< Wimbo wa Sulemani 5 >

1 Nimekuja katika bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; Nimekusanya udi wangu na manukato yangu. Nimekula mziga wangu wa asali na asali yangu; Nimekunywa mvinyo wangu pamoja na maziwa yangu. Marafiki wanazungumza na wapenzi Kuleni, marafiki; kunyweni na mlewe na mapenzi. Mwanamke mdogo akizungumza mwenyewe
Bride: May my beloved enter into his garden, and eat the fruit of his apple trees. Groom to Bride: I have arrived in my garden, O my sister, my spouse. I have harvested my myrrh, with my aromatic oils. I have eaten the honeycomb with my honey. I have drunk my wine with my milk. Eat, O friends, and drink, and be inebriated, O most beloved.
2 Nilikuwa nimelala, lakini moyo wangu ulikuwa umeamka katika ndoto. Sauti ya mpenzi wangu yabisha na kusema, “Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu, hua wangu, wangu usiye na doa, kwa kuwa kichwa changu kimelowa na matone, nywele zangu na unyevu wa usiku.”
Bride: I sleep, yet my heart watches. The voice of my beloved knocking: Groom to Bride: Open to me, my sister, my love, my dove, my immaculate one. For my head is full of dew, and the locks of my hair are full of the drops of the night.
3 “Nimevua joho langu; lazima nilivae tena? Nimeosha miguu yangu; lazima ni ichafue?”
Bride: I have taken off my tunic; how shall I be clothed in it? I have washed my feet; how shall I spoil them?
4 Mpenzi wangu anaeka mkono wake kwenye kitasa, na moyo wangu ukawaka kwa ajili yake.
My beloved put his hand through the window, and my inner self was moved by his touch.
5 Nimeamka kumfungulia mlango mpenzi wangu; mikono yangu ikawa yamiminika na udi, vidole vyangu na unyevu wa udi, katika komeo la mlango.
I rose up in order to open to my beloved. My hands dripped with myrrh, and my fingers were full of the finest myrrh.
6 Nimemfungulia mlango mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu aligeuka na kwenda. Moyo wangu ukadidimia; nikakosa tumaini. Nikamtafuta, lakini sikumpata; nikamuita, lakini hakunijibu.
I opened the bolt of my door to my beloved. But he had turned aside and had gone away. My soul melted when he spoke. I sought him, and did not find him. I called, and he did not answer me.
7 Walinzi waliokuwa wakizunguka mjini walinipata mimi; walinipiga chini na kunijeruhi; askari katika ukuta walichukua nguo yangu ya juu. Mwanamke mdogo akizungumza na wanawake wa mji
The keepers who circulate through the city found me. They struck me, and wounded me. The keepers of the walls took my veil away from me.
8 Ninataka uhaidi, mabinti wa Yerusalemu, kwamba mkimuona mpenzi wangu, mwambie ninaumwa sababu ya upendo wangu kwake. Wanawake wa mji wakizungumza na mwanamke mdogo
I bind you by oath, O daughters of Jerusalem, if you find my beloved, announce to him that I languish through love.
9 Mpenzi wako ana ubora gani kuliko mwanaume mwengine, wewe uliye mzuri miongoni mwa wanawake? Kwanini mpenzi wako bora kuliko mpenzi mwengine, hadi utuulize tuweke nadhiri kama hii? Mwanamke mdogo akizungumza na wanawake wa mji
Chorus to Bride: What kind of beloved is your beloved, O most beautiful among women? What kind of beloved is your beloved, so that you would bind us by oath?
10 Mpenzi wangu amenawiri na ana ng'aa, kati ya wanaume elfu kumi.
Bride: My beloved is white and ruddy, elect among thousands.
11 Kichwa chake ni dhahabu safi; nywele zake ni laini na nyeusi kama kunguru.
His head is like the finest gold. His locks are like the heights of palm trees, and as black as a raven.
12 Macho yake ni kama ya hua pembezoni ya vijito vya maji, yameoshwa na maziwa, yameundwa kama mikufu.
His eyes are like doves, which have been washed with milk over rivulets of waters, and which reside near plentiful streams.
13 Mashavu yake ni kama vitanda vya manukato, vinavyotoa arufu ya marashi. Midomo yake nni nyinyoro, inayo tiririka udi.
His cheeks are like a courtyard of aromatic plants, sown by perfumers. His lips are like lilies, dripping with the best myrrh.
14 Mikono yake ni ya mianzi ya dhahabu iliyo zungushiwa mikufu; tumbo lake ni pembe lililo funikwa yakuti samawi.
His hands are smoothed gold, full of hyacinths. His abdomen is ivory, accented with sapphires.
15 Miguu yake ni nguzo za marimari, iliyo ekwa juu ya dhahabu safi; muonekano wake ni kama Lebanoni, mizuri kama mierezi.
His legs are columns of marble, which have been established over bases of gold. His appearance is like that of Lebanon, elect like the cedars.
16 Mdomo wake ni mtamu; ni mzuri sana. Huyu ni mpenzi wangu, na huyu ni rafiki yangu, mabinti wa Yerusalemu.
His throat is most sweet, and he is entirely desirable. Such is my beloved, and he is my friend, O daughters of Jerusalem.

< Wimbo wa Sulemani 5 >