< Ruth 4 >
1 Ndipo Boazi akaenda kwenye lango la Bethelehemu na kukaa chini. Muda mfupi tu akaja ndugu wa karibu ambaye Boazi alimuongelea. Boazi akamwambia, “Rafiki yangu, njoo hapa na uketi. Kisha mtu huyo akaja na kuketi.
Or Boaz monta à la porte et s'y assit. Et voici qu'arrive le proche parent dont Boaz avait parlé. Boaz lui dit: « Viens ici, mon ami, et assieds-toi. » Il s'approcha et s'assit.
2 Ndipo Boazi akakusanya viongozi kumi wa mji na kusema, “Katini hapa.” Hivyo wakaketi.
Boaz prit dix hommes parmi les anciens de la ville, et dit: « Assieds-toi ici. » Et ils s'assirent.
3 Boazi alimwambia yule jamaa wa karibu, “Naomi aliyerudi kutoka mji wa Moabu, anauza sehemu ya aridhi ambayo ilikuwa ni miliki ya kaka yetu Elimeleki.
Il dit au parent le plus proche: « Naomi, qui est revenue du pays de Moab, vend la parcelle de terre qui appartenait à notre frère Elimelech.
4 Nilifikiria kukujulisha na kukwambia, 'Inunue mbele ya hawa waliokaa hapa, na mbele ya viongozi wa watu wangu.' Ikiwa utapenda kuikomboa, ikomboe. Lakini ikiwa hauhitaji kuikomboa, uniambie, ili nijue, kwa kuwa hakuna mwingine wa kuikomboa isipokuwa wewe, na mimi ni mdogo wako.” Ndipo huyo mtu mwingine akasema, “Nitalikomboa.”
J'ai pensé que je devais te le dire, en disant: « Achète-le devant ceux qui sont assis ici, et devant les anciens de mon peuple. Si tu veux la racheter, rachète-la; mais si tu ne veux pas la racheter, dis-le moi, pour que je le sache. Car il n'y a personne d'autre que toi pour la racheter, et je suis après toi. » Il a dit: « Je vais la racheter. »
5 Kisha Boazi akasema, “Ile siku utakayonunua shamba kutoka mkononi mwa Naomi, yakupasa pia kumchukua Ruth Mmoabu, mjane wa mtoto wa Elimeleki, ili kuliinua jina la marehemu kama urithi wake.”
Et Boaz dit: « Le jour où tu achèteras le champ de la main de Naomi, tu devras l'acheter aussi de Ruth la Moabite, la femme du mort, pour relever le nom du mort sur son héritage. »
6 Ndipo yule jamaa wa karibu akasema, “Mimi siwezi kuikomboa ardhi kwa ajili yangu bila kuleta athari kwenye urithi wangu binafsi. Nakupa wewe haki ya kuikomboa kwa ajili yako mwenyewe, kwa kuwa mimi sitoweza.”
Le proche parent dit: « Je ne peux pas le racheter pour moi-même, de peur de mettre en danger mon propre héritage. Prends pour toi mon droit de rachat, car je ne peux pas le racheter. »
7 Hii ilikuwa ni desturi ya zamani ya Israeli kuhusu ukombozi na kubadilishana mazuri. Kudhibitisha mambo haya yote, mtu huyu alivua kiatu chake na kumpatia jirani yake; hii ilikuwa ni namna ya kufanya makubaliano ya kisheria katika Israeli.
Or voici comment on procédait autrefois en Israël pour racheter et pour échanger, afin de confirmer toutes choses: un homme ôtait sa sandale et la donnait à son prochain; et c'était ainsi qu'on officialisait les transactions en Israël.
8 Kwa hiyo huyu jamaa wa karibu akamwambia Boazi, “Inunue mwenyewe.” Kisha akavua kiatu chake.
Le proche parent dit à Boaz: « Achète-le pour toi », et il ôta sa sandale.
9 Ndipo Boazi akawaambia viongozi na watu wote, “Ninyi ni mashaidi kuwa nimenunua kila kilichokuwa cha Elimeleki na kila kilichokuwa na Kileoni na Mahilon kutoka kwenye mikono ya Naomi.
Boaz dit aux anciens et à tout le peuple: « Vous êtes témoins aujourd'hui que j'ai acheté de la main de Naomi tout ce qui appartenait à Elimélek, à Chilion et à Mahlon.
10 Zaidi ya hayo kumhusu Ruth Mmoabu, mke wa Mahlon: nimempa kibali cha kuwa mke wangu, ili kuendeleza jina na urithi wa marehumu, ili kwamba jina lake lisipotee kati ya ndugu zake na lango la watu wake. Ninyi ni mashahidi leo.”
De plus, j'ai acheté Ruth la Moabite, femme de Mahlon, pour en faire ma femme, afin de relever le nom du défunt sur son héritage, pour que le nom du défunt ne soit pas retranché du milieu de ses frères et de la porte de son lieu. Vous êtes aujourd'hui témoins. »
11 Watu wote na viongozi waliokuwa katika lango, walisema, “Tu mashahidi. Yahweh amfanye mwanamke huyu ambaye amekuja nyumbani kwako kama Raheli na Leya, ambao wawili hawa wameijenga nyumba ya Israeli. Na ubarikiwe katika Efrata na kuwa mashuhuri katika Bethelehem.
Tout le peuple qui était à la porte, et les anciens, dirent: « Nous sommes témoins. Que l'Éternel rende la femme qui est entrée dans ta maison semblable à Rachel et à Léa, qui toutes deux ont bâti la maison d'Israël; qu'il te traite dignement à Éphrata, et qu'il soit célèbre à Bethléem.
12 Na nyumba yako kama nyumba ya Peres, ambaye Tamari alimzalia yuda, kupitia uzao ambao Yahweh atakupatia pamoja na msichana huyu.”
Que ta maison soit semblable à la maison de Pérez, que Tamar a enfanté à Juda, de la descendance que Yahvé te donnera par cette jeune femme. »
13 Hivyo Boazi alimchukua Ruth, na akawa mke wake. Boazi alilala naye, na Yahweh alimruhusu kupata mimba, na alizaa mtoto wa kiume.
Et Boaz prit Ruth, et elle devint sa femme; il alla vers elle, et Yahvé lui permit de concevoir, et elle enfanta un fils.
14 Wanamke huyu akamwambia Naomi, “Yahweh abarikiwe, ambaye hajakuacha bila ndugu wa karibu, yaani mtoto huyu. Jina lake na liwe maarufu katika Israeli.
Les femmes dirent à Naomi: « Béni soit Yahvé, qui ne t'a pas laissé aujourd'hui sans parent proche. Que son nom soit célèbre en Israël.
15 Na awe kwako mrutubishaji wa maisha na mwenye ruzuku uzeeni mwako, kwa kuwa mtoto wako mkwe, ambaye anakupenda, ambaye ni bora kwako kuliko watoto wa kiume saba, amemzaa.
Il te rendra la vie et te soutiendra dans ta vieillesse, car ta belle-fille, qui t'aime et qui vaut mieux pour toi que sept fils, lui a donné naissance. »
16 Kisha naomi akamchukua mtoto, akamlaza kifuani pake, na kumhudumia.
Naomi prit l'enfant, le coucha dans son sein et en prit soin.
17 Na majirani wa yule mwanamke, wakampa jina, wakisema, “Mtoto amezaliwa kwa Naomi.” Wakawita Obedi. Ambaye alikuja kuwa baba yake na Jese, ambaye alikuja kuwa baba yake na Daudi.
Les femmes, ses voisines, lui donnèrent un nom, en disant: « Un fils est né à Naomi ». Elles lui donnèrent le nom d'Obed. Il est le père de Jessé, le père de David.
18 Hiki kilikuwa ni kizazi cha Peresi: Peres alimzaa Hezroni,
Et voici l'histoire des générations de Pérez: Pérez engendra Hetsron,
19 Hezroni akamzaa Ram, Ram akamzaa Aminadabu,
et Hetsron engendra Ram, et Ram engendra Amminadab,
20 Aminadabu akamzaa Nashon, Nashon akamzaa Salmon,
et Amminadab engendra Nahshon, et Nahshon engendra Salmon,
21 Salmon akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obed,
et Salmon engendra Boaz, et Boaz engendra Obed,
22 Obedi akamzaa Jese, na Jese akamzaa Daudi.
et Obed engendra Isaï, et Isaï engendra David.