< Ruth 3 >
1 Naomi, mama mkwe wake, alimwambia, “Mwanangu, hainilazimu kutafuta mahali pa wewe kupumzika, ili kwamba mambo yako yaende vizuri?
Naomi, sa belle-mère, lui dit: « Ma fille, ne chercherai-je pas pour toi le repos, afin que tu sois heureuse?
2 Naye Boazi, mtu ambaye umekuwa pamoja na wasichana wake wa kazi, yeye si jamaa yetu? Tazama, jioni hii atakuwa akikung'uta shairi katika sakafu ya kupuria.
N'est-ce pas Boaz, notre parent, avec les jeunes filles duquel tu étais? Voici qu'il va vanner l'orge cette nuit sur l'aire de battage.
3 Kwa hiyo, oga, jipake mafuta, uvae nguo zako nzuri, na ushuke kwenda kwenye sakafu ya kupuria. Lakini usijulikane kwa mtu huyu mpaka atakapo maliza kula na kunywa.
C'est pourquoi tu te laveras, tu t'oindras, tu t'habilleras et tu descendras à l'aire; mais ne te fais pas connaître à cet homme avant qu'il ait fini de manger et de boire.
4 Na uhakikishe kuwa, atakapo lala chini, ukumbuke mahali alipo lala ili kwamba baadaye uende kwake, ufunue miguu yake, na ulale hapo. Kisha atakuambia cha kufanya.”
Lorsqu'il se couchera, tu remarqueras le lieu où il est couché. Puis tu entreras, tu découvriras ses pieds et tu te coucheras. Il te dira alors ce que tu dois faire. »
5 Ruth alimwambia Naomi, “Nitafanya kila kitu ulicho sema.”
Elle lui répondit: « Tout ce que tu dis, je le ferai. »
6 Alishuka kwenda kwenye sakafu ya kupuria, na alifuata maelekezo aliyopewa na mama mkwe wake.
Elle descendit à l'aire de battage et fit tout ce que sa belle-mère lui avait dit.
7 Boazi alipomaliza kula na kunywa na moyo wake ulikuwa na furaha, alienda kulala chini mwisho wa sehemu ya kuhifadhia nafaka. Kisha Ruth akaenda taratibu, akaaifunua miguu ya Boazi, na kulala hapo chini.
Lorsque Boaz eut mangé et bu, et que son cœur fut joyeux, il alla se coucher à l'extrémité du tas de blé. Elle vint doucement, lui découvrit les pieds et se coucha.
8 Panapo usiku wa manane Boazi alisituka. Akajigeuza, na hapo mwanamke alikuwa amelala katika miguu yake!
A minuit, l'homme fut surpris et se retourna; et voici qu'une femme était couchée à ses pieds.
9 Akamwambia, “Wewe ni nani?” Akajibu, “Mimi ni Ruth, mtumishi wako wa kike. Nifunike shuka lako mimi mtumishi wako wa kike, kwa kuwa wewe ni jamaa wa karibu.”
Il dit: « Qui es-tu? » Elle répondit: « Je suis Ruth, ta servante. Étends donc le coin de ton vêtement sur ta servante, car tu es un proche parent. »
10 Boazi akamwambia, “Mwanangu, Yahweh akubariki. Umeonyesha wema mwishoni kuliko mwazoni, kwa sababu hukwenda kwa wanaume vijana, awe tajiri au masikini.
Il dit: « Tu es bénie par Yahvé, ma fille. Tu as montré plus de bonté à la fin qu'au début, parce que tu n'as pas suivi les jeunes gens, qu'ils soient pauvres ou riches.
11 Na sasa, mwanangu, usiogope! Nitakufanyia yote unayosema, kwa sababu mji wa watu wangu wote wanajua kuwa wewe ni mwanamke unayestahili.
Maintenant, ma fille, n'aie pas peur. Je te ferai tout ce que tu me diras, car toute la ville de mon peuple sait que tu es une femme de valeur.
12 Nikweli kuwa mimi ni jamaa wa karibu; hata hivyo, kuna jamaa wa karibu kuliko mimi.
Il est vrai que je suis un proche parent. Mais il y a un parent plus proche que moi.
13 Baki hapa usiku huu, na asubuhi, ikiwa atafanya jukumu lake la jamaa wa karibu, vizuri, muache afanye jukumu lake la kindugu. lakini kama hata fanya jukumu la kindugu kwako, ndipo mimi nitafanya, kama Yahweh aishivyo. Lala mpaka asubuhi.”
Reste cette nuit, et demain matin, s'il veut jouer pour toi le rôle d'un parent, tant mieux. Qu'il fasse son devoir de parent. Mais s'il ne veut pas faire pour toi le devoir d'un parent, je ferai pour toi le devoir d'un parent, comme Yahvé est vivant. Couche-toi jusqu'au matin. »
14 Kwa hiyo Ruth alilala kwenye miguu ya Boazi hadi asubuhi. Lakini aliamka mapema kabla ya yeyote kuweza kumtambua mtu mwingine. Kwa kuwa alikwisha mwambia, “Isijulikane kuwa mwanamke alikuja kwenye sakafu ya kupuria.”
Elle resta couchée à ses pieds jusqu'au matin, puis elle se leva avant que l'on puisse en discerner une autre. Car il avait dit: « Que l'on ne sache pas que la femme est venue à l'aire de battage. »
15 Kisha Boazi akamwambia, lete mtandio wako na uushikilie.” Alipo fanya hivyo, alipima vipimo vikubwa sita vya shairi katika mtandio na kumtwisha Ruth. Kisha Boazi akaenda mjini.
Il dit: « Apporte le manteau qui est sur toi, et tiens-le. » Elle le tint; il mesura six mesures d'orge et les posa sur elle; puis il entra dans la ville.
16 Ruth aliporudi kwa mama mkwe wake, alisema, “Ulifanyaje, mwanangu?” Ndipo Ruth akamwambia mambo yote aliyotendewa na mtu huyo.
Lorsqu'elle arriva chez sa belle-mère, elle dit: « Comment cela s'est-il passé, ma fille? » Elle lui raconta tout ce que l'homme avait fait pour elle.
17 Alimwambia, “Hivi vipimo sita vya shairi ni vile alivyonipa yeye, kwa kuwa alisema, 'Usiende mikono mitupu kwa mama mkwe wako.'”
Elle dit: « Il m'a donné ces six mesures d'orge, car il a dit: « Ne va pas à vide chez ta belle-mère ».
18 Kisha Naomi akasema, “Baki hapa, mwanangu, mpaka utakapojua yatakavyo kuwa, kwa kuwa Boazi hata pumzika mpaka atakapolimaliza jambo hili leo.”
Alors elle dit: « Attends, ma fille, jusqu'à ce que tu saches ce qui va se passer; car l'homme ne se reposera pas avant d'avoir réglé cette affaire aujourd'hui. »