< Wimbo wa Sulemani 2 >
1 Mimi ni ua katika tambarare, nyinyoro katika bonde. Mwanaume akizungumza naye
I am a rose of Sharon, A lily of the valleys.
2 Kama nyinyoro miongoni mwa mimba, ndivyo wewe, mpenzi wangu, miongoni mwa mabinti wengine wote. Mwanamke akizungumza mwenyewe
[[Lov.]] As the lily among thorns, So is my love among the daughters.
3 Kama mti wa mpera ulivyo miongoni mwa miti ya misituni, ndivyo mpenzi wangu alivyo miongoni mwa wanaume. Nina kaa chini ya kivuli chake kwa furaha sana, na tunda lake ni tamu kwa ladha yangu.
[[M.]] As the apple-tree among the trees of the forest, So is my beloved among the sons. In his shadow I love to sit down, And his fruit is sweet to my taste.
4 Amenileta kwenye ukumbi wa maakuli, na bendera yake juu yangu ilikuwa upendo. Mwanamke akizungumza na mpenzi wake.
He hath brought me to his banqueting-house, And his banner over me is love. Strengthen me with raisins,
5 Ni uishe kwa keki za mizabibu na kuniuisha na mapera, kwa kuwa nimedhohofika na mapenzi. Mwanamke akizungumza mwenyewe
Refresh me with apples! For I am sick with love.
6 Mkono wake wakushuto upo chini ya kichwa changu, na mkono wake wa kulia wanikumbatia. Mwanamke akizungumza na wanawake wengine.
His left hand is under my head, And his right hand embraceth me!
7 Ninataka muhaidi, mabinti wa Yerusalemu, kwa swala na paa wa porini, kwamba hamtavuruga mapenzi yetu hadi yatakapo isha yenyewe. Mwanamke akizungumza mwenyewe.
[[Lov.]] I charge you, O ye daughters of Jerusalem, By the gazelles, and by the hinds of the field, That ye stir not up, nor awake my love, till she please!
8 Sauti ya mpenzi wangu hiyo! O, huyu yuwaja, akiruka ruka juu milima, akiruka vilimani.
[[M.]] The voice of my beloved! Behold, he cometh, Leaping upon the mountains, Bounding upon the hills.
9 Mpenzi wangu ni kama swala au mtoto mdogo wa paa; angalia, amesimama nyuma ya ukuta wetu, akishangaa kupitia dirishani, akichungulia wavuni.
Like a gazelle is my beloved, Or a young hind. Behold, he standeth behind our wall; He is looking through the windows; He glanceth through the lattice.
10 Mpenzi wangu alizungumza na mimi na kusema, “Amka, mpenzi wangu; mzuri wangu, twende pamoja nami.
My beloved speaketh, and saith to me, “Rise up, my love, my fair one, and come away!
11 Angalia, baridi imepita; mvua imeisha na kwenda.
For, lo, the winter is past, The rain is over and gone;
12 Maua yametokeza juu ya nchi; wakati wa kupunguza matawi na kuimba kwa ndege umekuja, na sauti za hua zimesikika nchini kwetu.
The flowers appear on the earth; The time of the singing of birds is come, And the voice of the turtle is heard in our land;
13 Mti wa tini umepevusha tini zake za kijani, na mizabibu imestawi; yatoa marashi yake. Inuka, mpenzi wangu, mzuri wangu, na uje nami.
The fig-tree is spicing its green fruit; The vines in blossom give forth fragrance. Arise, my love, my fair one, and come away!
14 Hua wangu, katika miamba ya mawe, katika miamba ya siri ya mipasuko ya milima, acha nione uso wako. Acha nisikie sauti yako, kwa kuwa sauti ni tamu, na uso wako ni mzuri.” Mwanamke akiongea mwenyewe
O my dove, that art in the recesses of the rock, In the hiding-places of the steep craggy mountain, Let me see thy face, Let me hear thy voice! For sweet is thy voice, And thy face lovely.”
15 Wakamate mbweha kwa ajili yetu, mbweha wadogo wanao haribu shamba za mizabibu, kwa kuwa shamba la mizabibu limestawi.
Take ye for us the foxes, The little foxes that spoil the vines; For our vines are now in blossom.
16 Mpenzi wangu ni wangu, na mimi ni wake; anakula penye nyinyoro kwa raha. Mwanamke anaongea na mpenzi wake
My beloved is mine, and I am his; He feedeth among the lilies.
17 Enenda zako, mpenzi wangu, kabla pepo za jioni hazija vuma na vivuli kutoweka. Nenda zako; kuwa kama ayala au mtoto mdogo wa paa katika milima mawe mengi.
When the day breathes, and the shadows flee away, Come again, my beloved, like a gazelle, or a young hind, Upon the craggy mountains.