< Warumi 9 >
1 Nasema ukweli katika Kristo. Sisemi uongo, na dhamira yangu hushuhudia pamoja nami katika Roho Mtakatifu,
Je dis la vérité en Christ, je ne mens point, ma conscience me rendant témoignage par le Saint-Esprit,
2 kwamba kuna huzuni kubwa na maumivu yasiyo koma ndani ya moyo wangu.
Que j'ai une grande tristesse et un continuel tourment en mon cœur.
3 Kwamba ningetamani mimi mwenyewe kulaaniwa na kutengwa mbali na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, wale wa jamii yangu katika mwili.
Car moi-même je souhaiterais d'être séparé de Christ pour mes frères, qui sont mes parents selon la chair;
4 Wao ni Waisraeli. Walio na hali ya kufanyika watoto, wa utukufu, wa maagano, na zawadi ya sheria, kumwabudu Mungu, na ahadi.
Qui sont Israëlites, desquels sont l'adoption, la gloire, les alliances, l'ordonnance de la Loi, le service divin, et les promesses.
5 Wao ni watangulizi ambako Kristo amekuja kwa heshima kuvaa mwili huu - ambaye yeye ni Mungu wa vyote. Naye asifiwe milele. Amina. (aiōn )
Desquels [sont] les pères, et desquels selon la chair [est descendu] Christ, qui est Dieu sur toutes choses, béni éternellement; Amen! (aiōn )
6 Lakini si kwamba ahadi za Mungu zimeshindwa kutimia. Maana si kila mtu aliye Israeli ni Mwiisraeli halisi.
Toutefois il ne se peut pas faire que la parole de Dieu soit anéantie; mais tous ceux qui sont d'Israël, ne sont pas pourtant Israël.
7 Sivyo hata kwa uzao wa Abrahamu kuwa ni watoto wake halisi. Lakini, “ni kupitia Isaka uzao wako utaitwa.”
Car pour être de la semence d'Abraham ils ne sont pas tous ses enfants; mais, c'est en Isaac qu'on doit considérer sa postérité.
8 Hii ni kwamba, watoto wa mwili si watoto wa Mungu. Lakini watoto wa ahadi wanatazamwa kuwa kama uzao.
c'est-à-dire, que ce ne sont pas ceux qui sont enfants de la chair, qui sont enfants de Dieu; mais que ce sont les enfants de la promesse, qui sont réputés pour semence.
9 Maana hili ndilo neno la ahadi: “Katika majira haya nitakuja, na Sara atapewa mtoto.”
Car voici la parole de la promesse: je viendrai en cette même saison, et Sara aura un fils.
10 Si hili tu, lakini baada ya Rebeka kupata mimba kwa mtu mmoja, Isaka baba yetu-
Et non seulement cela; mais aussi Rebecca, lorsqu'elle conçut d'un, [savoir] de notre père Isaac.
11 kwamba watoto walikuwa bado hawajazaliwa na alikuwa hajafanya jambo lolote zuri au baya, ili kwamba kusudi la Mungu kulingana na uchaguzi lisimame, wala si kwa matendo, lakini ni kwa sababu ya yule aitae.
Car avant que les enfants fussent nés, et qu'ils eussent fait ni bien ni mal, afin que le dessein arrêté selon l'élection de Dieu demeurât, non point par les œuvres, mais par celui qui appelle;
12 Ilinenwa kwake, “Mkubwa atamtumikia mdogo.”
Il lui fut dit: le plus grand sera asservi au moindre;
13 Kama ilivyo kwisha andikwa: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
Ainsi qu'il est écrit: j'ai aimé Jacob, et j'ai haï Esaü.
14 Basi tena tutasema nini? Je kuna udhalimu kwa Mungu? La hasha.
Que dirons-nous donc: y a-t-il de l'iniquité en Dieu? à Dieu ne plaise!
15 Kwa kuwa anasema kwa Musa, “nitakuwa na rehema kwa yule nitakayemrehemu, na nitakuwa na huruma kwa yule nitakayemhurumia.”
Car il dit à Moïse: j'aurai compassion de celui de qui j'aurai compassion; et je ferai miséricorde à celui à qui je ferai miséricorde.
16 Kwa hiyo basi, si kwa sababu ya yeye atakaye, wala si kwa sababu ya yeye ambaye hukimbia, lakini kwa sababu ya Mungu, ambaye huonesha rehema.
Ce n'est donc point du voulant, ni du courant: mais de Dieu qui fait miséricorde.
17 Kwa kuwa maandiko husema kwa Farao, “Kwa kusudi hili maalumu nilikuinua, ili kwamba nioneshe nguvu zangu katika wewe, na ili kwamba jina langu litangazwe katika nchi yote.”
Car l'Ecriture dit à Pharaon: je t'ai fait subsister dans le but de démontrer en toi ma puissance, et afin que mon Nom soit publié dans toute la terre.
18 Hivyo basi, Mungu huwa na rehema kwa yeyote ampendaye, na kwa ambaye humpenda, humfanya kuwa mkaidi.
Il a donc compassion de celui qu'il veut, et il endurcit celui qu'il veut.
19 Kisha utasema kwangu, “Kwa nini bado anaona kosa? Ni yupi ambaye alikwisha kustahimili matakwa yake?”
Or tu me diras: pourquoi se plaint-il encore? car qui est celui qui peut résister à sa volonté?
20 Kinyume chake, mwanadamu, wewe ni nani ujibue kinyume na Mungu? Kuna uwezekano wowote wa kilichofinyangwa kusema kwa mfinyanzi, “Kwanini ulinifanya hivi mimi?”
Mais plutôt, ô homme, qui es-tu, toi qui contestes contre Dieu? la chose formée dira-t-elle à celui qui l'a formée: pourquoi m'as-tu ainsi faite?
21 Je mfinyazi huwa hana haki juu ya udongo kutengeneza chombo kwa matumizi maalumu kutokana na bonge lile lile, na chombo kingine kwa matumizi ya kila siku?
Le potier de terre n'a-t-il pas la puissance de faire d'une même masse de terre un vaisseau à honneur, et un autre à déshonneur?
22 Vipi kama Mungu, ambaye ana utayari wa kuonesha gadhabu yake na kufanya nguvu yake kujulikana, alistahimili kwa uvumilivu wa kutosha vyombo vya gadhabu vilivyoandaliwa kwa kuangamiza?
Et [qu'est-ce], si Dieu en voulant montrer sa colère, et donner à connaître sa puissance, a toléré avec une grande patience les vaisseaux de colère, préparés pour la perdition?
23 Vipi kama alifanya hivi ili kwamba aoneshe wingi wa utukufu wake juu ya vyombo vya rehema, ambavyo alikwisha kuviandaa kwa ajili ya utukufu?
Et afin de donner à connaître les richesses de sa gloire dans les vaisseaux de miséricorde, qu'il a préparés pour la gloire;
24 Vipi kama alifanya hii pia kwetu, ambaye pia alituita, si tu kutoka kwa Wayahudi, lakini pia kutoka kwa watu wa Mataifa?
Et qu'il a appelés, [c'est à savoir] nous, non seulement d'entre les Juifs, mais aussi d'entre les Gentils.
25 Kama asemavyo pia katika Hosea: “Nitawaita watu wangu ambao hawakuwa watu wangu, na mpendwa wake ambaye hakupendwa.
Selon ce qu'il dit en Osée: j'appellerai mon peuple celui qui n'était point mon peuple; et la bien-aimée, celle qui n'était point la bien-aimée;
26 Na itakuwa kwamba pale iliposemwa kwao, 'Ninyi si watu wangu,' pale wataitwa 'wana wa Mungu aliye hai.”'
Et il arrivera, qu'au lieu où il leur a été dit: vous n'êtes point mon peuple, là ils seront appelés les enfants du Dieu vivant.
27 Isaya analia kuhusiana na Israeli, “Kama hesabu ya wana wa Israeli ingekuwa kama mchanga wa bahari, itakuwa ni masalia ambao wataokolewa.
Aussi Esaïe s'écrie au sujet d'Israël: quand le nombre des enfants d'Israël serait comme le sable de la mer, il n'y en aura qu'un [petit] reste de sauvé.
28 Kwa kuwa Bwana atalichukua neno lake juu ya nchi, mapema na kwa utimilifu.
Car le Seigneur consomme et abrège l'affaire en justice: il fera, dis-je, une affaire abrégée sur la terre.
29 Na kama jinsi Isaya alivyosema awali, “Kama Bwana wa majeshi hakutuachia nyuma uzao kwa ajili yetu, tungekuwa kama Sodoma, na tungefanywa kama Gomora.
Et comme Esaïe avait dit auparavant: si le Seigneur des armées ne nous eût laissé quelque semence, nous eussions été faits comme Sodome, et eussions été semblables à Gomorrhe.
30 Tutasema nini basi? kwamba watu wa Mataifa ambao walikuwa hawatafuti haki, walipata haki, haki kwa imani.
Que dirons-nous donc? que les Gentils qui ne cherchaient point la justice, ont atteint la justice, la justice, dis-je, qui est par la foi.
31 Lakini Israeli, ambaye alitafuta sheria ya haki, hakuifikia.
Mais Israël cherchant la Loi de la justice, n'est point parvenu à la Loi de la justice.
32 Kwanini si hivyo? Kwa sababu hawakuitafuta kwa imani, bali kwa matendo. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa,
Pourquoi? parce que ce n'a point été par la foi, mais comme par les œuvres de la Loi; car ils ont heurté contre la pierre d'achoppement.
33 kama ilivyo kwisha andikwa, “Tazama, nimelaza jiwe la kujikwaa katika Sayuni na mwamba wa kukosa. Yeye ambaye huamini katika hili hataaibika.”
Selon ce qui est écrit: voici, je mets en Sion la pierre d'achoppement; et la pierre qui occasionnera des chutes; et quiconque croit en lui ne sera point confus.