< Warumi 8 >

1 Kwa hiyo basi hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
Przetoż teraz żadnego potępienia nie masz tym, który będąc w Chrystusie Jezusie nie według ciała chodzą, ale według Ducha.
2 Kwa kuwa kanuni ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imenifanya mimi kuwa huru mbali na kanuni ya dhambi na mauti.
Albowiem zakon Ducha żywota, który jest w Chrystusie Jezusie, uwolnił mię od zakonu grzechu śmierci.
3 Kwa maana kile ambacho sheria ilishindwa kufanya kwa sababu ilikuwa dhaifu katika mwili, Mungu alifanya. Alimtuma Mwana wake wa pekee kwa mfano wa mwili wa dhambi awe sadaka ya dhambi, na akaihukumu dhambi katika mwili.
Bo co niemożnego było zakonowi, w czem on był słaby dla ciała, Bóg posławszy Syna swego w podobieństwie grzesznego ciała i dla grzechu, potępił grzech w ciele,
4 Alifanya hivi ili maagizo ya sheria yatimilizwe ndani yetu, sisi tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili, bali kwa kufuata mambo ya Roho.
Aby ona sprawiedliwość zakonu była wypełniona w nas, którzy nie według ciała chodzimy, ale według Ducha.
5 Wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili, lakini wale waifuatao Roho huyafikiri mambo ya Roho.
Albowiem, którzy są według ciała, o tem myślą, co jest cielesnego; ale którzy są według Ducha, myślą o tem, co jest duchowego.
6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti, bali nia ya Roho ni uzima na amani.
Gdyż zmysł ciała jest śmierć; ale zmysł ducha jest żywot i pokój,
7 Hii ni kwa sababu ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.
Przeto iż zmysł ciała jest nieprzyjacielem Bogu; bo się zakonowi Bożemu nie poddaje, gdyż też i nie może.
8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
Przetoż którzy są w ciele, Bogu się podobać nie mogą.
9 Hata hivyo, hampo katika mwili bali katika Roho, kama ni kweli kwamba Roho wa Mungu huishi ndani yenu. Lakini kama mtu hana Roho wa Kristo, yeye si wake.
Lecz wy nie jesteście w ciele, ale w duchu, gdyż Duch Boży mieszka w was: a jeźli kto Ducha Chrystusowego nie ma, ten nie jest jego.
10 Kama Kristo yumo ndani yenu, mwili umekufa kwa mambo ya dhambi, bali roho ni hai kwa mambo ya haki.
Ale jeźli Chrystus w was jest, tedy ciało jest martwe dla grzechu, a duch jest żywy dla sprawiedliwości.
11 Ikiwa Roho wa yule aliyemfufua Yesu kutoka wafu huishi ndani yenu, yeye yule aliyemfufua Kristo kutoka katika wafu ataipa pia miili yenu ya mauti uhai kwa njia ya Roho wake, aishie ndani yenu.
A jeźli Duch tego, który Jezusa wzbudził z martwych, mieszka w was, ten który wzbudził Chrystusa z martwych, ożywi i śmiertelne ciała wasze przez Ducha swego, który w was mieszka.
12 Hivyo basi, ndugu zangu, sisi tu wadeni, lakini si kwa mwili kwamba tuishi kwa jinsi ya mwili.
A tak, bracia! dłużnikami jesteśmy nie ciału, abyśmy według ciała żyli.
13 Maana ikiwa mnaishi kwa jinsi ya mwili, mpo karibu kufa, lakini ikiwa kwa Roho mnayafisha matendo ya mwili, nanyi mtaishi.
Albowiem jeźlibyście według ciała żyli, pomrzecie; ale jeźlibyście Duchem sprawy ciała umartwili, żyć będziecie.
14 Maana kama ambavyo wengi wanaongozwa na Roho wa Mungu, hawa ni wana wa Mungu.
Bo którzykolwiek Duchem Bożym prowadzeni bywają, ci są synami Bożymi.
15 Kwa kuwa hamkupokea roho wa utumwa tena hata muogope. Badala yake, mlipokea roho ya kufanywa kuwa wana, ambayo kwayo tunalia, “Abba, Baba!”
Gdyżeście nie wzięli ducha niewoli znowu ku bojaźni, aleście wzięli Ducha przysposobienia synowskiego, przez którego wołamy: Abba, to jest Ojcze!
16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kuwa tu watoto wa Mungu.
Tenże duch poświadcza duchowi naszemu, iż jesteśmy dziećmi Bożymi.
17 Ikiwa tu watoto, basi tu warithi pia, warithi wa Mungu. Na sisi tu warithi pamoja na Kristo, ikiwa kwa kweli tunateseka na yeye ili tupate kutukuzwa pamoja naye.
A jeźliż dziećmi, tedy i dziedzicami, dziedzicami wprawdzie Bożymi, a spółdziedzicami Chrystusowymi, jeźli tylko z nim cierpimy, abyśmy też z nim byli uwielbieni.
18 Kwa kuwa nayahesabu mateso ya wakati huu kuwa si kitu nikilinganisha na utukufu utakaofunuliwa kwetu.
Albowiem, (bracia!) mam za to, iż utrapienia teraźniejszego czasu nie są godne onej przyszłej chwały, która się ma objawić w nas.
19 Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.
Bo troskliwe wyglądanie stworzenia oczekuje objawienia synów Bożych.
20 Kwa maana uumbaji pia ulitiishwa chini ya ubatili, si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye aliyevitiisha. Ni katika tumaini
Gdyż stworzenie marności jest poddane, nie dobrowolnie, ale dla tego, który je poddał,
21 kwamba uumbaji wenyewe nao utawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, na kuingizwa katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.
Pod nadzieją, że i samo stworzenie będzie uwolnione z niewoli skażenia na wolność chwały dziatek Bożych.
22 Kwa maana twajua ya kuwa uumbaji nao pia unaugua na kuteseka kwa uchungu pamoja hata sasa.
Bo wiemy, iż wszystko stworzenie wespół wzdycha i wespół boleje aż dotąd.
23 Si hivyo tu, ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho - sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukisubiri kufanywa wana, yaani ukombozi wa miili yetu.
A nie tylko ono stworzenie, ale i my, którzy mamy pierwiastki Ducha, i my sami w sobie wzdychamy, oczekując przysposobienia synowskiego, odkupienia ciała naszego.
24 Kwa maana ni kwa taraja hili tuliokolewa. Lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana hakuna taraja tena, kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho?
Albowiem nadziejąśmy zbawieni. A nadzieja widoma nie jest nadzieją; bo co kto widzi, przecz się tego spodziewa?
25 Bali tukikitarajia kitu tusichokiona, twakingojea kwa saburi.
Ale czego nie widzimy, tego się spodziewamy i tego przez cierpliwość oczekujemy.
26 Kwa jinsi iyo hiyo, Roho naye hutusaidia katika udhaifu wetu. Kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Także też i Duch dopomaga mdłościom naszym. Albowiem o co byśmy się modlić mieli, jako potrzeba, nie wiemy; ale tenże Duch przyczynia się za nami wzdychaniem niewymownem.
27 Na yeye aichunguzaye mioyo huijua akili ya Roho, kwa sababu huomba kwa niaba yao walioamini kulingana na mapenzi ya Mungu.
A ten, który się serc bada, wie, który jest zmysł Ducha, ponieważ według Boga przyczynia się za świętymi.
28 Nasi twajua ya kuwa kwa wote wampendao Mungu, yeye hufanya mambo yote pamoja kwa wema, kwa wale wote walioitwa kwa kusudi lake.
A wiemy, iż tym, którzy miłują Boga, wszystkie rzeczy dopomagają ku dobremu, to jest tym, którzy według postanowienia Bożego powołani są.
29 Kwa sababu wale wote aliowajua tangu asili, pia aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miogoni mwa ndugu wengi.
Albowiem, które on przejrzał, te też przenaznaczył, aby byli przypodobani obrazowi Syna jego, żeby on był pierworodnym między wieloma braćmi,
30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao aliwaita pia. Na wale aliowaita, hao aliwahesabia haki. Na wale aliowahesabia haki, hao pia akawatukuza.
A które przenaznaczył, te też powołał; a które powołał, te też usprawiedliwił; a które usprawiedliwił, te też uwielbił.
31 Tuseme nini basi juu ya mambo haya? Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu?
Cóż tedy rzeczemy na to? Jeźli Bóg za nami, któż przeciwko nam?
32 Yeye asiyemwachilia mwana wake mwenyewe bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?
Który ani własnemu Synowi nie przepuścił, ale go za nas wszystkich wydał: jakoż by wszystkiego z nim nie darował nam?
33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
Któż będzie skarżył na wybrane Boże? Bóg jest, który usprawiedliwia.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa kwa ajili yetu, na zaidi ya hayo, yeye pia alifufuliwa. Naye anatawala pamoja na Mungu mahali pa heshima, na tena ndiye anayetuombea sisi.
Któż jest, co by je potępił? Chrystus jest, który umarł, owszem i zmartwychwstał, który też jest na prawicy Bożej, który się też przyczynia za nami.
35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Dhiki, au shida, au mateso, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?
Któż nas odłączy od miłości Chrystusowej? czyli utrapienie? czyli ucisk? czyli prześladowanie? czyli głód? czyli nagość? czyli niebezpieczeństwo? czyli miecz?
36 Kama ilivyoandikwa, “Kwa faida yako tunauawa mchana kutwa. Tulihesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”
Jako napisano: Dla ciebie cały dzień zabijani bywamy, poczytaniśmy jako owce na rzeź naznaczone;
37 Katika mambo haya yote sisi tu zaidi ya washindi katika yeye aliyetupenda.
Ale w tem wszystkiem przezwyciężamy przez tego, który nas umiłował.
38 Kwa maana nimekwisha kushawishika kwamba wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala mamlaka, wala vitu vilivyopo, wala vitu vijavyo, wala nguvu,
Albowiem pewienem tego, iż ani śmierć, ani żywot, ani Aniołowie, ani księstwa, ani mocarstwa, ani teraźniejsze ani przyszłe rzeczy,
39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote, hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu, ambaye ni Kristo Yesu Bwana wetu.
Ani wysokość, ani głębokość, ani żadne insze stworzenie nie będzie nas mogło odłączyć od miłości Bożej, która jest w Jezusie Chrystusie, Panu naszym.

< Warumi 8 >