< Tito 2 >

1 Lakini wewe yaseme yale yanayoendana na maelekezo ya kuaminika.
But do you, on your part, speak what becomes sound teaching;
2 Wazee wawe na kiasi, heshima, busara, imani safi, katika upendo, na katika uvumilivu.
that the older men be self-controlled, serious and sober-minded, sound in faith, in love, in patience;
3 Vilevile wanawake wazee lazima daima wajioneshe wao wenyewe kama wenye kujiheshimu, na sio wasengenyaji. Lazima wasiwe watumwa wa pombe.
that older women likewise be reverent in demeanor, not slanderers or slaves to much wine, but teachers of what is right.
4 Wanapaswa kufundisha yaliyo mazuri ili kuwaandaa wasichana kwa busara kuwapenda waume zao na watoto wao.
They should train the younger women to love their husbands and children,
5 Wanapaswa kuwafundisha kuwa na busara, wasafi, watunzaji wazuri wa nyumba zao, na watii kwa waume zao wenyewe. Inawalazimu kufanya mambo haya ili kwamba neno la Mungu lisitukanwe.
to be sober-minded, chaste, workers at home, kind and submissive to their husbands, in order that God’s message be not maligned.
6 katika namna iyo hiyo, watieni moyo vijana wa kiume wawe na busara.
The younger men exhort to be sober-minded; in every respect showing yourself an example of good works.
7 Katika njia zote jiwekeni wenyewe kuwa mfano katika kazi nzuri; na mfundishapo, onesheni uadilifu na heshima.
In your teaching be serious and sincere.
8 Ongeeni ujumbe wenye afya na usio na dosari, ili kwamba yeyote apingaye aaibishwe kwa sababu hana baya la kusema juu yetu.
Let the instruction that you give be sound and above reproach, so that our opponents may be ashamed because they find no evil things to say about us.
9 Watumwa na wawatii mabwana zao katika kila kitu. Wanapaswa kuwafurahisha na sio kubishana nao.
Exhort slaves to be obedient to their own masters, and to be well- pleasing to them in every respect;
10 Hawapaswi kuiba. Badala yake, wanapaswa kuonesha imani yote nzuri ili kwamba katika njia zote wayapambe mafundisho yetu kumhusu Mungu mwokozi wetu.
not to contradict nor pilfer, but to exhibit praiseworthy trustworthiness in every thing, that they may adorn the doctrine of God our Saviour in all things.
11 Kwa kuwa neema ya Mungu imeonekana kwa watu wote.
"For God’s grace has shined forth bringing salvation to all men
12 Inatufundisha kukataa mambo yasiyo ya kimungu na tamaa za kidunia. Inatufundisha kuishi kwa busara, kwa haki, na katika njia za kimungu kwa wakati huu. (aiōn g165)
And schooling us to renounce impiety and evil passions, And to live soberly, righteously, and godly in this present age; (aiōn g165)
13 Wakati tunatarajia kupokea tumaini letu lenye baraka, mwonekano wa utukufu wa Mungu wetu mkuu na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
While we look for the blessed hope and epiphany of the glory of our great God and Saviour, Jesus Christ.
14 Yesu alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu ili kutukomboa kutoka katika uasi na kutufanya wasafi, kwa ajili yake, watu maalumu walio na hamu ya kufanya kazi nzuri.
He gave himself for us to redeem us from all iniquity, and to purify unto himself a people zealous of good works."
15 Yaseme na kuyasisitiza mambo haya. Kemea kwa mamlaka yote. Usikubali mtu yeyote akupuuze.
Thus speak, exhort, reprove with all authority. Let no one despise you.

< Tito 2 >