< Warumi 2 >

1 Kwa hiyo hauna udhuru, wewe uhukumuye, kwa maana katika yale uhukumuyo mwingine wajitia hatiani mwenyewe. Kwa maana wewe uhukumuye unafanya mambo yale yale.
Torej si neopravičljiv, oh človek, kdorkoli si, ki sodiš; kajti v čemer sodiš drugega, obsojaš sebe; kajti ti, ki sodiš, počneš iste stvari.
2 Lakini twajua kwamba hukumu ya Mungu ni ya kweli juu yao wafanyao mambo kama hayo.
Toda mi smo prepričani, da je Božja sodba, glede na resnico, zoper te, ki izvajajo takšne stvari.
3 Lakini wewe tafakari hili, wewe ambaye unahukumu wale wanaotenda mambo hayo ingawa nawe unafanya mambo yayo hayo. Je utaepuka hukumu ya Mungu?
In mar misliš ti, oh človek, ki sodiš tiste, ki takšne stvari počno in delaš isto, da boš ubežal Božji sodbi?
4 Au unafikiri kidogo sana juu ya wingi wa wema wake, kuchelewa kwa adhabu yake, na uvumilivu wake? Je, hujui kwamba wema wake unapaswa kukuelekeza katika toba?
Ali preziraš bogastva njegove dobrote in prizanašanja in potrpežljivosti, ne vedoč, da te Božja dobrota vodi h kesanju?
5 Bali kwa kadiri ya ugumu wako na kwa moyo wako usio na toba wajiwekea mwenyewe akiba ya ghadhabu kwa siku ile ya ghadhabu, yaani, siku ile ya ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu.
Toda po svojem brezčutnem in zakrknjenem srcu si nabiraš bes za dan besa in razodetja pravične Božje sodbe;
6 Yeye atamlipa kila mtu kipimo sawa na matendo yake:
ki bo vsakemu človeku povrnil glede na njegova dejanja.
7 kwa wale ambao kwa uthabiti wa matendo mema wametafuta sifa, heshima na kutokuharibika, atawapa uzima wa milele. (aiōnios g166)
Večno življenje tem, ki si s potrpežljivim vztrajanjem v dobrem ravnanju prizadevajo za slavo in čast in nesmrtnost; (aiōnios g166)
8 Lakini kwa wale ambao ni wabinafsi, wasioitii kweli bali hutii dhuluma, ghadhabu na hasira kali itakuja.
toda tistim, ki so prepirljivi in ne ubogajo resnice, temveč ubogajo nepravičnost, ogorčenost in bes.
9 Mungu ataleta dhiki na shida juu ya kila nafsi ya binadamu aliyefanya uovu, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
Stiska in tesnoba nad vsako dušo človeka, ki počne zlo, najprej judovsko in prav tako pogansko;
10 Lakini sifa, heshima na amani itakuja kwa kila mtu atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
toda slava, čast in mir vsakemu človeku, ki dela dobro, najprej Judu in tudi poganu,
11 Kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.
kajti pri Bogu ni oziranja na osebe.
12 Kwa maana kama vile wengi waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na kama vile wengi waliokosa kulingana na sheria watahukumiwa kwa sheria.
Kajti kolikor jih je grešilo brez postave, bodo tudi propadli brez postave; in kolikor jih je grešilo v postavi, bodo sojeni po postavi.
13 Maana si wasikiaji wa sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki.
(Kajti pred Bogom niso pravični poslušalci postave, temveč bodo opravičeni uresničevalci postave.
14 Kwa maana watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanafanya kwa asili mambo ya sheria, wao, wamekuwa sheria kwa nafsi zao, ingawa wao hawana sheria.
Kajti kadar pogani, ki nimajo postave, po naravi delajo stvari, ki so vsebovane v postavi, so tisti, ki nimajo postave, samim sebi postava;
15 Kwa hili wanaonesha kwamba matendo yanayohitajika kwa mujibu wa sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao. Dhamiri zao pia zinawashuhudia wao, na mawazo yao wenyewe ama huwashitaki au huwalinda wao wenyewe
ki kažejo delo postave, zapisano v njihovih srcih in tudi njihova vest pričuje in njihove misli se medtem obtožujejo ali pa opravičujejo druga drugo),
16 na pia kwa Mungu. Haya yatatokea katika siku ambayo Mungu atazihukumu siri za watu wote, sawasawa na injili yangu, kwa njia ya Yesu Kristo.
na dan, ko bo Bog po Jezusu Kristusu sodil skrivnosti ljudi, glede na moj evangelij.
17 Tuseme kwamba unajiita mwenyewe Myahudi, aliyekaa katika sheria, shangilia kwa kujisifu katika Mungu,
Glej, imenuješ se Jud in počivaš na postavi in se bahaš z Bogom
18 yajue mapenzi yake, na kupima mambo ambayo yanatofautiana nayo, baada ya kuagizwa na sheria.
in poznaš njegovo voljo in ker si poučen iz postave, odobravaš stvari, ki so odličnejše;
19 Na tuseme kwamba una ujasiri kwamba wewe mwenyewe ni kiongozi wa kipofu, mwanga kwa wale walio gizani,
in si prepričan, da si ti sam vodnik slepim, svetloba tem, ki so v temi,
20 msahihishaji wa wajinga, mwalimu wa watoto, na kwamba unayo katika sheria jinsi ya elimu na kweli.
inštruktor nespametnih, učitelj otročičev, ki imaš v postavi obrazec spoznanja in resnice.
21 Wewe basi, uhubiriye mwingine, je, hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kutokuiba, je wewe huiba?
Ti torej, ki poučuješ drugega, samega sebe [pa] ne poučiš? Ti, ki oznanjaš naj človek ne krade, [pa] kradeš?
22 Wewe usemae usizini, je unazini? Wewe uchukiaye sanamu, je unaiba hekaluni?
Ti, ki praviš, naj človek ne stori zakonolomstva, [pa] storiš zakonolomstvo? Ti, ki preziraš malike, [pa] storiš svetoskrunstvo?
23 Wewe ujisifuye katika sheria, je haumfedheheshi Mungu katika kuvunja sheria?
Ti, ki se bahaš s postavo, [pa] zaradi prelamljanja postave onečaščaš Boga?
24 Kwa maana “jina la Mungu linafedheheshwa kati ya watu wa mataifa kwa sababu yenu,” kama ilivyoandikwa.
Kajti zaradi vas se med pogani izreka bogokletje proti Božjemu imenu, kakor je pisano.
25 Kwa maana Kutahiriwa kweli kwafaa kama ukitii sheria, lakini kama wewe ni mkiukaji wa sheria, kutahiriwa kwako kunakuwa kutokutahiriwa.
Kajti obreza resnično koristi, če se držiš postave; toda če si lomilec postave, je tvoja obreza postala neobreza.
26 Basi, ikiwa, mtu asiyetahiriwa anaendelea kushika matakwa ya sheria, je kutokutahiriwa kwake hakutachukuliwa kana kwamba ametahiriwa?
Torej, če se neobrezani drži pravičnosti postave, mar ne bo njegova neobreza šteta za obrezo?
27 Na yeye asiyetahiriwa kwa asili hatakuhukumu kama akitimiza sheria? Hii ni kwa sababu una maandiko yaliyoandikwa na tohara pia lakini bado u mkiukaji wa sheria!
In ali ne bo neobrezani, ki je po naravi, če izpolnjuje postavo, sodil tebe, ki po črki in obrezi prestopaš postavo?
28 Kwa maana yeye si Myahudi aliye kwa hali ya nje; wala kutahiriwa si kule ambako ni kwa nje tu katika mwili.
Kajti ni Jud tisti, ki je tak na zunaj; niti ni obreza ta, ki je zunanja, v mesu;
29 Lakini yeye ni Myahudi aliye kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko. Sifa ya mtu wa namna hiyo haitokani na watu bali yatoka kwa Mungu.
toda Jud je tisti, ki je tak navznoter; in obreza je ta od srca, v duhu in ne po črki; katerega hvala ni od ljudi, temveč od Boga.

< Warumi 2 >