< Tito 3 >

1 Uwakumbushe kuwanyenyekea viongozi na mamlaka, kuwatii na kuwa tayari katika kila kazi njema.
Remind people that they must submit to the rulers who are in authority over them; that they must obey the magistrates, be prepared for every right action,
2 Wakumbushe kutokumtendea mtu yeyote ubaya, waepuke majibizano, wawape nafasi watu wengine katika kufanya maamuzi, na kuonesha unyenyekevu kwa watu wote.
not speak evil of any one, nor be contentious, but yield unselfishly to others and constantly manifest a forgiving spirit towards all men.
3 Kwa kuwa sisi pia tulikuwa na mawazo potofu na wakaidi. Tulikuwa upotevuni na tulifanywa watumwa kwa tamaa nyingi na starehe. Tuliishi katika wivu na uovu. Tulichukiza na kuchukiana.
For there was a time when we also were deficient in understanding, obstinate, deluded, the slaves of various cravings and pleasures, spending our lives in malice and envy, hateful ourselves and hating one another.
4 Lakini wakati huruma ya Mungu mwokozi wetu na upendo wake kwa wanadamu ulipoonekana,
But when the goodness of God our Saviour, and His love to man, dawned upon us, not in consequence of things which we,
5 haikuwa kwa matendo yetu ya haki tuliyofanya, bali alituokoa kwa neema yake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa upya na katika kufanywa upya kwa Roho Mtakatifu.
as righteous men, had done, but as the result of His own mercy He saved us by means of the bath of regeneration and the renewal of our natures by the Holy Spirit,
6 Mungu alimwaga Roho Mtakatifu kwa wingi juu yetu kupitia Yesu Kristo mwokozi wetu.
which He poured out on us richly through Jesus Christ our Saviour;
7 Alifanya hivi ili kwamba, tukiwa tumehesabiwa haki kwa neema yake, tuwe washirika katika uhakika wa maisha ya milele. (aiōnios g166)
in order that having been declared righteous through His grace we might become heirs to the Life of the Ages in fulfilment of our hopes. (aiōnios g166)
8 Huu ni ujumbe wa kuaminika. Ninawataka myanene kwa ujasiri mambo haya, ili kwamba wale wanaomwamini Mungu wawe na dhamira juu ya kazi nzuri ambayo aliiweka mbele yao. Mambo haya ni mazuri na yanafaida kwa ajili ya watu wote.
This is a faithful saying, and on these various points I would have you insist strenuously, in order that those who have their faith fixed on God may be careful to set an example of good actions. For these are not only good in themselves, but are also useful to mankind.
9 Lakini jiepusheni na mijadala ya kipumbavu, nasaba, mashindano, na migongano kuhusu sheria. Mambo hayo hayana maana wala faida.
But hold yourself aloof from foolish controversies and pedigrees and discussions and wrangling about the Law, for they are useless and vain.
10 Mkataeni yeyote anayesababisha migawanyiko kati yenu. Baada ya onyo moja ama mawili,
After a first and second admonition, have nothing further to do with any one who will not be taught;
11 jueni kwamba mtu wa jinsi hiyo ameiacha njia iliyo sahihi na anatenda dhambi na kujihukumu mwenyewe.
for, as you know, a man of that description has turned aside from the right path and is a sinner self-condemned.
12 Nitakapomtuma kwako Artemi au Tikiko, harakisha uje kwangu huku Nikopoli ambapo nimeamua kukaa kipindi cha baridi.
After I have sent Artemas or Tychicus to you, lose no time in joining me at Nicopolis; for I have decided to pass the winter there.
13 Harakisha na umtume Zena mtaalamu katika sheria, na Apolo, pasipo kupungukiwa na kitu.
Help Zenas the lawyer forward on his journey with special care, and Apollos, so that they may have all they require.
14 Watu wetu lazima wajifunze kujishughulisha katika kazi nzuri ambazo zinagusa mahitaji muhimu ili kwamba wasije wakawa wasiozaa matunda.
And let our people too learn to set a good example in following honest occupations for the supply of their necessities, so that they may not live useless lives.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale watupendao katika imani. Neema iwe nanyi nyote.
Every one here sends you greeting. Greet the believers who hold us dear. May grace be with you all.

< Tito 3 >