< Tito 3 >
1 Uwakumbushe kuwanyenyekea viongozi na mamlaka, kuwatii na kuwa tayari katika kila kazi njema.
Rappelle aux fidèles le devoir d’être soumis aux magistrats et aux autorités, de leur obéir, d’être prêts à toute bonne œuvre,
2 Wakumbushe kutokumtendea mtu yeyote ubaya, waepuke majibizano, wawape nafasi watu wengine katika kufanya maamuzi, na kuonesha unyenyekevu kwa watu wote.
de ne dire du mal de personne, d’éviter les contestations, mais d’être condescendants, et de témoigner la plus grande douceur à l’égard de tous les hommes.
3 Kwa kuwa sisi pia tulikuwa na mawazo potofu na wakaidi. Tulikuwa upotevuni na tulifanywa watumwa kwa tamaa nyingi na starehe. Tuliishi katika wivu na uovu. Tulichukiza na kuchukiana.
Car nous aussi, nous étions autrefois insensés, indociles, égarés, esclaves de toutes sortes de convoitises et de jouissances, vivant dans la malignité et l’envie, dignes de haine, et nous haïssant les uns les autres.
4 Lakini wakati huruma ya Mungu mwokozi wetu na upendo wake kwa wanadamu ulipoonekana,
Mais lorsque Dieu notre Sauveur a fait paraître sa bonté et son amour pour les hommes,
5 haikuwa kwa matendo yetu ya haki tuliyofanya, bali alituokoa kwa neema yake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa upya na katika kufanywa upya kwa Roho Mtakatifu.
il nous a sauvés, non à cause des œuvres de justice que nous faisions, mais selon sa miséricorde, par le bain de la régénération et en nous renouvelant par le Saint-Esprit,
6 Mungu alimwaga Roho Mtakatifu kwa wingi juu yetu kupitia Yesu Kristo mwokozi wetu.
qu’il a répandu sur nous largement par Jésus-Christ notre Sauveur,
7 Alifanya hivi ili kwamba, tukiwa tumehesabiwa haki kwa neema yake, tuwe washirika katika uhakika wa maisha ya milele. (aiōnios )
afin que, justifiés par sa grâce, nous devenions héritiers de la vie éternelle selon notre espérance. (aiōnios )
8 Huu ni ujumbe wa kuaminika. Ninawataka myanene kwa ujasiri mambo haya, ili kwamba wale wanaomwamini Mungu wawe na dhamira juu ya kazi nzuri ambayo aliiweka mbele yao. Mambo haya ni mazuri na yanafaida kwa ajili ya watu wote.
C’est là une parole certaine, et je désire que tu affirmes ces choses, afin que ceux qui croient en Dieu s’appliquent à être les premiers dans la pratique des bonnes œuvres. C’est ce qui est bon et utile aux hommes.
9 Lakini jiepusheni na mijadala ya kipumbavu, nasaba, mashindano, na migongano kuhusu sheria. Mambo hayo hayana maana wala faida.
Quant aux questions folles, aux généalogies, aux querelles, aux disputes relatives à la Loi, évite-les, car elles sont inutiles et vaines.
10 Mkataeni yeyote anayesababisha migawanyiko kati yenu. Baada ya onyo moja ama mawili,
Pour celui qui fomente des divisions, après un premier et un second avertissement, éloigne-le de toi,
11 jueni kwamba mtu wa jinsi hiyo ameiacha njia iliyo sahihi na anatenda dhambi na kujihukumu mwenyewe.
sachant qu’un tel homme est entièrement perverti, et qu’il est un pécheur condamné de son propre jugement.
12 Nitakapomtuma kwako Artemi au Tikiko, harakisha uje kwangu huku Nikopoli ambapo nimeamua kukaa kipindi cha baridi.
Lorsque je t’aurai envoyé Artémas ou Tychique, hâte-toi de venir me rejoindre à Nicopolis, car j’ai résolu d’y passer l’hiver.
13 Harakisha na umtume Zena mtaalamu katika sheria, na Apolo, pasipo kupungukiwa na kitu.
Pourvois avec soin au voyage de Zénas, le docteur de la loi, et d’Apollos, en sorte que rien ne leur manque.
14 Watu wetu lazima wajifunze kujishughulisha katika kazi nzuri ambazo zinagusa mahitaji muhimu ili kwamba wasije wakawa wasiozaa matunda.
De plus que les nôtres aussi apprennent à se porter aux bonnes œuvres, de manière à subvenir aux besoins urgents, afin qu’ils ne soient pas sans fruits.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale watupendao katika imani. Neema iwe nanyi nyote.
Tous ceux qui sont avec moi te saluent; salue ceux qui nous aiment dans la foi. Que la grâce soit avec vous tous. Amen!