< Tito 1 >
1 Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo, kwa imani ya wateule wa Mungu na maarifa ya kweli iletayo utauwa.
Paul, a servant of God, and an apostle of Jesus Christ, according to the faith of God’s elect, and the acknowledgement of the truth, which is according to godliness;
2 Wapo katika tumaini la uzima wa milele ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele. (aiōnios )
in hope of eternal life, which God, who can not lie, promised be fore the times of the ages, (aiōnios )
3 Kwa wakati muafaka, alilifunua neno lake katika ujumbe alionipa mimi kuhubiri. Ilinipasa kufanya hivi kwa amri ya Mungu mwokozi wetu.
but he has in his own times manifested his word by preaching, which was committed to me according to the commandment of God our Savior;
4 Kwa Tito, mwana wa kweli katika imani yetu. Neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba na Yesu Kristo mwokozi wetu.
to Titus, my true son, according to the common faith: grace, mercy, and peace from God the Father, and the Lord Jesus Christ our Savior.
5 Kwa sababu hii nalikuacha Krete, kwamba uyatengeneze mambo yote yaliyokuwa hayajakamilika na kuweka wazee wa kanisa kwa kila mji kama nilivyokuagiza.
I left you in Crete for this purpose, that you might set in order the things that are wanting, and ordain elders in every city, as I commanded you:
6 Mzee wa kanisa lazima asiwe na lawama, mme wa mke mmoja, aliye na watoto waaminifu wasioshuhudiwa mabaya au wasio na nidhamu.
if any one is blameless, the husband of one wife, if he has faithful children that are not accused of riotous living, or disobedient.
7 Ni muhimu kwa mwangalizi, kama msimamizi wa nyumba ya Mungu, asiwe na lawama. Asiwe mtu wa kelele au asiye jizuia. Lazima asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi, asiwe mtu wa kusababisha ugomvi, na asiwe mwenye tamaa.
For the bishop must be blameless, as the steward of God; not self-willed, not passionate, not fond of wine, not quarrelsome, not one who makes money by base means;
8 Badala yake: awe mtu mkaribishaji, apendaye wema. Lazima awe mtu mwenye akili timamu, mwenye haki, mcha Mungu, anayejitawala mwenyewe.
but hospitable, a lover of goodness, sober-minded, just, holy, temperate,
9 Awezaye kusimamia mafundisho ya kweli yaliyofundishwa, ili aweze kuwatia moyo kwa mafundisho mazuri na awezaye kuwarekebisha wote wanaompinga.
holding fast the sure word as it is taught, that he may be able, by sound teaching, both to exhort and to convince the opposers.
10 Kwa kuwa kuna waasi wengi, hasa wale wa tohara. Maneno yao ni ya upuuzi. Wanadanganya na kuwaongoza watu katika upotovu.
For there are many unruly and vain talkers and deceivers, especially those of the circumcision,
11 Ni lazima kuwazuia watu kama hao. Wanafundisha yale wasiyopaswa kwa faida za aibu na kuharibu familia zote.
whose mouths must be stopped: these subvert whole houses by teaching, for the sake of base gain, things which they ought not to teach.
12 Mmoja wao, mtu mwenye busara, alisema, “Wakrete wana uongo usio na mwisho, wabaya na wanyama wa hatari, wavivu na walafi.”
One of themselves, a prophet of their own, has said: The Cretans are always liars, evil wild beasts, lazy gluttons.
13 Haya maelezo ni ya kweli, kwa hiyo uwazuie kwa nguvu ili kwamba waweze kusema kweli katika imani.
This testimony is true; wherefore rebuke them severely, that they may be sound in the faith,
14 Wewe usijihusishe na hadithi zisizo za kweli za Kiyahudi au amri za watu, ambao hurudisha nyuma ukweli.
and not give heed to Jewish fables, and commandments of men that turn away from the truth.
15 Kwa wote walio safi, vitu vyote ni visafi. Lakini kwa wote walio wachafu na wasioamini, hakuna kilicho kisafi. Kwa kuwa mawazo yao na dhamira zao zimechafuliwa.
To the pure, all things are pure: but to the denied and unbelieving, nothing is pure; but their mind and their conscience are denied.
16 Wanakiri kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Wao ni waovu na wasiotii. Hawakuthibitishwa kwa tendo lolote jema.
They profess that they know God, but in their works they deny him, being detestable and disobedient, and, as it respects every good work, rejected.