< Tito 3 >

1 Uwakumbushe kuwanyenyekea viongozi na mamlaka, kuwatii na kuwa tayari katika kila kazi njema.
Remind the people to be subject to rulers and authorities, to be obedient, to be ready for every good work,
2 Wakumbushe kutokumtendea mtu yeyote ubaya, waepuke majibizano, wawape nafasi watu wengine katika kufanya maamuzi, na kuonesha unyenyekevu kwa watu wote.
to slander no one, and to be peaceable and considerate, always showing gentleness toward everyone.
3 Kwa kuwa sisi pia tulikuwa na mawazo potofu na wakaidi. Tulikuwa upotevuni na tulifanywa watumwa kwa tamaa nyingi na starehe. Tuliishi katika wivu na uovu. Tulichukiza na kuchukiana.
For we ourselves were once foolish, disobedient, led astray, and enslaved to various lusts and pleasures. Living in wickedness and envy, we were loathsome and hated one another.
4 Lakini wakati huruma ya Mungu mwokozi wetu na upendo wake kwa wanadamu ulipoonekana,
But when the kindness of God our Savior and his love for mankind appeared,
5 haikuwa kwa matendo yetu ya haki tuliyofanya, bali alituokoa kwa neema yake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa upya na katika kufanywa upya kwa Roho Mtakatifu.
he saved us, not because of any righteous works we had done, but according to his mercy, through the washing of regeneration and the renewal of the Holy Spirit.
6 Mungu alimwaga Roho Mtakatifu kwa wingi juu yetu kupitia Yesu Kristo mwokozi wetu.
He richly poured out his Spirit upon us through Jesus Christ our Savior,
7 Alifanya hivi ili kwamba, tukiwa tumehesabiwa haki kwa neema yake, tuwe washirika katika uhakika wa maisha ya milele. (aiōnios g166)
so that, having been justified by his grace, we might become heirs according to the hope of eternal life. (aiōnios g166)
8 Huu ni ujumbe wa kuaminika. Ninawataka myanene kwa ujasiri mambo haya, ili kwamba wale wanaomwamini Mungu wawe na dhamira juu ya kazi nzuri ambayo aliiweka mbele yao. Mambo haya ni mazuri na yanafaida kwa ajili ya watu wote.
This saying is trustworthy. I want yoʋ to insist on these things, so that those who have put their trust in God may be careful to devote themselves to good works. These things are good and beneficial for people.
9 Lakini jiepusheni na mijadala ya kipumbavu, nasaba, mashindano, na migongano kuhusu sheria. Mambo hayo hayana maana wala faida.
But avoid foolish controversies, genealogies, quarrels, and disputes about the law, for they are unprofitable and futile.
10 Mkataeni yeyote anayesababisha migawanyiko kati yenu. Baada ya onyo moja ama mawili,
Reject a divisive person after a first and second warning.
11 jueni kwamba mtu wa jinsi hiyo ameiacha njia iliyo sahihi na anatenda dhambi na kujihukumu mwenyewe.
For yoʋ know that such a person is corrupted and sinful; he is self-condemned.
12 Nitakapomtuma kwako Artemi au Tikiko, harakisha uje kwangu huku Nikopoli ambapo nimeamua kukaa kipindi cha baridi.
When I send Artemas to yoʋ, or Tychicus, make every effort to come to me at Nicopolis, for I have decided to spend the winter there.
13 Harakisha na umtume Zena mtaalamu katika sheria, na Apolo, pasipo kupungukiwa na kitu.
Do everything yoʋ can to help Zenas the lawyer and Apollos on their way, and make sure they lack nothing.
14 Watu wetu lazima wajifunze kujishughulisha katika kazi nzuri ambazo zinagusa mahitaji muhimu ili kwamba wasije wakawa wasiozaa matunda.
Our people must learn to devote themselves to good works in order to meet pressing needs, so that they will not be unfruitful.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale watupendao katika imani. Neema iwe nanyi nyote.
All who are with me greet yoʋ. Greet those who love us in the faith. Grace be with you all. Amen.

< Tito 3 >