< Wimbo wa Sulemani 5 >

1 Nimekuja katika bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; Nimekusanya udi wangu na manukato yangu. Nimekula mziga wangu wa asali na asali yangu; Nimekunywa mvinyo wangu pamoja na maziwa yangu. Marafiki wanazungumza na wapenzi Kuleni, marafiki; kunyweni na mlewe na mapenzi. Mwanamke mdogo akizungumza mwenyewe
I have come into my garden, my sister, my bride; I have gathered my myrrh with my spice. I have eaten my honeycomb with my honey; I have drunk my wine with my milk. The friends speaking to the man and the woman Eat, friends; drink and be drunk with love.
2 Nilikuwa nimelala, lakini moyo wangu ulikuwa umeamka katika ndoto. Sauti ya mpenzi wangu yabisha na kusema, “Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu, hua wangu, wangu usiye na doa, kwa kuwa kichwa changu kimelowa na matone, nywele zangu na unyevu wa usiku.”
I was asleep, but my heart was awake. There is the sound of my beloved knocking and saying, “Open to me, my sister, my love, my dove, my undefiled one, for my head is wet with dew, my hair with the night's dampness.”
3 “Nimevua joho langu; lazima nilivae tena? Nimeosha miguu yangu; lazima ni ichafue?”
“I have taken off my robe; must I put it on again? I have washed my feet; must I get them dirty?”
4 Mpenzi wangu anaeka mkono wake kwenye kitasa, na moyo wangu ukawaka kwa ajili yake.
My beloved put in his hand through the opening of the door latch, and my heart was stirred up for him.
5 Nimeamka kumfungulia mlango mpenzi wangu; mikono yangu ikawa yamiminika na udi, vidole vyangu na unyevu wa udi, katika komeo la mlango.
I got up to open the door for my beloved; my hands were dripping with myrrh, my fingers with moist myrrh, on the door handle.
6 Nimemfungulia mlango mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu aligeuka na kwenda. Moyo wangu ukadidimia; nikakosa tumaini. Nikamtafuta, lakini sikumpata; nikamuita, lakini hakunijibu.
I opened the door for my beloved, but my beloved had turned and gone. My heart sank when he spoke. I looked for him, but I did not find him; I called him, but he did not answer me.
7 Walinzi waliokuwa wakizunguka mjini walinipata mimi; walinipiga chini na kunijeruhi; askari katika ukuta walichukua nguo yangu ya juu. Mwanamke mdogo akizungumza na wanawake wa mji
The watchmen found me as they were making their rounds in the city. They struck me and wounded me; the guards on the walls took away my cloak from me.
8 Ninataka uhaidi, mabinti wa Yerusalemu, kwamba mkimuona mpenzi wangu, mwambie ninaumwa sababu ya upendo wangu kwake. Wanawake wa mji wakizungumza na mwanamke mdogo
I want you to swear, daughters of Jerusalem, that if you find my beloved— What will you make known to him?— that I am sick from love.
9 Mpenzi wako ana ubora gani kuliko mwanaume mwengine, wewe uliye mzuri miongoni mwa wanawake? Kwanini mpenzi wako bora kuliko mpenzi mwengine, hadi utuulize tuweke nadhiri kama hii? Mwanamke mdogo akizungumza na wanawake wa mji
How is your beloved better than another beloved man, most beautiful among women? Why is your beloved better than another beloved, that you ask us to take an oath like this?
10 Mpenzi wangu amenawiri na ana ng'aa, kati ya wanaume elfu kumi.
My beloved is radiant and ruddy, outstanding among ten thousand.
11 Kichwa chake ni dhahabu safi; nywele zake ni laini na nyeusi kama kunguru.
His head is the purest gold; his hair is curly and as black as a raven.
12 Macho yake ni kama ya hua pembezoni ya vijito vya maji, yameoshwa na maziwa, yameundwa kama mikufu.
His eyes are like doves beside streams of water, bathed in milk, mounted like jewels.
13 Mashavu yake ni kama vitanda vya manukato, vinavyotoa arufu ya marashi. Midomo yake nni nyinyoro, inayo tiririka udi.
His cheeks are like beds of spices, yielding aromatic scents. His lips are lilies, dripping liquid myrrh.
14 Mikono yake ni ya mianzi ya dhahabu iliyo zungushiwa mikufu; tumbo lake ni pembe lililo funikwa yakuti samawi.
His arms are rounded gold set with jewels; his abdomen is ivory covered with sapphires.
15 Miguu yake ni nguzo za marimari, iliyo ekwa juu ya dhahabu safi; muonekano wake ni kama Lebanoni, mizuri kama mierezi.
His legs are pillars of marble, set on bases of pure gold; his appearance is like Lebanon, choice as the cedars.
16 Mdomo wake ni mtamu; ni mzuri sana. Huyu ni mpenzi wangu, na huyu ni rafiki yangu, mabinti wa Yerusalemu.
His mouth is most sweet; he is completely lovely. This is my beloved, and this is my friend, daughters of Jerusalem.

< Wimbo wa Sulemani 5 >