< Warumi 3 >

1 Kisha ni faida gani aliyo nayo Myahudi? Na faida ya tohara ni nini?
Was ist nun der Vorteil des Juden? oder was der Nutzen der Beschneidung?
2 Ni vyema sana kwa kila njia. Awali ya yote, Wayahudi walikabidhiwa ufunuo kutoka kwa Mungu.
Viel, in jeder Hinsicht. Denn zuerst sind ihnen die Aussprüche Gottes anvertraut worden.
3 Lakini, itakuwaje iwapo baadhi ya Wayahudi hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kutafanya uaminifu wa Mungu kuwa batili?
Was denn? wenn etliche nicht geglaubt haben, wird etwa ihr Unglaube [O. wenn etliche untreu waren, wird etwa ihre Untreue] Gottes Treue aufheben?
4 La hasha. Badala yake, acha Mungu aonekane kuwa kweli, hata kama kila mtu ni mwongo. Kama ilivyokuwa imeandikwa, “Ya kwamba uweze kuonekana kuwa mwenye haki katika maneno yako, na uweze kushinda uingiapo katika hukumu.”
Das sei ferne! Gott aber sei wahrhaftig, jeder Mensch aber Lügner, wie geschrieben steht: "Damit du gerechtfertigt werdest in deinen Worten, und überwindest, wenn du gerichtet wirst". [Ps. 51,4]
5 Lakini ikiwa uovu wetu unaonesha haki ya Mungu, tuseme nini? Mungu si dhalimu atoapo ghadhabu yake, je yupo hivyo? Naongea kutokana na mantiki ya kibinadamu.
Wenn aber unsere Ungerechtigkeit Gottes Gerechtigkeit erweist, was wollen wir sagen? Ist Gott etwa ungerecht, der Zorn auferlegt? [Ich rede nach Menschenweise.]
6 La hasha! Ni jinsi gani basi Mungu atauhukumu ulimwengu?
Das sei ferne! Wie könnte [Eig. wird] sonst Gott die Welt richten?
7 Lakini ikiwa kweli ya Mungu kupitia uongo wangu hutoa sifa tele kwa ajili yake, kwa nini ningali bado nahukumiwa kama mwenye dhambi?
Denn wenn die Wahrheit Gottes durch meine Lüge überströmender geworden ist zu seiner Herrlichkeit, warum werde ich auch noch als Sünder gerichtet?
8 Kwa nini tusiseme, kama tulivyosingiziwa na kama wengine wanavyothibitisha kwamba tunasema, “Tufanye uovu, ili mema yaje”? Hukumu juu yao ni ya haki.
und warum nicht, wie wir gelästert werden, und wie etliche sagen, daß wir sprechen: Laßt uns das Böse tun, damit das Gute komme? -deren Gericht gerecht ist.
9 Ni nini basi? Tunajitetea wenyewe? Hapana kabisa. Kwa kuwa sisi tayari tumewatuhumu Wayahudi na Wayunani wote pamoja, ya kuwa wapo chini ya dhambi.
Was nun? Haben wir einen Vorzug? [O. Schützen wir etwas vor] Durchaus nicht; denn wir haben sowohl Juden als Griechen zuvor beschuldigt, daß sie alle unter der Sünde seien, wie geschrieben steht:
10 Hii ni kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hata mmoja.
"Da ist kein Gerechter, auch nicht einer;
11 Hakuna mtu ambaye anaelewa. Hakuna mtu ambaye anamtafuta Mungu.
da ist keiner, der verständig sei; da ist keiner, der Gott suche.
12 Wote wamegeuka. Wao kwa pamoja wamekuwa hawana maana. Hakuna atendaye mema, la, hata mmoja.
Alle sind abgewichen, sie sind allesamt untauglich geworden; da ist keiner, der Gutes tue, [Eig. Güte übe] da ist auch nicht einer." [Ps. 14,1-3]
13 Makoo yao ni kaburi lililo wazi. Ndimi zao zimedanganya. Sumu ya nyoka ipo chini ya midomo yao.
"Ihr Schlund ist ein offenes Grab; mit ihren Zungen handelten sie trüglich." [Ps. 5,9] Otterngift ist unter ihren Lippen." [Ps. 140,3]
14 Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
"Ihr Mund ist voll Fluchens und Bitterkeit." [Ps. 10,7]
15 Miguu yao ina mbio kumwaga damu.
"Ihre Füße sind schnell, Blut zu vergießen;
16 Uharibifu na mateso yapo katika njia zao.
Verwüstung und Elend ist auf ihren Wegen,
17 Watu hawa hawajajua njia ya amani.
und den Weg des Friedens haben sie nicht erkannt." [Jes. 59,7. 8.]
18 Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yao.”
"Es ist keine Furcht Gottes vor ihren Augen." [Ps. 36,1]
19 Sasa tunajua kwamba chochote sheria isemacho, husema na wale walio chini ya sheria. Hii ni ili kwamba kila kinywa kifungwe, na hivyo kwamba ulimwengu wote uweze kuwajibika kwa Mungu.
Wir wissen aber, daß alles, was das Gesetz sagt, es denen sagt, die unter dem Gesetz sind, auf daß jeder Mund verstopft werde und die ganze Welt dem Gericht Gottes verfallen sei.
20 Hii ni kwa sababu hakuna mwili utakaohesabiwa haki kwa matendo ya sheria mbele za macho yake. Kwa kuwa kupitia Sheria huja ufahamu wa dhambi.
Darum, aus [O. verfallen sei, weil aus usw.] Gesetzeswerken wird kein Fleisch vor ihm gerechtfertigt werden; denn durch Gesetz kommt Erkenntnis der Sünde.
21 Lakini sasa pasipo sheria, haki ya Mungu imejulikana. Ilishuhudiwa kwa sheria na Manabii,
Jetzt aber ist, ohne [Eig. außerhalb, getrennt von] Gesetz, Gottes Gerechtigkeit geoffenbart worden, bezeugt durch das Gesetz und die Propheten:
22 hiyo ni, haki ya Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo kwa wale wote wanaoamini. Maana hakuna tofauti.
Gottes Gerechtigkeit aber durch Glauben an Jesum Christum [O. Glauben Jesu Christi] gegen alle und auf alle, die da glauben. Denn es ist kein Unterschied,
23 Kwa kuwa wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
denn alle haben gesündigt und erreichen nicht die [im Sinne von: reichen nicht hinan an die; ermangeln der] Herrlichkeit Gottes,
24 Wamehesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
und werden umsonst gerechtfertigt durch seine Gnade, durch die Erlösung, die in Christo Jesu ist;
25 Kwa maana Mungu alimtoa Kristo Yesu awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alimtoa Kristo kama ushahidi wa haki yake, kwa sababu ya kuziachilia dhambi zilizopita
welchen Gott dargestellt hat zu einem [O. als einem] Gnadenstuhl durch den Glauben an sein Blut, zur Erweisung seiner Gerechtigkeit wegen [O. in betreff] des Hingehenlassens der vorher geschehenen Sünden unter der Nachsicht Gottes;
26 katika uvumilivu wake. Haya yote yalitokea ili kuonesha haki yake wakati huu wa sasa. Hii ilikuwa ili aweze kujithibitisha mwenyewe kuwa haki, na kuonesha kwamba humhesabia haki mtu yeyote kwa sababu ya imani katika Yesu.
zur Erweisung seiner Gerechtigkeit in der jetzigen Zeit, daß er gerecht sei und den rechtfertige, der des Glaubens an Jesum [O. Glaubens Jesu] ist.
27 Kuwapi basi kujisifu? Kumetengwa. Kwa misingi ipi? Misingi ya matendo? Hapana, lakini kwa misingi ya imani.
Wo ist denn der Ruhm? Er ist ausgeschlossen worden. Durch was für ein Gesetz? Der Werke? Nein, sondern durch das Gesetz des Glaubens.
28 Hivyo tunahitimisha kwamba mtu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
Denn wir urteilen, daß ein Mensch durch Glauben gerechtfertigt wird, ohne [Eig. außerhalb, getrennt von] Gesetzeswerke.
29 Au Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Je yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Ndiyo, wa mataifa pia.
Oder ist Gott der Gott der Juden allein? Nicht auch der Nationen? Ja, auch der Nationen,
30 Ikiwa kwa kweli Mungu ni mmoja, atawahesabia haki walio wa tohara kwa imani, na wasiotahiriwa kwa njia ya imani.
sintemal es ein einiger Gott ist, der die Beschneidung aus Glauben [O. auf dem Grundsatz des Glaubens] und die Vorhaut durch den Glauben rechtfertigen wird.
31 Je sisi twaibatilisha sheria kwa imani? La hasha! Kinyume cha hayo, sisi twaithibitisha sheria.
Heben wir denn das Gesetz auf durch den Glauben? Das sei ferne! sondern wir bestätigen das Gesetz.

< Warumi 3 >