< Warumi 6 >
1 Tuseme nini basi? Tuendelee katika dhambi ili neema iongezeke?
Que dirons-nous donc? Que nous devons demeurer dans le péché, afin que la grâce abonde?
2 La hasha. Sisi tuliokufa katika dhambi, tunawezaje tena kuishi katika hiyo?
Non certes! Nous qui sommes morts au péché, comment vivrions-nous encore dans le péché?
3 Je hamjui ya kuwa wale waliobatizwa katika Kristo walibatizwa katika mauti yake?
Ou bien, ignorez-vous que nous tous, qui avons été baptisés en Jésus-Christ, nous avons été baptisés en sa mort?
4 Tulikuwa tumezikwa pamoja naye kupitia ubatizo katika kifo. Hii ilifanyika ili kwamba kama vile Kristo alivyoinuliwa kutoka mauti kupitia utukufu wa Baba, ili kwamba nasi tuweze kutembea katika upya wa maisha.
Nous avons donc été ensevelis avec lui par le baptême en sa mort, afin que, comme Christ est ressuscité des morts par la gloire du Père, de même, nous aussi, nous vivions d'une vie nouvelle.
5 Maana ikiwa tumeunganishwa pamoja naye katika mfano wa kifo chake, pia tutaunganishwa katika ufufuo wake.
Car si nous sommes devenus une même plante avec lui par une mort qui ressemble à la sienne, nous le serons aussi par une résurrection semblable,
6 Sisi tunajua hivi, utu wetu wa zamani ulisulubiwa pamoja naye, ili kwamba mwili wa dhambi uharibiwe. Hii ilitokea ili kwamba tusiendelee kuwa watumwa wa dhambi.
sachant bien que notre vieil homme a été crucifié avec lui, afin que ce corps de péché soit détruit et que nous ne soyons plus asservis au péché.
7 Yeye aliyekufa amefanywa mwenye haki kulingana na dhambi.
Car celui qui est mort est libéré du péché.
8 Lakini kama tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pamoja naye pia.
Or, si nous sommes morts avec Christ, nous croyons que nous vivrons aussi avec lui,
9 Tunajua kwamba Kristo amefufuliwa kutoka katika wafu, na kwamba si mfu tena. Kifo hakimtawali tena.
puisque nous savons que Christ, ressuscité des morts, ne meurt plus: la mort n'a plus d'empire sur lui.
10 Maana kwa habari ya kifo alichokufa kwa dhambi, alikufa mara moja kwa ajili ya wote. Hata hivyo, maisha anayoishi, anaishi kwa ajili ya Mungu.
Car, s'il est mort, il est mort pour le péché une fois pour toutes; mais maintenant qu'il est vivant, il est vivant pour Dieu.
11 Kwa njia iyo hiyo, nanyi pia mnapaswa kujihesabu kuwa wafu katika dhambi, bali hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
Vous donc aussi, considérez-vous comme morts pour le péché et comme vivants pour Dieu, en Jésus-Christ.
12 Kwa sababu hiyo usiruhusu dhambi itawale mwili wako ili kusudi uweze kuzitii tamaa zake.
Que le péché ne règne donc point dans votre corps mortel, et n'obéissez pas à ses convoitises.
13 Usitoe sehemu za mwili wako katika dhambi kama vyombo visivyo na haki, bali jitoeni wenyewe kwa Mungu, kama walio hai kutoka mautini. Na zitoeni sehemu za miili yenu kama vyombo vya haki kwa Mungu.
Ne livrez pas vos membres au péché, comme des instruments d'iniquité; mais donnez-vous vous-mêmes à Dieu, comme étant devenus vivants, de morts que vous étiez, et offrez vos membres à Dieu comme des instruments de justice.
14 Msiiruhusu dhambi iwatawale. Kwa kuwa hamko chini ya sheria, bali chini ya neema.
Car le péché ne dominera point sur vous, parce que vous n'êtes plus sous la loi, mais sous la grâce.
15 Nini basi? Tutende dhambi kwa kuwa hatupo chini ya sheria, bali chini ya neema? La hasha.
Quoi donc! Pécherions-nous, parce que nous ne sommes pas sous la loi, mais sous la grâce?
16 Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa wenyewe kama watumishi ndiye ambaye ninyi mnakuwa watumishi wake, yeye mnayepaswa kumtii? Hii ni kweli hata kama ninyi ni watumwa katika dhambi ambayo inapelekea mauti, au watumwa wa utii unaopelekea haki.
Non certes! Ne savez-vous pas que si vous vous livrez à quelqu'un comme esclaves pour lui obéir, vous êtes les esclaves de celui à qui vous obéissez, soit du péché pour la mort, soit de l'obéissance pour la justice?
17 Lakini ashukuriwe Mungu! Kwa kuwa mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mmetii kutoka moyoni ile namna ya fundisho mliopewa.
Or, grâces soient rendues à Dieu de ce que, après avoir été esclaves du péché, vous avez obéi de coeur à la doctrine qui vous a été donnée pour règle
18 Mmefanywa huru kutoka kwenye dhambi, na mmefanywa watumwa wa haki.
Étant donc affranchis du péché, vous êtes devenus les esclaves de la justice.
19 Ninazungumza kama mtu kwa sababu ya madhaifu ya miili yenu. Kwa maana kama vile mlivyotoa viungo vya miili yenu kuwa watumwa kwa uchafu na uovu, kwa jinsi iyo hiyo, sasa toeni viungo vya miili yenu kuwa watumwa wa haki kwa utakaso.
— Je parle à la manière des hommes, à cause de la faiblesse de votre chair! — Ainsi, de même que vous avez mis vos membres au service de l'impureté et de l'iniquité, pour commettre l'iniquité, de même, maintenant, mettez vos membres au service de la justice, pour votre sanctification.
20 Kwa kuwa mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na haki.
En effet, lorsque vous étiez esclaves du péché, vous étiez libres à l'égard de la justice.
21 Kwa wakati huo, mlikuwa na tunda lipi kwa mambo ambayo kwa sasa mnaona aibu kwayo? Kwa kuwa matokeo ya mambo hayo ni kifo.
Quels fruits portiez-vous donc alors? Des fruits dont maintenant vous avez honte! Car la fin de ces choses-là, c'est la mort.
22 Lakini kwa kuwa sasa mmefanywa huru mbali na dhambi na mmefanyika watumwa kwa Mungu, mna tunda kwa ajili ya utakaso. Tokeo ni uzima wa milele. (aiōnios )
Mais maintenant, affranchis du péché et devenus les esclaves de Dieu, vous avez pour fruit la sanctification et pour fin la vie éternelle. (aiōnios )
23 Kwa kuwa mshahara wa dhambi ni mauti, bali zawadi ya bure ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōnios )
Car le salaire du péché, c'est la mort; mais le don de Dieu, c'est la vie éternelle en Jésus-Christ, notre Seigneur! (aiōnios )