< Warumi 7 >
1 Au hamjui, ndugu zangu (kwa kuwa naongea na watu wanaoijua sheria), kwamba sheria humtawala mtu anapokuwa hai?
Azaż nie wiecie, bracia! (bo powiadomym zakonu mówię), iż zakon panuje nad człowiekiem, póki żyje?
2 Kwa maana mwanamke aliyeolewa amefungwa na sheria kwa yule mme wake anapokuwa hai, lakini ikiwa mme wake atakufa, atakuwa amewekwa huru kutoka sheria ya ndoa.
Albowiem niewiasta, która jest za mężem, póki żyw mąż, obowiązana mu jest zakonem; a jeźliby mąż umarł, uwolniona jest od zakonu mężowego.
3 Hivyo basi, wakati mme wake angali akiishi, ikiwa anaishi na mwanamme mwingine, ataitwa mzinzi. Lakini ikiwa mme wake akifa, yuko huru dhidi ya sheria, hivyo hatakuwa mzinzi ikiwa anaishi na mwanamme mwingine.
Przetoż tedy, póki mąż żyje, będzie zwana cudzołożnicą, jeźliby żoną inszego męża została; a jeźliby mąż jej umarł, wolna jest od zakonu onego, aby nie była cudzołożnicą, choćby się inszego męża żoną stała.
4 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninyi pia mlifanywa wafu kwa sheria kwa njia ya mwili wa Kristo. Imekuwa hivi ili mpate kuunganishwa na mwingine, kwake yeye ambaye alifufuliwa kutoka wafu ili tuweze kumzalia Mungu matunda.
A tak, bracia moi! i wyście umartwieni zakonowi przez ciało Chrystusowe, abyście się stali inszego, to jest tego, który wzbudzony jest z martwych, abyśmy owoc przynosili Bogu.
5 Kwa maana tulipokuwa katika hali ya mwili, tamaa za dhambi ziliamshwa katika viungo vyetu kwa njia ya sheria na kuizalia mauti matunda.
Albowiem gdyśmy byli w ciele, namiętności grzechów, które się wzniecały przez zakon, mocy dokazywały w członkach naszych ku przynoszeniu owocu śmierci.
6 Lakini sasa tumefunguliwa kutoka katika sheria. Tumeifia ile hali iliyotupinga. Ili sisi tupate kutumika katika hali mpya ya Roho, na si katika hali ya zamani ya andiko.
Lecz teraz staliśmy się wolni od zakonu, umarłszy temu, w którymeśmy byli zatrzymani, abyśmy Bogu służyli w nowości ducha, a nie w starości litery.
7 Tusemeje basi? Sheria ni dhambi? La hasha. Hata hivyo, nisingelitambua dhambi, isingelikuwa kwa njia ya sheria. Kwa kuwa nisingelijua kutamani kama sheria isingelisema, “Usitamani.”
Cóż tedy rzeczemy? Iż zakon jest grzechem? Nie daj tego Boże! I owszemem grzechu nie poznał, tylko przez zakon; bo i o pożądliwości bym był nie wiedział, by był zakon nie rzekł: Nie będziesz pożądał.
8 Lakini dhambi ilipata nafasi kwa ile amri na ikaleta ndani yangu kila aina ya kutamani. Kwa maana dhambi pasipo sheria imekufa.
Lecz grzech wziąwszy przyczynę przez przykazanie, sprawił we mnie wszelką pożądliwość; albowiem bez zakonu grzech jest martwy.
9 Nami nilikuwa hai hapo kwanza bila sheria, lakini ilipokuja ile amri, dhambi ilipata uhai, nami nikafa.
I jam żył niekiedy bez zakonu; lecz gdy przyszło przykazanie, grzech ożył, a jam umarł.
10 Ile amri na ambayo ingelileta uzima iligeuka kuwa mauti kwangu.
I znalazło się, że to przykazanie, które miało być ku żywotowi, jest mi ku śmierci.
11 Kwa maana dhambi ilipata nafasi kwa ile amri na ikanidanganya. Kupitia ile amri, iliniua.
Gdyż grzech, wziąwszy przyczynę przez przykazanie, zawiódł mię i przez nie zabił mię.
12 Hivyo sheria ni takatifu, na ile amri ni takatifu, ya yaki, na njema.
A tak zakon jest święty i przykazanie święte, i sprawiedliwe, i dobre.
13 Hivyo basi ile iliyo njema ilikuwa mauti kwangu mimi? Isiwe hivyo kamwe. Lakini dhambi, ili ionekane kuwa ni dhambi hasa kupitia ile njema, ilileta mauti ndani yangu. Hii ilikuwa ili kwamba kupitia ile amri, dhambi izidi kuwa mbaya mno.
To tedy dobre stałoż mi się śmiercią? Nie daj tego Boże! I owszem grzech, aby się pokazał być grzechem, sprawił mi śmierć przez dobre, żeby się stał nader grzeszącym on grzech przez ono przykazanie.
14 Kwa maana twajua ya kuwa sheria asili yake ni ya rohoni, lakini mimi ni mtu wa mwilini. Nimeuzwa chini ya utumwa wa dhambi.
Bo wiemy, iż zakon jest duchowny, alem ja cielesny, zaprzedany pod grzech.
15 Maana nifanyalo, silielewi dhahiri. Kwa kuwa lile nilipendalo kutenda, silitendi, na lile nilichukialo, ndilo ninalolitenda.
Albowiem tego, co czynię, nie pochwalam; bo nie, co chcę, to czynię, ale czego nienawidzę, to czynię.
16 Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, nakubaliana na sheria ya kuwa sheria ni njema.
A jeźli czego nie chcę, to czynię, przyzwalam zakonowi, że dobry jest.
17 Lakini sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.
Już tedy teraz nie ja to czynię, ale grzech we mnie mieszkający;
18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani ndani ya mwili wangu, halikai jambo jema. Kwa kuwa tamaa ya lililo jema imo ndani yangu, lakini silitendi.
Gdyż wiem, że nie mieszka we mnie (to jest w ciele mojem) dobre; albowiem chęć jest we mnie, ale wykonać to, co jest dobrego, nie znajduję.
19 Kwa maana lile jema nilipendalo silitendi, bali lile ovu nisilolipenda ndilo nilitendalo.
Bo nie czynię dobrego, które chcę; ale złe, którego nie chcę, to czynię.
20 Sasa kama natenda lile nisilolipenda, si mimi binafsi nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.
A jeźliż ja to czynię, czego nie chcę, już ja więcej nie czynię tego, ale grzech, który we mnie mieszka.
21 Nimefahama, tena, imo kanuni ndani yangu ya kutaka kutenda lililo jema, lakini uovu hakika umo ndani yangu.
Znajduję tedy ten zakon w sobie, gdy chcę dobre czynić, że się mnie złe trzyma.
22 Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani.
Albowiem kocham się w zakonie Bożym według wewnętrznego człowieka.
23 Lakini naona kanuni iliyo tofauti katika viungo vya mwili wangu. Inapiga vita dhidi ya kanuni mpya katika akili zangu. Inanifanya mimi mateka kwa kanuni ya dhambi iliyo katika viungo vya mwili wangu.
Lecz widzę inszy zakon w członkach moich, odporny zakonowi umysłu mego i który mię zniewala pod zakon grzechu, który jest w członkach moich.
24 Mimi ni mtu wa huzuni! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?
Nędznyż ja człowiek! Któż mię wybawi z tego ciała śmierci?
25 Lakini shukrani kwa Mungu kwa Yesu Kristo Bwana wetu! Hivyo basi. Mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu. Bali, kwa mwili naitumikia kanuni ya dhambi.
Dziękuję Bogu przez Jezusa Chrystusa, Pana naszego. Przetoż tedy ja sam umysłem służę zakonowi Bożemu, lecz ciałem zakonowi grzechu.