< Warumi 3 >

1 Kisha ni faida gani aliyo nayo Myahudi? Na faida ya tohara ni nini?
Šta je dakle bolji Jevrejin od drugijeh ljudi? Ili šta pomaže obrezanje?
2 Ni vyema sana kwa kila njia. Awali ya yote, Wayahudi walikabidhiwa ufunuo kutoka kwa Mungu.
Mnogo svakojako; prvo što su im povjerene rijeèi Božije.
3 Lakini, itakuwaje iwapo baadhi ya Wayahudi hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kutafanya uaminifu wa Mungu kuwa batili?
A što neki ne vjerovaše, šta je za to? Eda æe njihovo nevjerstvo vjeru Božiju ukinuti?
4 La hasha. Badala yake, acha Mungu aonekane kuwa kweli, hata kama kila mtu ni mwongo. Kama ilivyokuwa imeandikwa, “Ya kwamba uweze kuonekana kuwa mwenye haki katika maneno yako, na uweze kushinda uingiapo katika hukumu.”
Bože saèuvaj! nego Bog neka bude istinit, a èovjek svaki laža, kao što stoji napisano: da se opravdaš u svojijem rijeèima, i da pobijediš kad ti stanu suditi.
5 Lakini ikiwa uovu wetu unaonesha haki ya Mungu, tuseme nini? Mungu si dhalimu atoapo ghadhabu yake, je yupo hivyo? Naongea kutokana na mantiki ya kibinadamu.
Ako li nepravda naša Božiju pravdu podiže, šta æemo reæi? Eda li je Bog nepravedan kad se srdi? Po èovjeku govorim:
6 La hasha! Ni jinsi gani basi Mungu atauhukumu ulimwengu?
Bože saèuvaj! Jer kako bi mogao Bog suditi svijetu?
7 Lakini ikiwa kweli ya Mungu kupitia uongo wangu hutoa sifa tele kwa ajili yake, kwa nini ningali bado nahukumiwa kama mwenye dhambi?
Jer ako istina Božija u mojoj laži veæa postane na slavu njegovu, zašto još i ja kao grješnik da budem osuðen?
8 Kwa nini tusiseme, kama tulivyosingiziwa na kama wengine wanavyothibitisha kwamba tunasema, “Tufanye uovu, ili mema yaje”? Hukumu juu yao ni ya haki.
Zašto dakle kao što vièu na nas, i kao što kažu neki da mi govorimo) da ne èinimo zla da doðe dobro? Njima æe sud biti pravedan.
9 Ni nini basi? Tunajitetea wenyewe? Hapana kabisa. Kwa kuwa sisi tayari tumewatuhumu Wayahudi na Wayunani wote pamoja, ya kuwa wapo chini ya dhambi.
Šta dakle? Jesmo li bolji od njih? Nipošto! Jer gore dokazasmo da su i Jevreji i Grci svi pod grijehom,
10 Hii ni kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hata mmoja.
Kao što stoji napisano: ni jednoga nema pravedna;
11 Hakuna mtu ambaye anaelewa. Hakuna mtu ambaye anamtafuta Mungu.
Ni jednoga nema razumna, i ni jednoga koji traži Boga;
12 Wote wamegeuka. Wao kwa pamoja wamekuwa hawana maana. Hakuna atendaye mema, la, hata mmoja.
Svi se ukloniše i zajedno nevaljali postaše: nema ga koji èini dobro, nema ni jednoga ciglog.
13 Makoo yao ni kaburi lililo wazi. Ndimi zao zimedanganya. Sumu ya nyoka ipo chini ya midomo yao.
Njihovo je grlo grob otvoren, jezicima svojima varaju, i jed je aspidin pod usnama njihovima.
14 Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
Njihova su usta puna kletve i grèine.
15 Miguu yao ina mbio kumwaga damu.
Njihove su noge brze da proljevaju krv.
16 Uharibifu na mateso yapo katika njia zao.
Na putovima je njihovima raskopavanje i nevolja;
17 Watu hawa hawajajua njia ya amani.
I puta mirnoga ne poznaše.
18 Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yao.”
Nema straha Božijega pred oèima njihovima.
19 Sasa tunajua kwamba chochote sheria isemacho, husema na wale walio chini ya sheria. Hii ni ili kwamba kila kinywa kifungwe, na hivyo kwamba ulimwengu wote uweze kuwajibika kwa Mungu.
A znamo da ono što zakon govori, govori onima koji su u zakonu, da se svaka usta zatisnu, i sav svijet da bude kriv Bogu;
20 Hii ni kwa sababu hakuna mwili utakaohesabiwa haki kwa matendo ya sheria mbele za macho yake. Kwa kuwa kupitia Sheria huja ufahamu wa dhambi.
Jer se djelima zakona nijedno tijelo neæe opravdati pred njim; jer kroz zakon dolazi poznanje grijeha.
21 Lakini sasa pasipo sheria, haki ya Mungu imejulikana. Ilishuhudiwa kwa sheria na Manabii,
A sad se bez zakona javi pravda Božija, posvjedoèena od zakona i od proroka;
22 hiyo ni, haki ya Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo kwa wale wote wanaoamini. Maana hakuna tofauti.
A pravda Božija vjerom Isusa Hrista u sve i na sve koji vjeruju; jer nema razlike.
23 Kwa kuwa wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
Jer svi sagriješiše i izgubili su slavu Božiju,
24 Wamehesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
I opravdaæe se zabadava blagodaæu njegovom, otkupom Isusa Hrista.
25 Kwa maana Mungu alimtoa Kristo Yesu awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alimtoa Kristo kama ushahidi wa haki yake, kwa sababu ya kuziachilia dhambi zilizopita
Kojega postavi Bog oèišæenje vjerom u krvi njegovoj da pokaže svoju pravdu oproštenjem preðašnjijeh grijeha;
26 katika uvumilivu wake. Haya yote yalitokea ili kuonesha haki yake wakati huu wa sasa. Hii ilikuwa ili aweze kujithibitisha mwenyewe kuwa haki, na kuonesha kwamba humhesabia haki mtu yeyote kwa sababu ya imani katika Yesu.
U podnošenju Božijemu, da pokaže pravdu svoju u sadašnje vrijeme da je on pravedan i da pravda onoga koji je od vjere Isusove.
27 Kuwapi basi kujisifu? Kumetengwa. Kwa misingi ipi? Misingi ya matendo? Hapana, lakini kwa misingi ya imani.
Gdje je dakle hvala? Proðe. Kakijem zakonom? je li zakonom djela? Ne, nego zakonom vjere.
28 Hivyo tunahitimisha kwamba mtu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
Mislimo dakle da æe se èovjek opravdati vjerom bez djela zakona.
29 Au Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Je yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Ndiyo, wa mataifa pia.
Ili je samo Jevrejski Bog, a ne i neznabožaèki? Da, i neznabožaèki.
30 Ikiwa kwa kweli Mungu ni mmoja, atawahesabia haki walio wa tohara kwa imani, na wasiotahiriwa kwa njia ya imani.
Jer je jedan Bog koji æe opravdati obrezanje iz vjere i neobrezanje vjerom.
31 Je sisi twaibatilisha sheria kwa imani? La hasha! Kinyume cha hayo, sisi twaithibitisha sheria.
Kvarimo li dakle zakon vjerom? Bože saèuvaj! nego ga još utvrðujemo.

< Warumi 3 >