< Warumi 8 >

1 Kwa hiyo basi hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
No therefore now condemnation to those in Christ Jesus (not according to flesh walk but according to spirit. *K*)
2 Kwa kuwa kanuni ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imenifanya mimi kuwa huru mbali na kanuni ya dhambi na mauti.
For the law of the Spirit of life in Christ Jesus has set free (you *N(K)O*) from the law of sin and of death.
3 Kwa maana kile ambacho sheria ilishindwa kufanya kwa sababu ilikuwa dhaifu katika mwili, Mungu alifanya. Alimtuma Mwana wake wa pekee kwa mfano wa mwili wa dhambi awe sadaka ya dhambi, na akaihukumu dhambi katika mwili.
For powerless [being] the law, in that it was weak through the flesh, God His own Son having sent in likeness of flesh of sin and for sin condemned sin in the flesh,
4 Alifanya hivi ili maagizo ya sheria yatimilizwe ndani yetu, sisi tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili, bali kwa kufuata mambo ya Roho.
so that the righteousness of the law may be fulfilled in us not according to [the] flesh walking but according to [the] Spirit.
5 Wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili, lakini wale waifuatao Roho huyafikiri mambo ya Roho.
Those for according to flesh being the [things] of the flesh mind those however according to Spirit the [things] of the Spirit.
6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti, bali nia ya Roho ni uzima na amani.
The for mind of the flesh [is] death, the but mind of the Spirit life and peace.
7 Hii ni kwa sababu ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.
because the mind of the flesh [is] hostility toward God; for the law of God not it is subject, nor even for can it [be];
8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
Those now in flesh being God to please not are able;
9 Hata hivyo, hampo katika mwili bali katika Roho, kama ni kweli kwamba Roho wa Mungu huishi ndani yenu. Lakini kama mtu hana Roho wa Kristo, yeye si wake.
You yourselves now not are in flesh but in Spirit, if indeed if indeed Spirit of God dwells in you. if however anyone [the] Spirit of Christ not has, he not is of Him.
10 Kama Kristo yumo ndani yenu, mwili umekufa kwa mambo ya dhambi, bali roho ni hai kwa mambo ya haki.
If now Christ [is] in you, the indeed body [is] dead on account of sin the however Spirit [is] life on account of righteousness.
11 Ikiwa Roho wa yule aliyemfufua Yesu kutoka wafu huishi ndani yenu, yeye yule aliyemfufua Kristo kutoka katika wafu ataipa pia miili yenu ya mauti uhai kwa njia ya Roho wake, aishie ndani yenu.
If now the Spirit of the [One] having raised up (*no*) Jesus out from [the] dead dwells in you, the [One] having raised up (*k*) Christ out from [the] dead (Jesus *O*) will give life also to the mortal bodies of you on account of (the dwelling *N(k)O*) of His (Spirit *N(k)O*) in you.
12 Hivyo basi, ndugu zangu, sisi tu wadeni, lakini si kwa mwili kwamba tuishi kwa jinsi ya mwili.
So then, brothers, debtors we are not to the flesh according to flesh to live;
13 Maana ikiwa mnaishi kwa jinsi ya mwili, mpo karibu kufa, lakini ikiwa kwa Roho mnayafisha matendo ya mwili, nanyi mtaishi.
If for according to flesh you live, you are about to die; if however by [the] Spirit the deeds of the body you put to death, you will live.
14 Maana kama ambavyo wengi wanaongozwa na Roho wa Mungu, hawa ni wana wa Mungu.
As many as for by [the] Spirit of God are led, these sons of God are.
15 Kwa kuwa hamkupokea roho wa utumwa tena hata muogope. Badala yake, mlipokea roho ya kufanywa kuwa wana, ambayo kwayo tunalia, “Abba, Baba!”
Not for you have received a spirit of bondage again to fear, but you have received [the] Spirit of divine adoption as sons by whom we cry; Abba O Father!
16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kuwa tu watoto wa Mungu.
Himself the Spirit bears witness with the spirit of us that we are children of God.
17 Ikiwa tu watoto, basi tu warithi pia, warithi wa Mungu. Na sisi tu warithi pamoja na Kristo, ikiwa kwa kweli tunateseka na yeye ili tupate kutukuzwa pamoja naye.
If now children, also heirs; heirs indeed of God joint-heirs however of Christ; if indeed if indeed we suffer with [Him] so that also we shall be glorified together.
18 Kwa kuwa nayahesabu mateso ya wakati huu kuwa si kitu nikilinganisha na utukufu utakaofunuliwa kwetu.
I reckon for that not comparable the sufferings of the present time [are] to the coming glory to be revealed to us.
19 Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.
The for earnest expectation of the creation the revelation of the sons of God awaits;
20 Kwa maana uumbaji pia ulitiishwa chini ya ubatili, si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye aliyevitiisha. Ni katika tumaini
To the for futility the creation was subjected, not willingly but because of the [One] having subjected [it], in hope
21 kwamba uumbaji wenyewe nao utawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, na kuingizwa katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.
for also itself the creation will be set free from the bondage of decay into the freedom of the glory of the children of God.
22 Kwa maana twajua ya kuwa uumbaji nao pia unaugua na kuteseka kwa uchungu pamoja hata sasa.
We know for that all the creation groans together and it travails together until now;
23 Si hivyo tu, ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho - sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukisubiri kufanywa wana, yaani ukombozi wa miili yetu.
Not only [so] now, but even ourselves the firstfruit of the Spirit having we ourselves also ourselves in ourselves groan divine adoption as sons awaiting, the redemption of the body of us.
24 Kwa maana ni kwa taraja hili tuliokolewa. Lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana hakuna taraja tena, kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho?
In this for hope we were saved; hope however being seen not is hope; what for sees any (why also *KO*) does he hope for [it]?
25 Bali tukikitarajia kitu tusichokiona, twakingojea kwa saburi.
If however what not we see we hope for, in patience we await.
26 Kwa jinsi iyo hiyo, Roho naye hutusaidia katika udhaifu wetu. Kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Likewise now also the Spirit joins to help (the *N(k)O*) (weakness *N(K)O*) of us; the for things which (we may pray for *NK(o)*) as it behooves not we know, but Himself the Spirit makes intercession (for *k*) (of us *K*) with groanings inexpressible;
27 Na yeye aichunguzaye mioyo huijua akili ya Roho, kwa sababu huomba kwa niaba yao walioamini kulingana na mapenzi ya Mungu.
The [One] now searching hearts knows what [is] the mindset of the Spirit, because according to God He intercedes for [the] saints.
28 Nasi twajua ya kuwa kwa wote wampendao Mungu, yeye hufanya mambo yote pamoja kwa wema, kwa wale wote walioitwa kwa kusudi lake.
We know now that to those loving God all things works together (God *O*) for good, to those according to [His] purpose called being.
29 Kwa sababu wale wote aliowajua tangu asili, pia aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miogoni mwa ndugu wengi.
For those whom He foreknew, also He predestined [to be] conformed to the image of the Son of Him for to be Him firstborn among many brothers;
30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao aliwaita pia. Na wale aliowaita, hao aliwahesabia haki. Na wale aliowahesabia haki, hao pia akawatukuza.
Those whom then He predestined, these also He called; and whom He called, these also He justified; whom then He justified, these also He glorified.
31 Tuseme nini basi juu ya mambo haya? Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu?
What then will we say to these things? If God [is] for us, who [can be] against us?
32 Yeye asiyemwachilia mwana wake mwenyewe bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?
He who indeed [his] own Son not spared, but for us all gave up Him, how surely also with Him the [things] all us will He grant?
33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
Who will bring an accusation against [the] elect of God? God [is] who is justifying;
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa kwa ajili yetu, na zaidi ya hayo, yeye pia alifufuliwa. Naye anatawala pamoja na Mungu mahali pa heshima, na tena ndiye anayetuombea sisi.
Who [is] the [one] condemning? [For it is] Christ (Jesus *NO*) the [one] having died rather now (also *k*) having been raised up (from dead *O*) who also is at [the] right hand of God, who and is interceding for us.
35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Dhiki, au shida, au mateso, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?
Who us will separate from the love of Christ? Tribulation or distress or persecution or famine or nakedness or danger or sword?
36 Kama ilivyoandikwa, “Kwa faida yako tunauawa mchana kutwa. Tulihesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”
Even as it has been written that For the sake of you we face death all the day, we were regarded as sheep of slaughter.
37 Katika mambo haya yote sisi tu zaidi ya washindi katika yeye aliyetupenda.
But in these things all we more than conquer through the [One who] having loved us;
38 Kwa maana nimekwisha kushawishika kwamba wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala mamlaka, wala vitu vilivyopo, wala vitu vijavyo, wala nguvu,
I have been persuaded for that neither death nor life nor angels nor principalities nor things being present nor things to come nor powers
39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote, hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu, ambaye ni Kristo Yesu Bwana wetu.
nor height nor depth nor any created thing other will be able us to separate from the love of God in Christ Jesus the Lord of us.

< Warumi 8 >