< Wimbo wa Sulemani 2 >

1 Mimi ni ua katika tambarare, nyinyoro katika bonde. Mwanaume akizungumza naye
As a lily among the thorns,
2 Kama nyinyoro miongoni mwa mimba, ndivyo wewe, mpenzi wangu, miongoni mwa mabinti wengine wote. Mwanamke akizungumza mwenyewe
So [is] my friend among the daughters!
3 Kama mti wa mpera ulivyo miongoni mwa miti ya misituni, ndivyo mpenzi wangu alivyo miongoni mwa wanaume. Nina kaa chini ya kivuli chake kwa furaha sana, na tunda lake ni tamu kwa ladha yangu.
As a citron among trees of the forest, So [is] my beloved among the sons, In his shade I delighted, and sat down, And his fruit [is] sweet to my palate.
4 Amenileta kwenye ukumbi wa maakuli, na bendera yake juu yangu ilikuwa upendo. Mwanamke akizungumza na mpenzi wake.
He has brought me to a house of wine, And his banner over me [is] love,
5 Ni uishe kwa keki za mizabibu na kuniuisha na mapera, kwa kuwa nimedhohofika na mapenzi. Mwanamke akizungumza mwenyewe
Sustain me with grape-cakes, Support me with citrons, for I [am] sick with love.
6 Mkono wake wakushuto upo chini ya kichwa changu, na mkono wake wa kulia wanikumbatia. Mwanamke akizungumza na wanawake wengine.
His left hand [is] under my head, And his right embraces me.
7 Ninataka muhaidi, mabinti wa Yerusalemu, kwa swala na paa wa porini, kwamba hamtavuruga mapenzi yetu hadi yatakapo isha yenyewe. Mwanamke akizungumza mwenyewe.
I have adjured you, daughters of Jerusalem, By the roes or by the does of the field, Do not stir up nor wake the love until she pleases!
8 Sauti ya mpenzi wangu hiyo! O, huyu yuwaja, akiruka ruka juu milima, akiruka vilimani.
The voice of my beloved! Behold, this—he is coming, Leaping on the mountains, skipping on the hills.
9 Mpenzi wangu ni kama swala au mtoto mdogo wa paa; angalia, amesimama nyuma ya ukuta wetu, akishangaa kupitia dirishani, akichungulia wavuni.
My beloved [is] like to a roe, Or to a young one of the harts. Behold, this—he is standing behind our wall, Looking from the windows, Blooming from the lattice.
10 Mpenzi wangu alizungumza na mimi na kusema, “Amka, mpenzi wangu; mzuri wangu, twende pamoja nami.
My beloved has answered and said to me, “Rise up, my friend, my beautiful one, and come away,
11 Angalia, baridi imepita; mvua imeisha na kwenda.
For behold, the winter has passed by, The rain has passed away—it has gone.
12 Maua yametokeza juu ya nchi; wakati wa kupunguza matawi na kuimba kwa ndege umekuja, na sauti za hua zimesikika nchini kwetu.
The flowers have appeared in the earth, The time of the singing has come, And the voice of the turtle was heard in our land,
13 Mti wa tini umepevusha tini zake za kijani, na mizabibu imestawi; yatoa marashi yake. Inuka, mpenzi wangu, mzuri wangu, na uje nami.
The fig tree has ripened her green figs, And the sweet-smelling vines have given forth fragrance, Rise, come, my friend, my beautiful one, indeed, come away.
14 Hua wangu, katika miamba ya mawe, katika miamba ya siri ya mipasuko ya milima, acha nione uso wako. Acha nisikie sauti yako, kwa kuwa sauti ni tamu, na uso wako ni mzuri.” Mwanamke akiongea mwenyewe
My dove, in clefts of the rock, In a secret place of the ascent, Cause me to see your appearance, Cause me to hear your voice, For your voice [is] sweet, and your appearance lovely.”
15 Wakamate mbweha kwa ajili yetu, mbweha wadogo wanao haribu shamba za mizabibu, kwa kuwa shamba la mizabibu limestawi.
Seize for us foxes, Little foxes—destroyers of vineyards, Even our sweet-smelling vineyards.
16 Mpenzi wangu ni wangu, na mimi ni wake; anakula penye nyinyoro kwa raha. Mwanamke anaongea na mpenzi wake
My beloved [is] mine, and I [am] his, Who is delighting among the lilies,
17 Enenda zako, mpenzi wangu, kabla pepo za jioni hazija vuma na vivuli kutoweka. Nenda zako; kuwa kama ayala au mtoto mdogo wa paa katika milima mawe mengi.
Until the day breaks forth, And the shadows have fled away, Turn, be like, my beloved, To a roe, or to a young one of the harts, On the mountains of separation!

< Wimbo wa Sulemani 2 >