< Warumi 8 >

1 Kwa hiyo basi hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
There is now, therefore, no condemnation to those who are in Christ Jesus.
2 Kwa kuwa kanuni ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imenifanya mimi kuwa huru mbali na kanuni ya dhambi na mauti.
For the law of the spirit of life in Christ Jesus has freed me from the law of sin, and of death.
3 Kwa maana kile ambacho sheria ilishindwa kufanya kwa sababu ilikuwa dhaifu katika mwili, Mungu alifanya. Alimtuma Mwana wake wa pekee kwa mfano wa mwili wa dhambi awe sadaka ya dhambi, na akaihukumu dhambi katika mwili.
For what the law could not do, because it was weak through the flesh, God has done, who, sending his own son in the likeness of sinful flesh, and for a sin-offering, condemned sin in the flesh,
4 Alifanya hivi ili maagizo ya sheria yatimilizwe ndani yetu, sisi tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili, bali kwa kufuata mambo ya Roho.
that the righteousness of the law might be fulfilled in us, who walk not according to the flesh, but according to the Spirit.
5 Wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili, lakini wale waifuatao Roho huyafikiri mambo ya Roho.
For those who are according to the flesh, mind the things of the flesh; but those who are according to the Spirit, the things of the Spirit.
6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti, bali nia ya Roho ni uzima na amani.
For the mind of the flesh is death; but the mind of the Spirit is life and peace.
7 Hii ni kwa sababu ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.
Because the mind of the flesh is enmity against God; for it is not subject to the law of God, nor indeed can it be.
8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
Those, then, who are in the flesh, can not please God.
9 Hata hivyo, hampo katika mwili bali katika Roho, kama ni kweli kwamba Roho wa Mungu huishi ndani yenu. Lakini kama mtu hana Roho wa Kristo, yeye si wake.
But you are not in the flesh, but in the Spirit, if indeed the Spirit of God dwells in you. Now, if any one has not the Spirit of Christ, he is not his.
10 Kama Kristo yumo ndani yenu, mwili umekufa kwa mambo ya dhambi, bali roho ni hai kwa mambo ya haki.
But if Christ is in you, the body is dead, on account of sin, but the Spirit is life, on account of righteousness.
11 Ikiwa Roho wa yule aliyemfufua Yesu kutoka wafu huishi ndani yenu, yeye yule aliyemfufua Kristo kutoka katika wafu ataipa pia miili yenu ya mauti uhai kwa njia ya Roho wake, aishie ndani yenu.
And if the Spirit of him who raised Jesus from the dead dwells in you, he that raised the Christ from the dead will give life to your mortal bodies, because of his Spirit that dwells in you.
12 Hivyo basi, ndugu zangu, sisi tu wadeni, lakini si kwa mwili kwamba tuishi kwa jinsi ya mwili.
Therefore, brethren, we are debtors, not to the flesh, to live according to the flesh;
13 Maana ikiwa mnaishi kwa jinsi ya mwili, mpo karibu kufa, lakini ikiwa kwa Roho mnayafisha matendo ya mwili, nanyi mtaishi.
for if you live according to the flesh, you shall die: but if, through the Spirit, you put to death the deeds of the body, you shall live.
14 Maana kama ambavyo wengi wanaongozwa na Roho wa Mungu, hawa ni wana wa Mungu.
For as many as are led by the Spirit of God, they are the sons of God.
15 Kwa kuwa hamkupokea roho wa utumwa tena hata muogope. Badala yake, mlipokea roho ya kufanywa kuwa wana, ambayo kwayo tunalia, “Abba, Baba!”
For you have not again received the spirit of bondage, that you may fear; but you have received the spirit of adoption, by which we cry, Abba, Father.
16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kuwa tu watoto wa Mungu.
The Spirit itself testifies with our spirit, that we are the children of God;
17 Ikiwa tu watoto, basi tu warithi pia, warithi wa Mungu. Na sisi tu warithi pamoja na Kristo, ikiwa kwa kweli tunateseka na yeye ili tupate kutukuzwa pamoja naye.
and, if children, then heirs; heirs of God, and joint-heirs with Christ, if indeed we suffer with him, that we may also be glorified together.
18 Kwa kuwa nayahesabu mateso ya wakati huu kuwa si kitu nikilinganisha na utukufu utakaofunuliwa kwetu.
For I consider the sufferings of the present time not worthy to be compared with the glory that shall be revealed for us.
19 Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.
For the earnest expectation of the creature waits for the revelation of the sons of God.
20 Kwa maana uumbaji pia ulitiishwa chini ya ubatili, si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye aliyevitiisha. Ni katika tumaini
For the creature was subject to frailty, (not by its own will, but for his sake who subjected it, )
21 kwamba uumbaji wenyewe nao utawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, na kuingizwa katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.
in hope, that even the creature itself shall be made free from the bondage of corruption, and introduced into the glorious liberty of the children of God.
22 Kwa maana twajua ya kuwa uumbaji nao pia unaugua na kuteseka kwa uchungu pamoja hata sasa.
For we know that every creature groans, and is in pain together, till now:
23 Si hivyo tu, ila na sisi wenyewe tulio na malimbuko ya Roho - sisi pia tunaugua katika nafsi zetu, tukisubiri kufanywa wana, yaani ukombozi wa miili yetu.
and not only they, but ourselves also, who have the first fruits of the Spirit, even we ourselves groan within ourselves, waiting for the adoption, the redemption of our body.
24 Kwa maana ni kwa taraja hili tuliokolewa. Lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana hakuna taraja tena, kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho?
For we are saved by this hope; but hope that is seen is not hope; for, what any one sees, why does he also hope for it?
25 Bali tukikitarajia kitu tusichokiona, twakingojea kwa saburi.
But if we hope for that which we see not we wait for it with patience.
26 Kwa jinsi iyo hiyo, Roho naye hutusaidia katika udhaifu wetu. Kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
In like manner, also, the Spirit helps our infirmities; for we know not what we should pray for as we ought, but the Spirit itself intercedes for us, with groanings unutterable.
27 Na yeye aichunguzaye mioyo huijua akili ya Roho, kwa sababu huomba kwa niaba yao walioamini kulingana na mapenzi ya Mungu.
And he that searches the hearts knows what is the mind of the Spirit, that he intercedes for the saints according to the will of God.
28 Nasi twajua ya kuwa kwa wote wampendao Mungu, yeye hufanya mambo yote pamoja kwa wema, kwa wale wote walioitwa kwa kusudi lake.
And we know that all things work together for good, to those who love God, to those who are called according to his purpose.
29 Kwa sababu wale wote aliowajua tangu asili, pia aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miogoni mwa ndugu wengi.
For those whom he foreknew, he predestinated to be conformed to the image of his Son, that he might be the first-born among many brethren:
30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao aliwaita pia. Na wale aliowaita, hao aliwahesabia haki. Na wale aliowahesabia haki, hao pia akawatukuza.
and those whom he predestinated he also called, and those whom he called he also justified, and those whom he justified he also glorified.
31 Tuseme nini basi juu ya mambo haya? Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu?
What, then, shall we say to these things? If God be for us, who can be against us?
32 Yeye asiyemwachilia mwana wake mwenyewe bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?
He that spared not his own Son, but delivered him up for us all, how will he not with him also freely give us all things?
33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.
Who shall lay any thing to the charge of God’s elect? It is God that justifies.
34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa kwa ajili yetu, na zaidi ya hayo, yeye pia alifufuliwa. Naye anatawala pamoja na Mungu mahali pa heshima, na tena ndiye anayetuombea sisi.
Who is he that condemns? It is Christ that died: rather, indeed, that has risen, who is at the right hand of God, who also intercedes for us.
35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Dhiki, au shida, au mateso, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?
Who shall separate us from the love of the Christ? Shall affliction, or distress, or persecution, or famine, or nakedness, or danger, or the sword?
36 Kama ilivyoandikwa, “Kwa faida yako tunauawa mchana kutwa. Tulihesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”
As it is written: For thy sake, we are killed all the day long; we are counted as sheep for the slaughter.
37 Katika mambo haya yote sisi tu zaidi ya washindi katika yeye aliyetupenda.
Yet, in all these things, we are more than conquerors, through him that loved us.
38 Kwa maana nimekwisha kushawishika kwamba wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala mamlaka, wala vitu vilivyopo, wala vitu vijavyo, wala nguvu,
For I am persuaded that neither death, nor life, nor angels, nor principalities, nor powers, nor things present, nor things to come,
39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote, hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu, ambaye ni Kristo Yesu Bwana wetu.
nor hight, nor depth, nor any other creature, will be able to separate us from the love of God which is in Christ Jesus our Lord.

< Warumi 8 >