzę ich z powrotem w pokoju, bo zlituję się nad nimi. I będą [takimi], jak gdybym ich nie odrzucił. Ja bowiem jestem PAN, ich Bóg, i wysłucham ich.
7 Ndipo Efraimu atakapokuwa kama shujaa, na mioyo yao itafurahi kama kwa mvinyo; wana wao wataona na kufurahi. Mioyo yao itanifurahia!
Efraimici będą jak mocarz, ich serce rozweseli się jak od wina. Ich synowie to zobaczą i będą się cieszyć, a ich serce rozraduje się w PANU.
8 Nitawanong'oneza na kuwakusanya, kwani nitawaokoa, nao watakuwa wakuu kama walivyokuwa mwanzo!
Zaświstam na nich i zgromadzę ich, bo ich odkupiłem; i będą tak liczni, jak byli [dawniej].
9 Niliwapanda kati ya watu, lakini watanikumbuka katika nchi ya mbali, hivyo wao na wana wao wataishi na kurejea.
I rozsieję ich wśród narodów, aby w dalekich krajach przypomnieli sobie o mnie, a żyjąc tam ze swoimi dziećmi, nawrócą się.
10 Kwa maana nitawarejesha kutoka nchi ya Misri na kuwakusanya kutoka Ashuru. Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni mpaka kutakapokuwa hakuna nafasi tena kwa ajili yao.
Wyprowadzę ich znowu z ziemi Egiptu i zgromadzę ich z Asyrii, zaprowadzę do ziemi Gilead i do Libanu, ale nie starczy dla nich [miejsca].
11 Nitapita katika bahari ya mateso yao; nitayapiga mawimbi ya bahari hiyo na nitavikausha vilindi vyote vya Nile. Utukufu wa Ashuru utashushwa chini, na fimbo ya Misri itakwenda mbali kutoka kwa Wamisri.
Przejdzie przez morze ucisku, rozbije fale na morzu i wyschną wszystkie głębie rzeki. Wtedy pycha Asyrii będzie poniżona, a berło Egiptu zniknie.
12 Nitawatia nguvu katika mimi mwenyewe, nao watatembea katika jina langu - asema Yahwe.
Umocnię ich też w PANU i będą chodzić w jego imię, mówi PAN.