< Zekaria 1 >
1 Katika mwezi wa nane mwaka wa pili wa kutawala kwake Dario, neno la Yahwe lilimjia nabii Zekaria, mwana wa Berekia mwana wa Ido, kusema,
Au huitième mois, en la seconde année du roi Darius, la parole du Seigneur fut adressée à Zacharie, le prophète, fils de Barachie, fils d’Addo, disant:
2 “Yawhe alikuwa na hasira sana juu ya baba zenu!
Le courroux du Seigneur a été irrité contre vos pères.
3 Wambie, 'Yahwe wa majeshi asema hivi: Nirudieni! - nami nitawarudia ninyi, asema Yahwe wa majeshi.
Et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur des armées: Revenez à moi, dit le Seigneur des armées, et je reviendrai à vous, dit le Seigneur des armées.
4 Msiwe kama baba zenu ambao hapo zamani manabii waliwambia, wakisema, “Yahwe wa majeshi asema hivi: Geukeni kutoka katika njia zenu za mbaya na matendo yenu mabaya!” Lakini hawakuweza kusikia wala kunijari - asema Yahwe.'
Ne soyez pas comme vos pères auxquels les prophètes antérieurs criaient en disant: Voici ce que dit le Seigneur des armées: Revenez de vos voies mauvaises et de vos pensées très mauvaises; et ils ne m’ont pas écouté, et ils n’ont pas fait attention à moi, dit le Seigneur.
5 Wako wapi baba zenu? Na manabii, je wapo hapa daima?
Vos pères, où sont ils? et les prophètes, est-ce qu’ils vivront éternellement?
6 Lakini maneno yangu na maagizo niliyowaamru watumishi wangu manabii, je hayakuwapata baba zenu? Hivyo walitubu na kusema, 'Kama vile Yahwe wa majeshi alivyokusudia kututenda kwa kadili zinavyostahili njia na matendo yetu, ndivyo alivyotutenda.”
Mais cependant mes paroles et mes décrets, que j’ai confiés à mes serviteurs les prophètes, est-ce qu’ils n’ont pas atteint vos pères, et est-ce qu’ils se sont convertis, et ont dit: Comme le Seigneur des armées avait résolu de nous faire selon nos voies et selon nos inventions, ainsi il a fait?
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, ndiyo mwezi wa Shebati, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yahwe lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido, akasema,
Le vingt-quatrième jour du onzième mois appelé Sabath, en la deuxième année du roi Darius, la parole du Seigneur fut adressée à Zacharie, le prophète, fils de Barachie, fils d’Addo, disant:
8 “niliona wakati wa usiku, na tazama! mtu alikuwa amepanda farasi mwekundu, naye alikuwa kati ya miti ya mihadasi iliyoko bondeni; na nyuma yake kulikuwa na farasi mwekundu, farasi wa kijivu, na farasi mweupe.”
Je vis pendant la nuit; et voilà un homme monté sur un cheval roux, et il se tenait parmi les myrtes qui étaient dans un lieu profond; et après lui des chevaux roux, mouchetés et blancs.
9 Nikauliza, “Bwana, hivi ni vitu gani?” Malaika aliyesema nami akaniambia, “Nitakueleza vitu hivi ni nini.”
Et je dis: Qui sont ceux-ci, ô mon Seigneur? Et l’ange, qui parlait en moi, me répondit: Moi, je t’indiquerai ce que ceci signifie.
10 Kisha mtu aliyesimama kati ya miti ya mihadasi akajibu na kusema, “Hawa ndiyo Yahwe aliowatuma kuzunguka katika dunia yote.”
Et l’homme qui se tenait parmi les myrtes répondit, et dit: Ceux-ci sont ceux qu’a envoyés le Seigneur, afin qu’ils parcourent la terre.
11 Wakamjibu malaika wa Yahwe aliyekuwa amesimama kati ya miti ya mihadasi na kumwambia, “Tumekuwa tukizunguka duniani pote; tazama, dunia yote imekaa na kutulia.”
Et ils répondirent à l’ange du Seigneur, qui se tenait parmi les myrtes, et dirent: Nous avons parcouru la terre, et voilà que toute la terre est habitée, et est en repos.
12 Ndipo malaika wa Yahwe alipojibu na kusema, “Yahwe wa majeshi, hata lini usiuhurumie Yerusalemu na miji ya Yuda ambayo imeteswa na kudhurumiwa miaka hii sabini?”
Et l’ange du Seigneur reprit et dit: Seigneur des armées, jusqu’à quand n’aurez-vous point pitié de Jérusalem, et des villes de Juda contre lesquelles vous êtes irrité? C’est déjà la soixante et dixième année.
13 Yahwe akamjibu malaika aliyekuwa amesema nami, kwa maneno mazuri, maneno ya faraja.
Et le Seigneur répondit à l’ange qui parlait en moi de bonne paroles, des paroles de consolation.
14 Hivyo malaika aliyekuwa anaongea nami akaniambia, “Ita kwa sauti na useme 'Yahwe wa majeshi asema: Nina wivu kwa ajili ya Yerusalemu yaani Sayuni kwa uchungu mkubwa!
Et l’ange qui parlait en moi me dit: Crie en disant: Voici ce que dit le Seigneur des armées: Je brûle pour Jérusalem et pour Sion d’un très grand zèle.
15 Nami nina hasira juu ya mataifa yaliyo na utulivu. Kwa maana nilikasirika kidogo tu, lakini wao wakasababisha madhara mabaya.
Et je suis aussi enflammé d’une très grande colère contre les nations opulentes, parce que, quand moi je n’ai été qu’un peu irrité, elles, au contraire, ont aidé au châtiment.
16 Kwa hiyo Yahwe wa majeshi asema hivi: Nimeirudia Yerusalema kwa huruma. Hivyo nyumba yangu itajengwa ndani yake - asema Yahwe wa majeshi. Kipimo kitanyoshwa juu ya Yerusalemu!
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Je reviendrai à Jérusalem avec des sentiments de miséricorde; et ma maison y sera bâtie, dit le Seigneur des armées, et le niveau sera étendu sur Jérusalem.
17 Ita tena, ukisema, 'Yahwe wa majeshi asema hivi: Miji yangu kwa mara nyingine itajawa na uzuri, na Yahwe ataifariji tena Sayuni, na kuichagua Yerusalemu kwa mara nyingine tena.”
Crie encore, en disant: Voici ce que dit le Seigneur des armées: Mes cités regorgeront encore de biens; le Seigneur consolera encore Sion, et il choisira encore Jérusalem.
18 Kisha nikainua macho na kuona pembe nne!
Et j’ai levé mes yeux, et j’ai vu; et voilà quatre cornes.
19 Nikaongea na malaika aliyesema nami, “Hivi ni vitu gani? Akanijibu “hizi ni pembe zilisosababisha kutawanyika kwa Yuda, Israeli, na Yerusalemu.”
Et j’ai dit à l’ange qui parlait en moi: Qu’est ceci? et il me répondit: Ce sont les cornes qui ont jeté au vent Juda, Israël et Jérusalem.
20 Kisha Yahwe akanionesha mafundi stadi wanne.
Et le Seigneur me montra quatre ouvriers.
21 Nikasema, “Watu hawa wanakuja kufanya nini?” Akajibu na kusema, “Hizi ni pembe zililoitawanya Yuda na hakuna mtu angeweza kuinua kichwa chake. Lakini watu hawa wanakuja kuziondoa, kutupa chini pembe za mataifa yaliyoinua nguvu zao kinyume cha nchi ya Yuda na kuisambaza.”
Et je dis: Que viennent faire ceux-ci? Il répondit en disant: Voilà les cornes qui ont jeté au vent, homme par homme, tous les habitants de Juda, et aucun d’eux n’a levé sa tête; et ceux-ci sont venus les épouvanter, afin d’abattre les cornes des nations qui ont levé la corne contre la terre de Juda pour la disperser.