< Warumi 6 >

1 Tuseme nini basi? Tuendelee katika dhambi ili neema iongezeke?
What, then, shall we say? Shall we continue in sin that grace may abound?
2 La hasha. Sisi tuliokufa katika dhambi, tunawezaje tena kuishi katika hiyo?
It can not be. How shall we that are dead to sin, live any longer in it?
3 Je hamjui ya kuwa wale waliobatizwa katika Kristo walibatizwa katika mauti yake?
Know you not that as many of us as were immersed into Christ Jesus, were immersed into his death?
4 Tulikuwa tumezikwa pamoja naye kupitia ubatizo katika kifo. Hii ilifanyika ili kwamba kama vile Kristo alivyoinuliwa kutoka mauti kupitia utukufu wa Baba, ili kwamba nasi tuweze kutembea katika upya wa maisha.
Therefore, we are buried with him, by immersion, into death, that as Christ was raised from the dead by the glory of the Father, so also we should walk in a new life.
5 Maana ikiwa tumeunganishwa pamoja naye katika mfano wa kifo chake, pia tutaunganishwa katika ufufuo wake.
For if we have become united to him by the likeness of his death, we shall certainly be united to him by the likeness of his resurrection;
6 Sisi tunajua hivi, utu wetu wa zamani ulisulubiwa pamoja naye, ili kwamba mwili wa dhambi uharibiwe. Hii ilitokea ili kwamba tusiendelee kuwa watumwa wa dhambi.
knowing this, that our former man has been crucified with him, in order that the sinful body may be deprived of its power, so that we should no longer serve sin:
7 Yeye aliyekufa amefanywa mwenye haki kulingana na dhambi.
for he that is dead is freed from sin.
8 Lakini kama tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pamoja naye pia.
Now if we have died with Christ, we believe that we shall also live with him;
9 Tunajua kwamba Kristo amefufuliwa kutoka katika wafu, na kwamba si mfu tena. Kifo hakimtawali tena.
because we know that Christ, having been raised from the dead, dies no more; death has dominion over him no longer;
10 Maana kwa habari ya kifo alichokufa kwa dhambi, alikufa mara moja kwa ajili ya wote. Hata hivyo, maisha anayoishi, anaishi kwa ajili ya Mungu.
for, as it regards his dying, he, once for all, died to sin; but as it regards his living, he lives to God.
11 Kwa njia iyo hiyo, nanyi pia mnapaswa kujihesabu kuwa wafu katika dhambi, bali hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
So also do you count yourselves as dead indeed to sin, but as living to God, in Christ Jesus our Lord.
12 Kwa sababu hiyo usiruhusu dhambi itawale mwili wako ili kusudi uweze kuzitii tamaa zake.
Therefore, let not sin reign in your mortal body so that you obey it;
13 Usitoe sehemu za mwili wako katika dhambi kama vyombo visivyo na haki, bali jitoeni wenyewe kwa Mungu, kama walio hai kutoka mautini. Na zitoeni sehemu za miili yenu kama vyombo vya haki kwa Mungu.
and present not your members to sin, as instruments of unrighteousness: but present yourselves to God, as alive from the dead; and your members to God, as instruments of righteousness.
14 Msiiruhusu dhambi iwatawale. Kwa kuwa hamko chini ya sheria, bali chini ya neema.
For sin shall not have dominion over you; for you are not under law, but under grace.
15 Nini basi? Tutende dhambi kwa kuwa hatupo chini ya sheria, bali chini ya neema? La hasha.
What then? Shall we sin, because we are not under law, but under grace? It can not be.
16 Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa wenyewe kama watumishi ndiye ambaye ninyi mnakuwa watumishi wake, yeye mnayepaswa kumtii? Hii ni kweli hata kama ninyi ni watumwa katika dhambi ambayo inapelekea mauti, au watumwa wa utii unaopelekea haki.
Know you not, that to whom you present yourselves as servants to obey, his servants you are whom you obey, whether of sin that leads to death, or of obedience that leads to righteousness?
17 Lakini ashukuriwe Mungu! Kwa kuwa mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mmetii kutoka moyoni ile namna ya fundisho mliopewa.
But thanks be to God, that though you were the servants of sin, yet you have obeyed from the heart the form of teaching, in which you have been instructed;
18 Mmefanywa huru kutoka kwenye dhambi, na mmefanywa watumwa wa haki.
and being made free from sin, you have become the servants of righteousness.
19 Ninazungumza kama mtu kwa sababu ya madhaifu ya miili yenu. Kwa maana kama vile mlivyotoa viungo vya miili yenu kuwa watumwa kwa uchafu na uovu, kwa jinsi iyo hiyo, sasa toeni viungo vya miili yenu kuwa watumwa wa haki kwa utakaso.
I speak of what is common among men, oil account of the weakness of your flesh: for as you have presented your members as servants to uncleanness, and to lawlessness, in order to lawlessness, so now present your members as servants to righteousness, in order to holiness.
20 Kwa kuwa mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na haki.
For when you were the servants of sin, you were free with respect to righteousness.
21 Kwa wakati huo, mlikuwa na tunda lipi kwa mambo ambayo kwa sasa mnaona aibu kwayo? Kwa kuwa matokeo ya mambo hayo ni kifo.
What fruit, therefore, had you at that time, in those things of which you are now ashamed? For the end of those things is death.
22 Lakini kwa kuwa sasa mmefanywa huru mbali na dhambi na mmefanyika watumwa kwa Mungu, mna tunda kwa ajili ya utakaso. Tokeo ni uzima wa milele. (aiōnios g166)
But now, since you have been made free from sin, and have become servants to God, you have your fruit to holiness, and the end, eternal life. (aiōnios g166)
23 Kwa kuwa mshahara wa dhambi ni mauti, bali zawadi ya bure ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōnios g166)
For the wages of sin is death; but the gift of God is eternal life in Christ Jesus our Lord. (aiōnios g166)

< Warumi 6 >